Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Boti illiojaa mahujaji yazama Thailand
Boti moja imezama baada ya kugonga daraja katikati mwa mji wa Thailand wa Ayutthaya,na kuwaua takriban watu saba akiwemo mtoto mmoja kulingana na vyombo vya habari vya eneo hilo.
Boti hilo lilikuwa likisafiri kupitia mto Chao Phraya wakati ajali hiyo ilipotokea.
Lilidaiwa kuwabeba zaidi ya watu 100 na huenda idadi ya waliofariki na wale waliotoweka ikaongezeka.
Ajali hiyo ilitokea karibu na hekalu la Wat Sanam Chai ,ambalo ni maarufu sana na watalii.
Abiria walikuwa wakisafiri kutoka Nonthaburi ,makaazi ya mji mkuu Bangkok kuelekea Ayutthaya kwa ibada ya dini ya Kiislamu kulingana na gazeti la the Bangkok Post.