Waziri mpya wa usalama wa taifa wa mrengo mkali wa kulia wa Israel Itamar Ben-Gvir alizuru kwa muda mfupi eneo la msikiti wa Al-Aqsa mjini Jerusalem siku ya Jumanne, eneo ambalo pia linaheshimiwa na Wayahudi, na kusababisha kulaaniwa kutoka kwa Wapalestina na nchi jirani ya Jordan.
"Hekalu la Mlima liko wazi kwa wote," Ben-Gvir alisema kwenye Twitter, akitumia jina la Kiyahudi kwa eneo hilo.
Picha za video zilimuonyesha akitembea pembezoni mwa boma, akiwa amezungukwa ulinzi mzito.
Afisa mmoja wa Israel alisema ziara ya Ben Gvir ya dakika 15 katika eneo la Al Aqsa ilizingatia kile kinachoitwa mpangilio wa hali ilivyo, wa miongo kadhaa iliyopita, ambao unawaruhusu wasio Waislamu kuzuru kwa sharti la kutoswali.
Kujiunga kwa Ben-Gvir, kiongozi wa chama cha Jewish Power, kujiunga na muungano wa kidini-kitaifa chini ya Waziri Mkuu aliyechaguliwa tena Benjamin Netanyahu kumezidisha hasira ya Wapalestina kuhusu juhudi zao za muda mrefu za kupata taifa.
Wizara ya Mambo ya Nje ya Palestina ilisema "inalaani vikali kuvamiwa kwa msikiti wa Al-Aqsa na waziri mwenye itikadi kali Ben-Gvir na inaona kuwa ni uchochezi usio na kifani na ongezeko la hatari la mzozo".
Msemaji wa Hamas, kundi la Kiislamu la Palestina ambalo linakataa kuishi pamoja na Israel, alisema kuhusu ziara ya Ben-Gvir: "Kuendelea kwa tabia hii kutazileta pande zote karibu na mzozo mkubwa."
Mvutano kati yake na Israel ambao ulizidi kuwa ghasia katika eneo hilo mnamo Mei 2021 ulishuhudia Hamas wakirusha makombora kuelekea Jerusalem, na kusababisha mzozo wa siku 11 na Israel.
Ziara ya mwaka 2000 ya kiongozi wa mrengo wa kulia wa Israel Ariel Sharon, kiongozi wa upinzani wakati huo, iliwakasirisha Wapalestina. Ghasia zilizofuata ziliongezeka na kuwa maasi ya pili ya Wapalestina, au maarufu intifada.
Jumba la Al Aqsa, linalojulikana kwa Waislamu kama Patakatifu, ni eneo la tatu kwa Uislamu kwa utakatifu. Pia ni eneo takatifu zaidi la Uyahudi, mabaki ya mahekalu mawili ya kale ya imani.