Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Meya wa New York aeleza hofu ya jamii za Wahamiaji kuhusu Trump
Meya wa New York kutoka chama cha Democratic, Bill de Blasio amesema kuwa amemwambia Donald Trump kwamba jamii za wahamiaji katika mji huo zinahofia juu ya hatua atakazozichukua dhidi yao.
Bwana Trump ametishia kuwarejesha makwao ama kuwafunga wahamiaji milioni tatu wenye historia ya uhalifu.
Mameya wa miji mingine ikiwemo Los Angeles na Washington wamesema kuwa watawalinda watu dhidi ya kurejeshwa walikotoka.