Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Haiti yakumbwa na kimbunga kikali
Kimbunga Matthew kimeharibu miundombinu muhimu kama vile barabara ambapo maafisa wanasema kuanguka kwa daraja kumegawa sehemu ya kusini na sehemu nyengine ya nchi.
Mtu mmoja mpaka sasa amepoteza maisha nchini Haiti na wengine wanne kutoka nchi jirani ya Jamuhuri ya Dominica.
Bado mpaka sasa haijafahamika kiwango cha uharibifu wa kimbunga hicho nchini Haiti, lakini nyumba nyingi zimebomolewa, huku barabara zikiwa hazipitiki kutokana na miti iliyoanguka pamoja na mafuriko.
Wahanga wa kimbunga hicho wanaendelea kujaa katika makazi yaliyotengwa na serikali katika mji mkuu wa Port-au-Prince huku mamlaka ikiendelea kuomba msaada wa maji pamoja na chakula.