Mtoto wa mbuzi mwenye masikio marefu apata umaarufu duniani
Kila mtu amesikia kuhusu Dumbo: kikaragosi cha tembo ambaye kutokana na masikio makubwa sana alidhihakiwa na wenzake na kulazimishwa sarakasi kali.
Dumbo sio mnyama pekee ambaye amepata umaarufu kwa kucheza michezo wa kuvuta vitu virefu.
Kutana na Simba - mtoto wa mbuzi kutoka Karachi, Pakistani ambaye masikio yake mawili yana urefu wa 54cm (21in) kila moja.
Na muda unavozidi kwenda. Badala ya kudhihakiwa, sasa amekuwa nyota ulimwengu: ameshinda mashindano ya urembo na maisha ya kupendeza.
Mfugaji wa mbuzi huyu ‘Simba’, Mohammad Hasan Narejo, aliliambia shirika la habari la AFP kwamba hata anakaribia kufika katika rekodi za dunia za Guinness.
Kwa sasa hakuna kipengele cha "mbuzi mwenye masikio marefu zaidi," kwa hivyo haijulikani ikiwa ni kweli masikio ya Simba yanavunja rekodi.
Iwe ni maskio mrefu zaidi duniani au la, mbuzi huyo tayari amekuwa mnyama mashuhuri kwenye mitandao ya kijamii nchini Pakistani baada ya picha za masikio yake ya kuvutia kuanza kusambaa.
Lakini pamoja na kuipandisha nyota ya mbuzi huyo, kuzaliwa na sifa hizo ndefu kunaleta changamoto za kipekee.
Kwa mfano, ukweli kwamba wao ni hatari kwa safari. Ili kuzuia ajali, Bw Narejo ameamua kukunja masikio ya Simba mgongoni mwake na pia amebuni uzi wa kuvaa unaofanya kazi hiyo hiyo.
Hofu nyingine ni wafugaji wanaoshindana, ambao umakini wao usiohitajika unamtia wasiwasi Bw Narejo. Amegeukia sala na desturi za kitamaduni ili kuzuia nia mbaya inayoweza kutokea kutoka kwa wengine.
"Tunamkariri aya za Kurani na kumpulizia ili kutupilia mbali jicho baya," aliiambia AFP.
Hatimaye, hata hivyo, mipango yake ni kabambe zaidi. Anataka kumkuza mbuzi huyu ili kutangaza taswira ya Pakistan kuwa kinara wa ufugaji wa mbuzi duniani.
- Je mbuzi anaweza kuendesha baiskeli ?
- Jinsi wanyama wanavyogundua majanga hata kabla yatokee
- Sababu inayochangia ndege wanaohama hufurika mijini