Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Kijana Mkenya aliyekaidi ulemavu kucheza soka ya kulipwa Uturuki
Kijana Mkenya aliyekaidi ulemavu kucheza soka ya kulipwa Uturuki
Wanamichezo wengi maarufu duniani wameshinda vikwazo vingi ikiwa ni pamoja na magonjwa na hata upasuaji kupata umaarufu.
Hata hivyo, kwa Mkenya Mohammed Munga, hali yake ya ulemavu imempa nguvu na ari ya kuwa mmoja wa wanasoka maarufu zaidi.
Munga anayeichezea timu ya taifa ya Kenya ya wachezaji wanaotumia magongo pia anacheza soka la kulipwa nchini Uturuki katika club ya Depsas huko Uturuki.
Mwandishi wa BBC Seif Abdalla Dzungu amezungumza na mchezaji huyo pamoja na familia yake na kutuandalia taarifa hii.
Video: Frank Mavura