Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
ANC chabwagwa uchaguzi wa Meya Johannesburg Afrika Kusini
Chama tawala nchini Afrika kusini ANC kimepoteza udhibiti katika jiji la Johannesburg ambapo meya mpya wa jiji hilo Herman Mashamba anatoka chama cha upinzani cha Democratic Alliance.
Chama cha ANC kipo madarakani tangu kipindi cha ubaguzi wa rangi nchini humo zaidi ya miaka 20.
Mashamba ameahidi kubadilisha utawala wa jiji.
ANC ilipoteza majimbo mengi katika uchaguzi wa mwezi uliopita lakini bado ni chama kikubwa na kikongwe nchini humo.