Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Ufisadi Nigeria: Majaji wanaswa na $800,000 nyumbani
Mamlaka kuu inasema kwamba imenasa zaidi ya dola elfu 800,000 katika sarafu tofauti pale ilipotekeleza uvamizi wa ghafla wa vita dhidi ya ufisadi, miongoni mwa majaji kadha waandamizi.
Pesa hizo zilizokuwa katika sarafu za Nigeria na kigeni, zilipatikana nyumbani kwa majaji hao ambao bado hawajatambuliwa.
Rais Muhammadu Buhari alizindua vita vikali dhidi ya ufisadi, huku akisema kuwa mabilioni ya dola yaliibwa muda mfupi kabla hajaingia mamlakani mwaka jana.
Lakini wakosoaji wake wanamlaumu kwa kuwalenga wapinzani wake wa kisiasa.