Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
‘Lugha ya Kiswahili ni tamu’
“Lugha ya Kiswahili ni tamu… pia kuna maneno ambayo ukisema na kizungu, haivutii kama vile ukisema kwa Kiswahili”
Elliot Berry almaarufu kama ‘mzungu mwitu’ ama ‘mwalimu wa Kiswahili’ ni mzaliwa wa Uingereza lakini amepata umaarufu nchini Kenya kwa ujuzi wake wa lugha ya Kiswahili japokuwa lafudhi yake imeshangaza wengi kwani ni ya jamii ya Waluhya kutoka Magharibi mwa Kenya.
Mwanahabari wetu @judith_wambare aliwasiliana naye akiwa mjini London na kupata kujua kwanini anapendelea Kiswahili kama lugha yake rasmi ya mawasiliano na maoni yake kuhusu kutengwa kwa siku rasmi ya Kiswahili ambayo ni tarehe 7 mwezi wa Julai