Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Muhubiri anayepinga mapenzi ya jinsia moja afurushwa Botswana
Muhubiri mwenye utata anayepinga mapenzi ya jinsia moja kutoka Marekani Steven Anderson anafurushwa nchini Botswana na kurudishwa kwao Marekani.
Kulingana na gazeti la Mmegi katika ukurasa wake wa facebook,muhubiri huyo kwa sasa anazuiliwa katika idara ya uhamiaji na anangojea kurudishwa makwao.
Wiki moja iliopita Afrika Kusini ilimzuia bwana Anderson kutozuru taifa hilo kutokana na matamshi yake ya ukosoaji kuhusu mapenzi ya jinsia moja.
Waziri wa maswala ya ndani nchini humo anasema kuwa alikatazwa viza kwa sababu katiba ya taifa hilo inapinga matamshi ya chuki.
''Ninawaonea huruma watu wanaoishi Afrika Kusini,lakini nashkuru Mungu ,tuna fursa kubwa nchini Botswana'' ,Anderson alichapisha katika ukurasa wake wa facebook baada ya uamuzi wa kumkataza viza.