Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Ali Bongo: Komeni kuingilia maswala ya Gabon
Msemaji wa rais wa Gabon Ali Bongo ambaye anataka kuendelea kusalia mamlakani ameyataka mataifa ya kigeni kutoingilia maswala ya taifa hilo.
Amekishtumu chama cha kisosholisti cha rais Francois Hollande kwa kuegemea upande wa kiongozi wa upinzani Jean Ping mbali na kutaka kuingilia shughuli ya uchaguzi nchini Gabon.
Chama cha bwana Hollande kilitoa taarifa siku mbili zilizopita kikisema mabadiliko ya uongozi yatakuwa ishara na mfano mzuri.
Tayari rais wa Ivory Coast Allasane Outtara amemfuta kazi mshauri wake aneyetuhumiwa kuingilia shughuli za uchaguzi wa Gabon.
Tume ya uchaguzi nchini Gabon hatimaye imekutana mapema siku ya Jumatano ili kuanza kujumlisha matokeo kutoka maeneo tofauti ya taifa hilo.
Mkutano huo ulitarajiwa kufanyika hapo jana jioni.
Matokeo rasmi yatachelewa kwa siku moja.