Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Ali Bongo aapishwa kwa muhula wa pili
Rais wa Gabon Ali Bongo ameapishwa kwa muhula wa pili wa miaka saba kufuatia uchaguzi uliokumbwa na utata ambapo watu kadhaa waliuawa.
Kuapishwa huku kunafanyika siku tatu baada ya mahakama ya katiba kukataa shinikizo za upinzani za kutaka kura kuhesabiwa tena.
Ali Bongo ambaye babake Omar Bongo alikuwa rais wa Gaboin kwa miongo minne, alishinda uchaguzi huo kwa kura zisizozidi 6000.