Lengo la Wagner PMC nchini Belarus ni kuivuruga NATO mashariki - Poland

Mamluki wa PMC ya Urusi "Wagner" walihamishiwa Belarus ili kuyumbisha upande harakati za NATO upande wa mashariki, amesema Waziri Mkuu wa Poland Mateusz Morawiecki.

Moja kwa moja

  1. Vita vya Ukraine: Lengo la Wagner PMC nchini Belarus ni kuivuruga NATO mashariki - Poland

    g

    Chanzo cha picha, VOENTV/BELARUSIAN DEFENCE MINISTRY VIA REUTERS

    Maelezo ya picha, Mwezi Julai picha ziliibuka zikidaiwa kuwaonyesha wapiganaji wa Wagner wakiwafunza wanajeshi wa Belarusi katika kambi ya kusini-mashariki mwa Minsk.

    Mamluki wa PMC ya Urusi "Wagner" walihamishiwa Belarus ili kuyumbisha upande harakati za NATO upande wa mashariki, amesema Waziri Mkuu wa Poland Mateusz Morawiecki.

    Aliongeza kuwa kulingana na makadirio ya Poland na Lithuania ambayo ni jirani, kuna mamluki wapatao 4,000 kutoka kundi la Wagner PMC nchini Belarus, ambao wanaweza kutumiwa kwa mashambulizi.

    "Lazima tujitayarishe kwa ukweli kwamba idadi za chokochoko zitaongezeka," Morawiecki alisema baada ya kukutana na Rais wa Lithuania Gitanas Nausėda.

    Siku ya Jumamosi, Morawiecki alisema kuwa zaidi ya mamluki 100 wa Wagner walioko Belarus walihamishiwa katika eneo la ukanda wa Suwalki (ukanda wa ardhi kati ya Belarusi na mkoa wa Kaliningrad, karibu kilomita 100, kwenye mpaka kati ya Poland na Lithuania.

    "Kundi la Wagner ni hatari sana, na vitengo vya kundi hili vinapelekwa kwenye eneo la mashariki linalodhibitiwa na NATO ili kuliyumbisha usalama," Morawiecki alisema.

    Belarus inakanusha kuwepo kwa mipango hiyo. Kiongozi wa Belarus Alexander Lukashenko alisema siku chache zilizopita kwamba Belarusi "haihitaji" ukanda wa Suwalki kwa miaka elfu: "Hatuendi kwenye ukanda huu."

    Baada ya kuonekana kwa kambi za mamluki za Wagner kwenye eneo la Belarus, viongozi wa Kipolishi waliamua kuimarisha vikosi vya wanajeshi wao kwenye mpaka wa mashariki, wakipeleka askari zaidi ya 1,000 kwenye mpaka wao wa mashariki.

    Vita vya Ukraine: Mengi zaidi:

    • YA MSINGI:Mzozo wa Ukraine: Kwanini Urusi inaivamia Ukraine na Putin anataka nini?
    • UFAFANUZI:Mzozo wa Ukraine: Swift ni nini na kwa nini kuipiga marufuku Urusi ni muhimu sana?
    • UCHAMBUZI:Mzozo wa Ukraine: Putin humsikiliza nani?
    • KWENYE RAMANI:Uvamizi wa Ukraine: Shambulio la Urusi kwenye ramani
    • ZELENSKY:Volodymyr Zelensky: Mfahamu rais wa Ukraine aliyeacha umaarufu wake wa TV na kuingia kwenye siasa
    • PUTIN:Vladimir Putin: Rais wa Urusi aliyeagiza shambulio Ukraine
  2. Uingereza: Waandamanaji wakamatwa baada ya kupanda juu ya paa la nyumba ya waziri mkuu

    g

    Chanzo cha picha, PA Media

    Maelezo ya picha, Wanaharakati wamefunika sehemu ya mbele ya jengo hilo kwa kitambaa cheusi

    Wanaharakati wamepanda juu ya paa la nyumba ya waziri mkuu katika eneo bunge lake la North Yorkshire kupinga vibali vipya 100 vya mafuta na gesi ya Bahari ya Kaskazini.

    Wanaharakati hao wa Greenpeace iwalisema walikuwa wamefunika "kitambaa cheusi cha mafuta" upande mmoja wa nyumba ya bw sunak Kirby Sigston, karibu na Northallerton.

    Ofisi ya Bw Sunak ilithibitisha kuwa yeye na familia yake hawakuwapo kwenye nyumba hiyo wakati wa tukio hilo.

    Wanaharakati wanne walitumia ngazi kulifikia paa kabla ya kutandaza kitamba kwenye jengo la makazi ya waziri mkuu, kuonyesha hisia zao juu ya athari za kibali hicho.

    Watu hao wanne walishuka saa saba na robo mchana kwa saa za Uingereza na mara moja wakawekwa ndani ya gari la polisi.

    Bw Sunak na familia yake wako likizoni huko California.

    h

    Chanzo cha picha, PA Media

    Mwenyekiti wa kamati ya mambo ya nje wa chama cha Conservative katika bungee la Uingereza Alicia Kearns alisema hatua hiyo "haikubaliki".

    Alisema nyumba za familia za wanasiasa hazipaswi "kushambuliwa".

    Mmoja wa waandamanaji hao, Philip Evans, aliiambia BBC: "Tuko hapa kumletea waziri mkuu madhara makubwa ya hali mpya ya kuchimba visima katika Bahari ya Kaskazini."

