Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Rais Mugabe awaonya mahakimu Zimbabwe
Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe, amewalaumu mahakimu wanaoruhusu maandamano dhidi ya serikali, ambayo baadae huwa na fujo.
Alisema mahakimu wanadharau amani, na akawaonya kutothubutu kuonesha dharau wanapofikia uamuzi.
Hapo kesho wafuasi wa upinzani watakwenda mahakamani, kupinga amri iliyopiga marufuku maandamano kwa majuma mawili.
Kiongozi mmoja wa upinzani, Tendai Biti, amemshutumu Rais Mugabe, kwamba anajaribu kuwatisha majaji.
Maandamano kadha ya fujo yamefanywa nchini Zimbabwe katika majuma ya karibuni, huku msukosuko wa kiuchumi ukizidi.