Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Apple yaongeza bei ya laptopu na kompyuta zake
Kampuni ya teknolojia ya Apple imeongeza bei ya laptopu na kompyuta zake nchini Uingereza kwa pauni 100.
Siku ya Alhamisi ,kampuni hiyo ilizindua laptopu za Macbook Pro zikiwa na bei sawa na ile ya Marekani.
Lakini kampuni hiyo pia iliongeza bei ya tarakilishi zake ,ikiwemo ile ya Mac Pro ilio na miaka mitatu kwa pauni 100.
Mchanganuzi mmoja alisema kuwa wateja wanafaa kutarajia kuongezwa kwa bei hizo zaidi.