    Bw Evans alikataa kusema jinsi wanaharakati hao walivyoweza kuifikia nyumba hiyo.

  3. Mshukiwa sugu wa ulanguzi wa mihadarati anayesakwa awashukuru polisi kwa 'kumpa habari' katika jaribio la kumkamata

    g

    Chanzo cha picha, Reuters

    Sebastián Marset alirekodi video yake na kuituma kwa vyombo vya habari nchini Bolivia

    Mtu anayedaiwa kuwa mlanguzi wa dawa za kulevya, ambaye analengwa na msako wa kimataifa, ametuma video kwa vyombo vya habari ambapo anawashukuru polisi wa Bolivia kwa madai ya kumpa onyo la awali la jaribio la kumkamata.

    Siku ya Jumamosi, maafisa wa Bolivia walivamia nyumba ya Sebastián Marset, ambaye anatafutwa katika nchi yake ya asili ya Uruguay, na vile vile Brazil, Paraguay na Marekani. Lakini Bw Marset, 32, alifanikiwa kutoroka.

    Polisi wa Bolivia wamekana kumdokeza na kuendelea kumsaka.

    Zaidi ya maafisa wa polisi 2,250 wametumwa kumsaka lakini hadi sasa hawajafanikiwa kumkamata.

    g

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Baadhi ya makazi yaliyosakwa ni majumba ya kifahari

    Maafisa walikwenda kumkamata katika jiji la Bolivia la Santa Cruz siku ya Jumamosi lakini walinzi wa Bw Marset walimkamata mmoja wao na mwanamume anayetafutwa alifanikiwa kutoroka pamoja na mkewe na watoto wao.

    Polisi wamepekua jumla ya mali nane na kuwakamata watu kadhaa wanaoshukiwa kuwa na uhusiano na raia huyo wa Uruguay lakini hadi sasa wameshindwa kumpata.

  4. Mapinduzi ya Niger: Raia wa Uingereza waliohamishwa kutoka Niger wamefika salama Ufaransa

    g

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Baadhi ya nchi nyingine za Ulaya tayari zimeanza safari za ndege za uokoaji kutoka Niger

    Kundi la kwanza la raia wa Uingereza kuhamishwa kutoka Niger wamewasili salama mjini Paris.

    Naibu Waziri Mkuu Oliver Dowden alisema Waingereza 14 walisafirikwa ndege ya Ufaransa Jumatano kuyoka Niger.

    Wizara ya Mambo ya Nje ilisema "idadi ndogo sana ya raia wa Uingereza" wamesalia nchini humo.

    Ghasia zimezuka katika nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika kufuatia mapinduzi ya kijeshi ya wiki iliyopita.

    Mataifa yakiwemo Ufaransa na Italia yamepanga safari za ndege kwa ajili ya raia wao, ambazo pia zimesafirisha baadhi ya watu kutoka nchi nyingine.

    Uingereza bado haijapanga safari zake za ndege.

    Serikali ya Uingereza hapo awali ilikuwa iliwashauri raia wa Uingereza kutoa taarifa kuhusu mahali walipo na kusalia majumbani.

    Inaaminika kuwa kuna chini ya raia 100 wa Uingereza nchini Niger.

    Wa kwanza kuhamishwa walikuwa wale ambao walikuwa wameomba kuondoka Niger na waliweza kufika uwanja wa ndege kwa wakati, wakati ndege hiyo ilipoondoka.

    Taarifa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ilisema: "Balozi wa Uingereza na maafisa wengine muhimu wamesalia nchini Niger kusaidia idadi ndogo sana ya raia wa Uingereza ambao bado wako huko. Tunawashukuru Wafaransa kwa msaada wao katika uhamishaji huu."

  5. Zambia: Mkanganyiko kuhusu zaidi ya Wanyarwanda 200 waliofungwa

    G

    Watu kutoka eneo la Maziwa Makuu nchini Zambia hivi karibuni wamekamatwa na mamlaka ya usalama na uhamiaji, katika kile wanachosema ni msako mkali dhidi ya wahamiaji wasio na vibali.

    Hayo yalitokea Jumapili iliyopita, katika makanisa matatu katika mji mkuu Lusaka, eneo linaloitwa Mandevu.

    Innocent Rukundo, mratibu wa Chama cha Wanyarwanda wanaoishi Zambia, anasema kuwa kati ya zaidi ya watu 300 waliokamatwa, Wanyarwanda 210 bado wako gerezani.

    Anasema kuwa ni pamoja na wale ambao wamezuiliwa na wameonyesha hati za kuwa nchini Zambia.

    Waliokamatwa ni pamoja na "watu wazima na watoto", kulingana na Rukundo.

    Serikali ya Zambia haikuwa imetangaza hadharani kukamatwa kwa watu hawa.

    Katika ziara yake nchini Rwanda mwezi Juni (6) mwaka huu, Rais wa Zambia, Hakainde Hichilema, alifanya makubaliano na Rais wa Rwanda, Paul Kagame, ambayo ni pamoja na uhamiaji na uhamiaji. Haijulikani iwapo kukamatwa kwa watu hao kuna uhusiano wowote na makubaliano hayo.

