Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wanachama wa ANC waandamana dhidi ya rais Zuma
Kundi moja la wanachama wa ANC nchini Afrika Kusini linapinga uongozi dhidi ya Jacob Zuma.
Wanayaita maandamano hayo #OccupyLuthuliHouse,wakitaja makao makuu ya chama hicho mjini Johannesburg,mji mkuu wa taifa hilo.
Lakini waandamanaji wamepunguza kasi ya maandamano yao baada ya usalama kuimarishwa.
Mwandishi wa BBC Nomsa Maseko ambaye yuko katika eneo la maandamano hayo anasema kuwa yanaendelea kuwa mabaya.
Ametuma ujumbe katika mtandao wa Twitter akisema wanajeshi wa zamani kwa jina uMkhonto we Sizwe,wanazuia waandamanaji kuingia katika afisi ya katibu mkuu wa ANC Gwede Mantashe.
Lakini wanajeshi hao wa zamani wamekuwa wakitumia nguvu.