Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mwindaji aliyeua Simba aondolewa mashtaka Zimbabwe
Mahakama nchini Zimbabwe imetupilia mbali kesi dhdi ya muwindaji Theo Bronkhurst, inayohusu mauaji ya simba kwa Jina Cecil aliyeuawa mwaka 2015.
Simba huyo aliuawa na daktari raia wa Marekani mwezi Julai mwaka 2015, kisa ambacho kilishutumiwa kote dunaini.
Simba huyo wa umri wa miaka 13 amekuwa kivutio kikubwa kwa watalii kwenye mbuga ya kitaifa ya Hwange nchini Zimbabwe.
Zimbabwe ilimlaumu Theo Bronkhurst kwa kumhadaa Cecil kutoka nje ya mbuga hiyo, na kisha kuuawa na mwindaji akitumia mshale.
Cecil alikuwa amewekewa kifaa cha kumfuatilia cha GPS kwa utafiti na chuo cha Uingereza cha Oxford.
Mauaji ya Cecil yalisababisha kuanza kwa kampeni ya kimataifa ya kumaliza uwindaji wa Simba.