    Katika mahojiano na BBC, Rukundo alisema: "Watu bado wamefungwa, na tunapojaribu kuwatembelea watu hawa, ni watu wa huzuni sana kwa sababu wameacha familia zao majumbani, wameacha watoto wadogo majumbani mwao, kwa hiyo. unaona kuwa inatia wasiwasi sana."

    Rukundo anasema baadhi ya aliozungumza nao walimweleza kuwa walikamatwa kwa sababu ni wakimbizi na hawana hati, lakini wanazo nyaraka na walizionyesha, wakasema wanazitoa lakini hawakuwa nazo. kuwatoa nje."

    g
    Maelezo ya picha, Innocent Rukundo, mratibu wa Chama cha Wanyarwanda Waishio Zambia, anasema kuwa kukamatwa kwao "kunatia wasiwasi sana".

    Kulingana na Rukundo, kikomo cha saa 48 kilichowekwa na sheria ya Zambia kwa mtu kuwa chini ya ulinzi wa polisi tayari kimepitishwa.

    Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), ofisi yake mjini Lusaka, liliambia BBC kwamba kuna wakimbizi wa Rwanda 4,900 nchini Zambia, huku wakimbizi 9,400 wakiwa ni wa Burundi.

  6. Tazama video fupi: 'Toka nje ya boti - italipuka'

    Maelezo ya video, Michigan: Watu wawili waliokolewa baada ya kuruka kutoka kwa boti inayowaka

    Watu wawili waliokuwa kwenye boti, Traverse Bay, Michigan, walilazimika kuruka majini baada ya kuteketea kwa moto.

    Wanandoa waliokuwa wakisafiri karibu nao waliwaokoa wawili hao, baada ya kuwataka waingie ndani ya maji wakati moto ulipokuwa mkali sana. Ilihofiwa boti hiyo inaweza kulipuka wakiwemo.

    Wanandoa hao waliweza kuwatoa waendesha boti waliokuwa wamekwama kwenye maji kwa usalama

    Baadaye chombo cha dharura kilifika kwenye eneo la tukio na kuzima moto huo.

  7. Tazama : Nyoka yavamia uwanja wa mechi ya mchezo wa kriketi nchini Sri Lanka

    Maelezo ya video, Tazama : Nyoka yavamia uwanja wa mechi ya mchezo wa kriketi nchini Sri Lanka

    Nyoka mkubwa alivamia mechi ya Ligi Kuu ya Lanka mjini Colombo, Sri Lanka, na kusimamisha mchezo.

    Mnyama huyo anayeaminika kutokuwa na sumu hatahivyo alifukuzwa nje ya uwanja kabla ya mechi kati ya Galle Titans na Dambulla Aura kuendelea.

  8. Niger: Umati wa watu wakusanyika Niamey kuunga mkono mapinduzi ya kijeshi

    g

    Chanzo cha picha, AFP

    Watu wameanza kukusanyika katika uwanja mmoja katikati mwa Niamey, mji mkuu wa Niger, kuonyesha uungaji mkono wao kwa mapinduzi ya kijeshi ya wiki iliyopita.

    Katika maadhimisho ya uhuru wa nchi hiyo, muungano wa asasi za kiraia ulitoa wito kwa watu kujitokeza kukemea vikwazo vilivyowekwa na jumuiya ya kikanda ya Afrika Magharibi, ECOWAS.

    ECOWAS Inasema ikiwa rais Mohamed Bazoum hatarejeshwa inaweza kutumia nguvu.

    Karibu wote wanaokusanyika katika uwanja wa uhuru katika siku ya uhuru kwa ajili ya kuonyesha uungaji mkono wao ni vijana huku wakiwa na kauli mbiu za Ufaransa na bendera chache za Urusi.

    Licha ya kuonyesha uungaji mkono kwa watu waliompindua rais, wengi nchini Niger wanapinga mapinduzi hayo.

    Kuna mtazamo kwamba ilikuwa ni hatua ya wanajeshi waandamizi ambao walikuwa katika hatari ya kubadilishwa na kupoteza madaraka yao.

    Lakini sasa wakati wanatafuta kuhalalisha hatua yao, hisia za kupinga Ufaransa zinasikika.

    Matukio haya ni sawa na yale yaliyofanyika katika nchi za Mali na Burkina Faso ambapo viongozi wa mapinduzi wameimarisha uhusiano na Urusi.

    Soma zaidi:

    • Mapinduzi ya Niger: Viongozi wa Afrika Magharibi watishia kuingilia kijeshi
    • Mapinduzi Niger: 'Kwa nini naitaka Urusi na si Ufaransa'
  9. Somalia imemsimamisha kazi afisa michezo kwa sababu ya mwanariadha aliyekimbia kwa kasi ya chini

    g

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Somalia imemsimamisha kazi afisa wa michezo kwa upendeleo baada ya mwanariadha novice kuruhusiwa kushiriki mashindano ya kimataifa ya michezo.

    Nasra Abubakar Ali alichukua karibu mara mbili ya muda wa mshindi kumaliza mbio za mita 100 katika mashindano ya michezo ya Vyuo Vikuu vya Dunia yaliyofanyika nchini China.

    Uchunguzi wa wizara ya jijana na michezo ya Somalia ulifichua kuwa "si mtu mwanamichezo, wala si mkimbiaji".

    Mwenyekiti wa Shirikisho la Riadha la Somalia ameshutumiwa kwa kutumia vibaya mamlaka yake na kuiaibisha Somalia.

