Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Ney wa Mitego: Wakati mwingine sipewi vibali hata nikiandaa matamasha yangu
Ney wa Mitego: Wakati mwingine sipewi vibali hata nikiandaa matamasha yangu
Mashabiki wake hupenda kumuita 'rais wa kitaa', Emmanuel Elibariki, maarufu Nay wa Mitego ni miongoni mwa wasanii wa muziki nchini Tanzania ambaye tungo zake mara kadhaa zimemtia matatani kutokana na mamlaka za udhibiti wa maudhui kutoridhishwa na tungo zake.
Mwandishi wa BBC Veronica Mapunda amekutana na msanii huyo na kuzungumza naye masuala mbalimbali ikiwemo kwanini hutunga mashairi yanayomuweka matatani mara kwa mara?