Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Vikosi vya Iraq vyakaribia kuudhibiti mji wa Mosul
Vikosi vya Iraq sasa vimebaki kilomita moja tu kudhibiti mji wa Mosul, mji wa mwisho kwa ukubwa nchini humo bado unadhibitiwa na wapiganaji wa Islamic State.
Vikosi maalum vinaelekea katika mji wa Mosul kutoka Mashariki walifanya mashambulizi kabla ya alfajiri.
Mwandishi wa BBC anayesafiri na safu ya kivita alisema wamekuwa wakilengwa mara kwa mara na wapiganaji wa kundi la IS waliokuwa wakiendesha magari yaliotegeshwa mabomu.
Lakini bado mafanikio ni makubwa na vikosi vya serikali vimesonga mbele hadi kijiji cha Bazwaya, nje kidogo ya mji wa Mosul.