Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Uturuki na Marekani kushambulia ngome ya IS Syria
Uturuki imekariri mpango wa Marekani kushirikiana nayo kufanya oparesheni ya pamoja kuwafurusha wanamgambo wa Islamic State kutoka mji wa Raqqa ambao ni ngome kuu ya wapiganaji hao nchini Syria.
Rais Reccep Tayyip Erdogan wa Uturuki amesema mazungumzo baina yake na Obama juu ya suala hilo,yanaendelea na kwamba taifa lake liko tayari kushirikiana naye.
Majeshi ya Uturuki yamekuwa yakiendeleza oparesheni kali Kaskazini mwa Syria dhidi ya waasi wa kikurdi.