    Khadijo Aden Dahir alisimamishwa kazi kufuatia mkutano kati ya wizara ya michezo ya nchi hiyo na kamati yake ya kitaifa ya Olimpiki.

    Uchunguzi wao wa awali pia uligundua kuwa shirika la michezo linalojulikana kama Chama cha Michezo cha Chuo Kikuu cha Somalia halipo.

    Wizara hiyo ilisema itafuatilia hatua za kisheria dhidi ya mwenyekiti wa Shirikisho la Riadha la Somalia na wengine waliohusika na "udanganyifu" katika kikundi cha michezo.

    Haikufafanua zaidi uhusiano kati ya Bi Dahir na Bi Ali ni upi.

    Katika video ya tukio hilo, mwanariadha huyo akiachwa mbali na wanariadha wengine na mwishowe anakamilisha mbio kwa kuruka kwa furaha.

    Mwanariadha huyo alimaliza mbio kwa sekunde 21.81 - zaidi ya sekunde 10 nyuma ya mshindi wa mwisho.

    Waziri wa Michezo Mohamed Barre Mohamud alitaja tukio hilo kuwa la aibu.

    "Kilichotokea leo si uwakilishi wa watu wa Somalia... tunaomba radhi kwa watu wa Somalia," alisema.

    Ukweli kwamba aliripotiwa kuwa hakuwa na uzoefu wa awali wa kushindana umewafanya baadhi ya Wasomali kushangaa kwa nini alichaguliwa kushiriki mashindano hayo.

  10. Rwanda yawapokea wanafunzi wa udaktari wanaokimbia vita vya Sudan,

    h

    Kundi la wanafunzi wa udaktari kutoka Sudan wamekaribishwa nchini Rwanda kuendelea na masomo baada ya vita vya wenyewe kwa wenyewe kuzuka katikati ya mwezi Aprili.

    Chuo chao katika Chuo Kikuu cha Sayansi ya Tiba na Teknolojia kilizidiwa na kugeuzwa kambi ya wapiganaji katika mji mkuu, Khartoum, ambapo vikosi vya kijeshi na jeshi vinahusika katika vita vya kuwania madaraka.

    Wanafunzi 160 wa shahada ya kwanza, ambao walikuwa wamebakisha miezi minane kumaliza kozi yao, wamepewa nafasi, pamoja na wahadhiri wao, katika Chuo Kikuu cha Rwanda.

    Kikundi hicho, ambacho kinaundwa na wanawake, pia kitakuwa kikifanya mazoezi katika hospitali za mitaa.

    Mmoja wa wanafunzi, Dina Abdalrahim Obaid , aliambia hafla katika mji mkuu, Kigali, nini maana ya kukaribisha:

    j

    Tunaishukuru Rwanda kwa kutupatia hifadhi na fursa ya kuendelea na masomo yetu."

    Prof Mamoun Mohamed Ali Homeida , naibu chansela wa chuo kikuu cha Sudan, alisisitiza jinsi walivyojisikia bahati, kwani wanafunzi wengine wengi walikimbilia nchi tofauti "bila nafasi ya kuendelea na masomo". Msomi huyo aliongeza:

    g

    Tuliomba kuja Rwanda kwa sababu tunatumai kwamba vita vitakapomalizika, nchi yetu itahitaji madaktari."

    Wakiwa nchini Rwanda, wanafunzi hao wataendelea na mtaala wao wa Sudan lakini watafanya mafunzo katika hospitali za ndani, alithibitisha Didas Muganga Kayihura, makamu mkuu wa Chuo Kikuu cha Rwanda.

    Maafisa walisema kuwa madaktari waliofunzwa walitarajiwa kurejea nyumbani watakapomaliza - au kama mapigano bado yanaendelea, watapata fursa ya kufanya kazi nchini Rwanda au kwingineko.

    Mnamo 2021 shule ya bweni ya kibinafsi ya wasichana ilihamisha wanafunzi na wafanyikazi wake hadi Rwanda baada ya Taliban kuchukua madaraka nchini Afghanistan kupiga marufuku elimu ya juu kwa wasichana na wanawake.

    g
  11. Vita vya Ukraine: Raia wa Ukraine 10,749 wameuawa tangu vita vianze – Ukraine

    d

    Raia wa Ukraine 10,749 waliuawa, na wengine 15,599 wamejeruhiwa, vita vya vianze dhidi ya Ukraine kulingana na Ofisi ya Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Ukraine.

    “Tuna uthibitisho wa vifo vya raia 10,749 na majeruhi 15,599. Idadi hii inajumuisha watoto 499 waliouawa na watoto 1,090 waliojeruhiwa,” Yury Belousov, mkuu wa idara ya ofisi ya Mwendesha mashitaka mkuu wa Ukraine kwa ajili ya kupambana na uhalifu uliofanyika wakati wa vita, alisema katika mahojiano na Interfax-Ukraine.

    Aliziita takwimu hizi "ncha ya kilima cha barafu" na kuongeza kuwa zinaweza kuongezeka zaidi wakati Ukraine itakapopata tena udhibiti wa maeneo yanayokaliwa na Urusi.

    Katika ripoti yake ya hivi karibuni iliyotolewa mwezi Julai, Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Haki za Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa iliripoti kwamba, kwa mujibu wa data zao, watu 9,369 walikufa wakati wote wa vita vya Ukraine.

