Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
WhatsApp kugawana data na Facebook
Kamishna wa mawasiliano nchini Uingereza anachunguza uamuzi wa programu ya WhatsApp wa kugawana data na kampuni ya facebook.
Data hiyo ya watumiaji wa WhatsApp itatumiwa kuvutia matangazo yanayoonekana na watumiaji wa mtandao wa facebook.
Itagawana nambari za simu na maelezo ya mara ya mwisho mteja kuingia katika akaunti yake ya WhatsApp na facebook.
Kamishna huyo amesema kuwa kwa kuwa mabadiliko hayo yataathiri watu wengi ,anataka maelezo zaidi kuhusu kile kitakachogawanywa kati ya huduma hizo mbili.
Kamishna Elizabeth Denham amesema kuwa watumiaji watakuwa na maoni tofauti kuhusu mabadiliko hayo.