Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Marekani: Jaribio la roketi ya Korea Kaskazini lashindwa
Jeshi la majini la Marekani na lile la Korea Kusini, kwa pamoja yanasema kuwa, jaribio jingine la roketi ya Korea Kaskazini limeshindwa.
Wakorea Kusini wanasema kuwa, lililipuka mara tu baada ya kurushwa.
Kamanda mkuu wa jeshi la majini la Marekani Gary Ross, anasema kwamba uzinduzi huo uligunduliwa hapo jana Jumamosi karibu na mji wa Kusong.
Roketi hiyo inaaminika kuwa aina ya Musudan na yenye masafa marefu, na inayokisiwa kulipua umbali wa kilomita elfu tatu.
Korea Kaskazini haijasema lolote.