    Wakati huohuo, wataalam wa Umoja wa Mataifa walisema kwamba idadi ya vifo vya raia ni kubwa zaidi, kwa kuwa hawana habari sahihi za vifo kuhusu maeneo kama vile Mariupol, Lysychansk, Severodonetsk au Popasnaya, ambako maelfu ya watu waliuawa kutokana na ulipuaji wa mabomu wa Urusi na mapigano katika miji inayokaliwa na raia.

  12. Usalama waimarishwa kabla ya Donald Trump kufikishwa mahakamani

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Rais wa zamani wa Marekani Donald Trump atashtakiwa rasmi mahakamani siku ya Alhamisi kwa tuhuma za kupanga kubatilisha kushindwa kwake katika uchaguzi wa 2020.

    Usiku wa kuamkia kesi hiyo alikashifu kesi hiyo kama ushahidi wa "ufisadi, kashfa na kushindwa" kwa Marekani chini ya urais wa Joe Biden.

    Bw Trump tayari anakabiliwa na kesi nyingine mbili za uhalifu huku akifanya kampeni ya kurejea Ikulu ya Marekani mwaka ujao.

    Usalama umeimarishwa mjini Washington DC kwa ajili ya kusikilizwa kwa kesi hiyo siku ya Alhamisi.

    Vizuizi vya chuma vimewekwa nje ya mahakama ya shirikisho ambapo mashtaka dhidi ya Bw Trump yatasomwa rasmi.

    Miundo kama hiyo imewekwa karibu na majengo ya Capitol ya Marekani, ambapo wafuasi wa Trump walifanya ghasia mnamo Januari 2021, wakikerwa na matokeo ya uchaguzi.

    Huduma ya Siri, ambayo hutoa ulinzi kwa marais na marais wa zamani, ilitoa taarifa ikionya umma kuhusu "athari za muda mfupi za trafiki" katikati mwa Washington DC.

    Soma zaidi:

    • Trump kukabiliwa na kesi ya kula njama ya kubatilisha uchaguzi mahakamani
    • Trump ashtakiwa kwa jaribio la kubatilisha matokeo ya uchaguzi wa 2020
    • Je, Donald Trump anakabiliwa na mashtaka gani ya jinai kuhusu nyaraka za siri?
    • Mashitaka ya Donald Trump: Rais wa zamani wa Marekani kushtakiwa kwa kutoa pesa kununua kimya cha muigizaji wa filamu za utupu
    • ‘Trump alijua wafuasi wake walikuwa wamejihami na aliwataka wavamie bunge’
  13. AfroBasket ya Wanawake: Nusu fainali yaanza huku wenyeji Rwanda wakimenyana na Nigeria

    .

    Chanzo cha picha, bb

    Maelezo ya picha, Timu ya Rwanda ikisherehekea baada ya kufika nusu fainali kwa mara ya kwanza

    Kwa mara ya kwanza katika nusu fainali wenyeji leo wanamenyana na Nigeria mabingwa watetezi ambao bado hawajapoteza mchezo wowote katika mji mkuu wa Rwanda ambao ndio wenyeji Kigali.

    Jana usiku, Nigeria iliitoa Msumbiji kwa pointi 59 kwa 52 huku Rwanda ikiwasisimua maelfu ya mashabiki - ambao ni pamoja na Rais Paul Kagame katika uwanja wa Kigali Arena, kwa kumpiga mpinzani wake wa kimchezo na jirani yake Uganda kwa mabao 69 kwa 61.

    "Hakuna aliyewahi kufikia hilo hapo awali, na sisi tumeweza. Tutafanya kila linalowezekana kufika fainali. Tumejipanga kushinda yote", Sifa Ineza aliyefunga pointi 19 na kuipeleka Rwanda katika nusu fainali yake ya kwanza aliwaambia waandishi wa habari baada ya mchezo huo.

    1800 kwa saa za eneo wenyeji watamenyana na Nigeria huku Senegal, mabingwa mara 11, wakimenyana na Mali saa 2100.

    .
    Maelezo ya picha, Nigeria ikisherehekea baada ya kuitoa Msumbiji

    Leo, katika kufuzu kwa nambari 5 hadi 8 Cameroon itacheza na Guinea huku Uganda ikimenyana na Msumbiji.

  14. Travis King: Korea Kaskazini yathibitisha kwa mara ya kwanza kumshikilia mwanajeshi wa Marekani

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Korea Kaskazini imethibitisha kumshikilia Travis King katika jibu lake la kwanza kwa ombi la kupata taarifa kuhusu aliko mwanajeshi huyo wa Marekani, kamandi ya Umoja wa Mataifa imesema.

    Mwanajeshi huyo mwenye umri wa miaka 23 alivuka mpaka kutoka Korea Kusini tarehe 18 Julai akiwa katika ziara ya kuongozwa.

    Kamandi ya Umoja wa Mataifa ilikataa kufafanua zaidi kinachoendelea "ili kutoingilia juhudi zetu za kumrudisha nyumbani".

    Hata hivyo, jibu linaonyesha Pyongyang inaweza kuwa tayari kuanza mazungumzo.

    Kamandi ya Umoja wa Mataifa, ambayo inasimamia eneo lisilo na wanajeshi (DMZ), ilikuwa imetafuta habari kuhusu Travis King kwa kutumia laini yake ya simu kwa Jeshi la Korea Kaskazini katika eneo la Usalama la Pamoja.

