Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Familia za wahanga wa shambulizi la Septemba 11 kuishitaki Saudi Arabia
Ikulu ya marekani imesema kuwa Rais Obama atapitisha muswada kwa bunge mbili za Marekani kuruhusu familia za wahanga waliokufa kwenye shambulizi la septemba 11 kuishtaki Saudi Arabia.
Msemaji wa ikulu Josh Earnest amesema kuwa kama muswada huo utakua sheria basi kuna uwezekano mkubwa nchi nyingine zitalipisha raia wa Marekani.
Mapema kundi la nchi sita za kiarabu ikiwemo Saud Arabia walionesha hisia zao kuhusu suala hilo na kusema kuwa ni kinyume na kanuni za sheria ya kimataifa.
Wahalifu 15 kati ya 18 waliohusika katika mashambulizi ya huko New York na Pennsylvania ni raia wa Saud Arabia.