Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Zaidi ya raia wa Sudan Kusini 110,000 walitorokea Uganda
Shirika la Umoja wa mataifa la huduma kwa wakimbizi linasema kuwa takriban watu 110,000 wamekimbilia nchini Uganda kutoka taifa jirani la Sudan Kusini mwaka huu.
Linasema robo tatu ya wakimbizi hao waliwasili tangu yalipoibuka mapigano mapya ya mwezi uliopita.
Uganda inahangaika kukabiliana na wimbi hilo. Wakati mwingine vituo vya kupokelea wakimbizi hupokea mara tano ya idadi inayopaswa kupokelewa.
Umoja wa mataifa umesema matatizo ya kiuchumi Sudan Kusini, kunakosababisha mfumuko wa bei za bidhaa na kushuka kwa thamani ya sarafu ya nchi kwa asilimia 600%, inaongezea hali ya mzozo huo.