Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wageni 10 washikiliwa Uturuki wakihusishwa na mapinduzi
Uturuki imesema inawashikilia watu kumi wenye asili ya kigeni walioingia nchini humo kinyume na sheria, na kuhusika kwenye jaribio la kimapinduzi mwezi uliopita.
Raia hao wa kigeni hawajajulikana utaifa wao lakini serikali imesema mmoja wao alihukumiwa baada ya kuingia kinyemela akitokea nchini Syria.
Zaidi ya watu elfu kumi na nane wametiwa kizuizini wote wakihusishwa na kuhusika kwenye mapinduzi. Mhubiri mkuu Fethullah Gullen anatuhumiwa kuunga mkono mapinduzi hayo.