    Awali, Korea Kaskazini ilikubali ombi hilo, lakini hii ni mara yao ya kwanza kujibu, na kuthibitisha kwamba mwanajeshi huyo wa Marekani yuko chini ya ulinzi wao.

    Korea Kaskazini haijakiri hadharani kumzuilia Travis King.

    Kabla ya kuvuka mpaka, King alitumikia kifungo cha miezi miwili gerezani huko Korea Kusini kwa mashtaka ya kumshambulia mtu. Aliachiliwa tarehe 10 Julai.

    Alitakiwa kurejea Marekani kwa ndege ili kukabiliana na kesi za kinidhamu, lakini aliweza kuondoka uwanja wa ndege na kujiunga na ziara hiyo.

    Yeye ni mtaalamu wa upelelezi ambaye alikuwa jeshini tangu Januari 2021 na alikuwa Korea Kusini kama sehemu ya zamu yake.

    Soma zaidi:

  15. Papa akutana na waathiriwa wa unyanyasaji wa kijinsia uliotekelezwa na makasisi Ureno

    .

    Chanzo cha picha, EPA

    Papa Francis amefanya mkutano wa faragha na waathiriwa wa unyanyasaji wa kijinsia wa makasisi katika ziara ya siku tano nchini Ureno.

    Katika taarifa yake, Vatikani ilisema kuwa mkutano huo ulifanyika Jumatano katika "mazingira ya usikilizaji mkubwa".

    Ripoti ya mwaka huu ilihitimisha kwamba angalau watoto 4,815 wamenyanyaswa nchini Ureno na kwamba Kanisa lilikuwa limetafuta "utaratibu" kuficha suala hilo.

    Katika ibada ya jioni mjini Lisbon, Papa alisema lazima Kanisa lisikilize "kilio cha uchungu cha waathiriwa".

    Aliongeza kuwa kashfa hiyo "inatuita kwenye utakaso wa unyenyekevu na unaoendelea" na kwamba hasira iliyoenea juu yake imechangia "kuongezeka kwa kujitenga na imani".

    Mkutano huo, uliofanyika katika ujumbe wa kidiplomasia wa Holy See nchini Ureno, ulijumuisha waathiriwa 13 wa unyanyasaji na ulidumu zaidi ya saa moja, Vatican ilisema.

    Viongozi wa Kanisa la Ureno wanaohusika na ulinzi wa watoto wadogo pia walihudhuria.

    Mnamo Februari, tume huru iliyoundwa na Kanisa Katoliki nchini Ureno ilichapisha ripoti iliyoandika uzoefu wa watu 564 ambao walisema wamenyanyaswa na makasisi au maafisa wengine wa Kanisa.

    Zoezi hilo - sawa na ukaguzi uliofanywa kwingineko barani Ulaya na Marekani - liliangalia kesi zilizoanza mwaka 1950.

    Mara nyingi, ushuhuda ulionyesha watoto wengine waliodhulumiwa, hivyo makadirio ya maelfu ya waathirika kwa jumla.

    Akiwasilisha ripoti hiyo, rais wa tume hiyo, daktari wa magonjwa ya akili ya watoto Pedro Strecht, alisema makadirio hayo yanawakilisha "kiwango cha chini kabisa" na kwamba "idadi hizi ni ncha tu ya barafu".

    Akitoa pongezi kwa waliowasiliana na tume hiyo kutoa ushahidi, alisema "wamethubutu kutoa sauti ya kunyamazisha".

    Papa Francis yuko nchini Ureno kuadhimisha Siku ya Vijana Duniani, tamasha la wiki moja la matukio ya kidini na kitamaduni ambayo huandaliwa na Kanisa kila baada ya miaka michache katika miji mbalimbali duniani.

    Soma zaidi:

  16. Trump kukabiliwa na kesi ya kula njama ya kubatilisha uchaguzi mahakamani

    Donald Trump

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Rais wa zamani wa Marekani Donald Trump anatarajiwa kushtakiwa rasmi katika kikao cha mahakama kwa tuhuma za kupanga kubatilisha kushindwa kwake katika uchaguzi wa 2020.

    Usiku wa kuamkia kushtakiwa alikashifu kesi hiyo kama ushahidi wa "ufisadi, kashfa na kushindwa" kwa Marekani chini ya urais wa Joe Biden.

    Usalama umeimarishwa mjini Washington DC kwa ajili ya kusikilizwa kwa kesi hiyo siku ya Alhamisi.

    Bw Trump tayari anakabiliwa na kesi nyingine mbili za uhalifu huku akifanya kampeni ya kuingia tena Ikulu ya Marekani mwaka ujao.

    Lakini kesi ya uchaguzi inaonekana kuwa mbaya zaidi kuliko zote.

    Katika ujumbe wenye herufi kubwa kwenye jukwaa lake la mawasiliano la Truth Social siku ya Jumatano, Bw Trump, ambaye alikuwa katika klabu yake ya gofu ya Bedminster, New Jersey, aliwashukuru wafuasi wake na kusema: "Sijawahi kuungwa mkono sana na chochote hapo awali."

    Katika nyadhifa zingine aliwashambulia wapinzani wanaowania urais wa Republican, akiwemo Makamu wake wa zamani wa Rais Mike Pence na Gavana wa Florida Ron DeSantis.

