Israel yadai Iran iwekewe vikwazo dhidi ya mpango wake wa makombora
Huku kila mmoja akisubiri kuona jinsi Israel inavyoijibu kijeshi Iran, nayo inachukua hatua kidiplomasia.
Israel inaonekana kutengwa kidogo kwani angalizo sasa limepungua sana kwa Gaza na watakuwa na matumaini ya kufaidika na hili kuweka shinikizo la kimataifa kwa Iran.
Waziri wa mambo ya nje wa Israel amesema ameziandikia barua nchi 32 akitaka Iran iwekewe vikwazo zaidi. Hii ni pamoja na, alisema, vikwazo kwa mpango wa makombora wa Iran.
Msururu wa vikwazo vya Umoja wa Mataifa dhidi ya mpango wa makombora wa Iran uliisha Oktoba mwaka jana kwa sababu vilihusishwa na mapatano mapana zaidi kuhusu Mpango wa Nyuklia wa Iran.
Nchi zikiwemo Marekani, Uingereza na EU tayari zimedumisha vikwazo na kuongeza vingine vipya.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel pia alitoa wito kwa Jeshi la Ulinzi la Iran Islamic Revolutionary Guard Corps (IRGC) kutangazwa kuwa shirika la kigaidi.
Marekani tayari imefanya hivyo lakini Uingereza bado.
Mjadala kuhusu kufuata njia hii umekuwa mgumu na wenye mgawanyiko ndani ya serikali.
Wengine wanapendelea kupigwa marufuku na wengine wanapinga kwa sababu wanafikiri kuwa IRGC ni sehemu ya serikali badala ya shirika la kigaidi, na marufuku hiyo ingesababisha Iran kufunga njia za mawasiliano kati ya nchi hizo mbili.
Soma zaidi: