China yawanyonga wanandoa waliowatupa watoto 2 wachanga kutoka ghorofa ya 15
Uchina imewaua wanandoa ambao waliwatupa watoto wawili nje ya dirisha la jengo la ghorofa.
Zhang Bo - baba wa watoto - na Ye Chengchen hapo awali walipatikana na hatia ya kumuua msichana wa miaka miwili na mvulana wa mwaka mmoja mnamo 2020.
Zhang alikuwa ameanza uchumba na Ye na baadaye akatalikiana na mke wake, na kuanza kupanga njama ya kuwaua watoto wake.
Mahakama ya Juu ya Uchina ilikuwa imetaja nia za wanandoa hao kuwa "mbaya sana", ikiangazia "mbinu zao za kikatili".Wanandoa hao walinyongwa katika mji wa kusini-magharibi wa Chongqing siku ya Jumatano.
Haijabainika wazi jinsi mauaji hayo yalivyotekelezwa, ingawa hukumu za kifo nchini China mara nyingi hutekelezwa kwa kudungwa sindano ya kuua au kupigwa risasi.
Zhang alikuwa ameanza uhusiano "usiofaa" na Ye bila kumjulisha hali yake ya ndoa au ya mzazi, lakini Ye aliendelea kumuona baada ya kujua ukweli, mahakama ilisikiliza.
Baada ya Zhang kuachana na mkewe mnamo Februari 2020, Ye bado aliwaona watoto hao wawili kama "vizuizi kwake kuolewa na Zhang na mizigo kwa maisha yao ya baadaye pamoja".
Mara kwa mara walimshinikiza Zhang kutekeleza mauaji, ambayo walipanga njama kama kuanguka kwa bahati mbaya, mahakama ilielezwa Mnamo tarehe 2 Novemba 2020, Zhang aliwatupa watoto wake nje ya dirisha la nyumba yake kutoka ghorofa ya 15.