    Alirudia hoja yake kwamba Bw Pence alikuwa na mamlaka ya kisheria ya kusimamisha Bunge la Congress kuthibitisha ushindi wa Bw Biden mnamo Januari 6 2021, kesi ambazo zilitatizwa huku wafuasi wa Trump wakizua ghasia katika Ikulu ya Marekani.

    Bw Trump, 77, anatarajiwa kufika katika mahakama ya shirikisho huko Washington DC siku ya Alhamisi saa 16:00 EDT (20:00 GMT).

    Anatarajiwa kukana mashtaka.

    Ingawa ana chaguo la kuonekana kupitia video, inaeleweka kuwa atahudhuria ana kwa ana.

    Bw Trump amezuru jiji hilo mara moja pekee tangu kuondoka Ikulu ya White House.

    Tayari foleni ilikuwa ikipangwa Jumatano jioni nje ya jengo hilo.

    Soma zaidi:

    • Trump ashtakiwa kwa jaribio la kubatilisha matokeo ya uchaguzi wa 2020
    • Je, Donald Trump anakabiliwa na mashtaka gani ya jinai kuhusu nyaraka za siri?
    • Mashitaka ya Donald Trump: Rais wa zamani wa Marekani kushtakiwa kwa kutoa pesa kununua kimya cha muigizaji wa filamu za utupu
    • ‘Trump alijua wafuasi wake walikuwa wamejihami na aliwataka wavamie bunge’
  17. Uvamizi wa polisi nchini Brazil umesababisha vifo vya takriban watu 45

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Uvamizi wa polisi unaolenga magenge ya dawa za kulevya katika majimbo matatu ya Brazil umesababisha vifo vya takriban watu 45.

    Katika operesheni ya hivi punde mjini Rio de Janeiro, polisi walisema walijibu shambulizi la ufyatuaji risasi katika eneo la Complexo da Penha, na kuua takriban watu 10.

    Hapo awali, watu 16 walikufa katika mapigano wakati wa msako wa siku tano wa polisi katika jimbo la São Paulo, uliopewa jina la Operesheni Shield.

    Na katika jimbo la kaskazini-mashariki la Bahia, maafisa wanasema washukiwa 19 wameuawa tangu Ijumaa.

    Watu 58 walikamatwa wakati wa operesheni hiyo katika jimbo la São Paulo, iliyoanza baada ya afisa wa polisi wa kikosi maalum kuuawa siku ya Alhamisi katika mji wa pwani wa Guarujá.

    Polisi walinasa kilo 385 za dawa za kulevya, pamoja na bunduki, kulingana na vyombo vya habari vya ndani.

    Operesheni hiyo ya Guarujá ilikosolewa na Waziri wa Sheria wa Brazil Flavio Dino, ambaye alisema hatua iliyochukuliwa na polisi haikulingana na uhalifu uliofanywa.

    Wakati wa mahojiano siku ya Jumanne, gavana wa jimbo la São Paulo Tarcisio de Freitas alisema maafisa wawili wa polisi walikuwa miongoni mwa waliouawa wakati wa mapigano.

    Amnesty International ilisema uvamizi wa polisi wa Guarujá ulionyesha "dalili za wazi za kutaka kulipiza kisasi kwa kifo cha afisa wa polisi".

    Huko Rio de Janeiro, kiongozi wa ulanguzi wa dawa za kulevya na msafirishaji watu kwa njia haramu walikuwa miongoni mwa watu 10 waliouawa siku ya Jumatano, kulingana na ripoti za vyombo vya habari vya ndani.

    Walioshuhudia waliambia vyombo vya habari kwamba walisikia milio kadhaa ya risasi na mapigano kati ya wanachama wa genge waliokuwa na silaha nzito na polisi.

    Pia unaweza kusoma:

  18. Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau na mkewe Sophie watengana

    Sophie and Justin Trudeau

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau na mkewe Sophie wanatengana baada ya miaka 18, kufuatia "mazungumzo yenye tija na magumu".

    Wanandoa hao walisema watasalia kuwa "familia ya karibu yenye upendo na heshima kubwa" katika mtandao wa Instagram.

    Walifunga ndoa huko Montreal mnamo 2005 na wana watoto watatu pamoja.

    Katika taarifa, afisi ya Bw Trudeau ilisema kwamba ingawa wenzi hao walikuwa wametia saini makubaliano ya kutengana bado watajitokeza hadharani.

    “Wamejitahidi kuhakikisha kuwa hatua zote za kisheria na kimaadili kuhusiana na uamuzi wao wa kutengana zimechukuliwa, na wataendelea kufanya hivyo kwa kusonga mbele,” ilisema taarifa hiyo na kuongeza kuwa watakuwa likizoni kama familia wiki ijayo.

    Wanandoa hao wameomba faragha kwa ajili ya "ustawi" wa watoto wao, Xavier, 15, Ella-Grace 14, na Hadrien, tisa.

    "Tunasalia kuwa familia ya karibu yenye upendo mkubwa na heshima kwa kila mmoja na kwa kila kitu ambacho tumejenga na tutaendelea kujenga," Bw Trudeau, 51, na Sophie Grégoire Trudeau, 48, walisema.

    Wameonekana pamoja hadharani mara chache sana katika miaka ya hivi karibuni, ingawa walihudhuria kutawazwa kwa Mfalme Charles III pamoja mwezi wa Mei na kumkaribisha Rais wa Marekani Joe Biden nchini Canada mwezi Machi.

    Wakati Bw Trudeau alipochaguliwa kuwa waziri mkuu kwa mara ya kwanza mwaka wa 2015, wanandoa hao walionekana kwenye jarida maarufu la Vogue ambapo aliliambia wakati wa mwisho wa chakula cha jioni baada ya siku yao ya kwanza kukutana alisema, "Nina umri wa miaka 31, na nimekuwa nikikusubiri kwa miaka 31".

    Katika ujumbe wa maadhimisho ya harusi kwenye Instagram mnamo Mei 2022, Bi Grégoire Trudeau aliandika kuhusu changamoto za mahusiano ya muda mrefu, akisema "tumepitia siku za jua, dhoruba kali, na kila kitu kilicho katikati".

    Bw Trudeau pia amezungumza kuhusu changamoto katika ndoa yao, akiandika katika wasifu wake wa 2014: "Ndoa yetu si kamilifu, na tumekuwa na misukosuko migumu, hata hivyo Sophie anabaki kuwa rafiki yangu mkubwa, mshirika wangu, mpenzi wangu. Ni waaminifu kwa kila mmoja, hata kama inaumiza."

    Wawili hao walianza kuchumbiana mnamo 2003, wakati Bi Grégoire Trudeau alipokuwa akifanya kazi kama mtangazaji wa TV.

    Pia anajulikana kwa kazi yake ya hisani kuhusu afya ya akili na matatizo ya ulaji.

    Bw Trudeau ndiye waziri mkuu wa pili wa Canada kutangaza kujitenga akiwa madarakani.

    Wa kwanza alikuwa baba yake, marehemu Pierre Elliott Trudeau, na mama Margaret Trudeau, ambao walitangaza kutengana kwao mnamo 1977 baada ya miaka sita pamoja. Baadaye waliachana.

  19. Marekani yatangaza uhamisho wa sehemu ya ubalozi wake Niger

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Marekani imeamuru kuhamishwa wa sehemu ya ubalozi wake nchini Niger kufuatia mapinduzi ya wiki iliyopita.

    Mamia ya raia wa kigeni tayari wamehamishwa kutoka nchini humo na siku ya Jumapili ubalozi wa Ufaransa ulishambuliwa na waandamanaji.

    Kiongozi wa mapinduzi Jenerali Abdourahamane Tchiani ameonya dhidi ya "uingiliaji wowote wa masuala ya ndani" ya nchi.

    Niger ni mzalishaji mkubwa wa madini ya uranium na iko kwenye njia kuu ya uhamiaji kwenda Afrika Kaskazini na Mediterania.

    Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken alizungumza na Rais aliyeondolewa madarakani, Mohamed Bazoum siku ya Jumatano, wizara ya mambo ya nje inasema, na kuongeza kuwa Marekani imejitolea kurejesha serikali iliyochaguliwa kidemokrasia ya Niger.

    Msemaji Matthew Miller alisema kuwa licha ya kuhamishwa kwa sehemu ya shughuli zake, ubalozi wa nchi hiyo katika mji mkuu Niamey utaendelea kuwa wazi.

    "Tunasalia kujitolea kwa watu wa Niger katika uhusiano wetu na tunaendelea kushirikiana kidiplomasia katika ngazi za juu," alisema.

    Marekani ni mfadhili mkuu wa misaada ya kibinadamu na usalama kwa Niger, na hapo awali ilionya kwamba mapinduzi hayo yanaweza kusababisha kusitishwa kwa ushirikiano wote.

    Ufaransa, ukoloni wa zamani nchini Niger, na EU tayari zimesitisha misaada ya kifedha na maendeleo.

    Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi (Ecowas), ya nchi 15 za Afrika Magharibi, imeweka vikwazo ambavyo ni pamoja na kusitishwa kwa miamala yote ya kibiashara na Niger na kuzuiwa kwa mali ya nchi hiyo katika benki kuu ya kikanda.

    Katika hotuba ya televisheni siku ya Jumatano, Jenerali Tchiani alisema serikali mpya ilikataa "vikwazo hivi kwa ujumla na inakataa kutii tishio lolote, popote linapotoka".

    Wakuu wa kijeshi kutoka Ecowas pia walikutana nchini Nigeria siku ya Jumatano kujadili uwezekano wa kuingilia kijeshi, ingawa walisema hatua kama hiyo itakuwa "suluhisho la mwisho".

    Jenerali Tchiani, mkuu wa zamani wa walinzi wa rais wa Bw Bazoum, alichukua mamlaka tarehe 26 Julai, akisema alitaka kuepusha "maangamizi ya taratibu na yasiyoepukika" ya Niger.

    Pia unaweza kusoma:

    • Mapinduzi Niger: 'Kwa nini naitaka Urusi na si Ufaransa'
    • Mapinduzi ya Niger mtihani wa demokrasia Afrika Magharibi
    • Mapinduzi ya Niger: Viongozi wa Afrika Magharibi watishia kuingilia kijeshi
    • Mapinduzi Niger: Makao makuu ya chama tawala yashambuliwa baada ya Rais Bazoum kuondolewa madarakani
    • Marekani yatoa 'msaada usio na kikomo' kwa rais aliyeondolewa madarakani Niger
  20. Hujambo na karibu katika matangazo yetu ya leo 03/08/2023