Polisi nchini Kenya wameanzisha msako mkali kwa waendesha bodaboda walionaswa kwenye kamera wakimshambulia dereva wa mjini Nairobi.
Katika video hiyo ya kutisha, mwanamke huyo anaonekana akipiga mayowe huku akijaribu kujinasua kutoka kwenye mikono ya wanaume hao ambao walikuwa wakijaribu kumvua nguo huku wengine wakiamuru atolewe ndani ya gari.
Genge hilo lilimmuweka nusu uchi mwakamke huyo.
Inadaiwa kuwa gari aliyokuwa anaendesha mwanamke huyo ilihusika kwenye ajali iliyohusisha mwendesha pikipiki, au boda boda, kama wanavyojulikana nchini Kenya.
Video hiyo imezua taharuki nchini humo. Wakenya mtandaoni wametaka hatua zichukuliwe na wanaharakati wakiishutumu serikali kwa kuruhusu uvunjaji wa sheria kuongezeka miongoni mwa waendesha pikipiki.
Inaelezwa kuwa waendesha bodaboda huendesha bila tahadhari na mmoja wao anapohusika kwenye ajali wengine hujitokeza kwa wingi na kuwashambulia na kuwatisha waendesha magari.
Mwaka 2020, kundi la waendesha pikipiki lilinaswa kwenye kamera likimshambulia dereva katika barabara kuu ya Thika baada ya kuripotiwa kumpiga mwenzao.
Tanzania yazungumza na Urusi ili kuwaondoa kwa usalama raia wake walioko Ukraine
Chanzo cha picha, Getty Images
Tanzania imesema imezungumza na Urusi kuhusu wanafunzi wake wanaosoma katika chuo kikuu cha Ukraine karibu na Kharkiv, vyombo vya habari nchini humo vimeripoti.
Ubalozi wa Tanzania mjini Moscow sasa umewataka raia wake wanaosoma katika Chuo Kikuu cha Sumy State mashariki mwa Ukraine kuelekea kwenye mpaka wa Urusi, kwa mujibu wa gazeti la kibinafsi la Mwananchi.
"Taarifa kutoka ubalozi wa Tanzania... alitoa wito kwa wanafunzi hao kuelekea Sudja ambako watapokelewa na jeshi la Urusi," ripoti hiyo imesema.
"Kutoka Sudja, watasafirishwa na jeshi kwenda Belgorod [nchini Urusi] ambako watakaribishwa na maafisa kutoka ubalozi wa Tanzania mjini Moscow kwa ajili ya kufanya maandalizi kabla ya kurejea nyumbani Tanzania," ilisema taarifa hiyo.
"Ubalozi pia umewashauri wanafunzi kuondoka chuoni hapo kwa makundi na kubeba bendera ya Tanzania kwa ajili ya utambulisho wakati wakipita katika ukanda salama," ilisema ripoti hiyo.
Tangazo la ukanda (njia) salama limekuja baada ya mazungumzo ya kidiplomasia na Urusi, ripoti hiyo imesema.
Televisheni ya binafsi ya ITV ilichapisha taarifa hiyo kutoka ubalozi wa Tanzania mjini Moscow. Haikufahamika mara moja ni wanafunzi wangapi wa Tanzania walioko Sumy. Gazeti la Mwananchi limeripoti kuwa zaidi ya wanafunzi 400 wa Kitanzania huko Odesa na 200 huko Kyiv tayari wamefanikiwa kuondoka Ukraine.
Mpatanishi wa Ukraine ataka kusitishwa kwa mashambulizi dhidi ya raia
Wakati duru ya tatu ya mazungumzo kati ya Urusi na Ukraine ikianza, mjumbe wa Ukraine Mykhailo Podolyak ameitaka Urusi kusitisha mashambulizi dhidi ya raia.
Katika ujumbe wa Twitter, anasema: "Katika dakika chache, tutaanza kuzungumza na wawakilishi wa nchi ambayo inaamini sana vurugu kubwa dhidi ya raia ni hoja. Kuthibitisha kwamba hii sio kesi."
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje
Mwisho wa X ujumbe
Habari za hivi punde, Urusi yatoa masharti ya kusitisha vita Ukraine
Chanzo cha picha, Getty Images
Urusi imesema kuwa inaweza kusitisha operesheni "wakati wowote" ikiwa Ukraine itatimiza masharti ya Urusi.
Msemaji wa Kremlin Dmitry Peskov amesema Ukraine lazima itambue Crimea kama Urusi, na Donetsk na Luhansk kama mataifa huru.
Mbali na hayo, Peskov anasema Ukraine lazima irekebishe katiba yake na kukataa madai ya kuingia katika kambi yoyote (kama vile Nato, kwa mfano).
Anaongeza kuwa Urusi itamaliza "kuondoa jeshi" kwa Ukraine, na ikiwa masharti haya yatatimizwa hatua za kijeshi za Urusi "zitakoma mara moja".
Msemaji wa Kremlin amesisitiza kuwa Urusi haitaki kutoa madai yoyote zaidi ya eneo nchini Ukraine.
Rais wa Ukraine atoa wito wa vikwazo zaidi dhidi ya Urusi
Chanzo cha picha, EPA
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky atoa wito wa vikwazo zaidi dhidi ya Urusi.
Akizungumza katika mkutano wake wa kila siku, Zelensky anasema uvamizi unaoendelea unaonesha kwamba "Urusi haijaacha mipango yake dhidi ya Ukraine" - kwa hivyo, anaongeza, "tunahitaji kifurushi kipya cha vikwazo".
Zelensky ametoa wito wa "kususia uuzaji nje wa Urusi, haswa kukataliwa kwa bidhaa za mafuta kutoka Urusi". Anaongeza kuwa hatua hizi kali "zinaweza kuitwa zuio, au maadili tu".
Mawaziri wa mambo ya nje wa Urusi na Ukraine kukutana
Chanzo cha picha, Reuters
Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi Sergei Lavrov anatarajiwa kukutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ukraine Dmytro Kuleba siku ya Alhamisi mjini Antalya, Uturuki.
Mkutano huo unafanyika huku Urusi ikiendelea na uvamizi wake nchini Ukraine.
Ukraine inasema mashambulizi ya roketi yameendelea kwenye maeneo ya makazi katika miji kadhaa, na kwamba mji mkuu wa Kyiv unaweza kukabiliwa na mashambulizi ya kila namna.
Mazungumzo ya awamu ya tatu kuanza hivi karibuniAwamu ya tatu ya mazungumzo inatarajiwa kufanyika kati ya wapatanishi wa Ukraine na Urusi katika muda wa saa chache.
Sasa tumesikia zinatarajiwa kuanza saa 16:00 saa za Kyiv (14:00 GMT), kulingana na maafisa wa Ukraine
Marekani na washirika 'tayari kukabiliana na tishio lolote' - Blinken
Chanzo cha picha, EPA
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken, ambaye yuko kwenye ziara nchini Lithuania, anasema Urusi imejaribu "kudhoofisha demokrasia ya Lithuania na kusababisha mgawanyiko kwa mashambulizi ya mtandao na habari za upotoshaji ''.
Pia anasema Marekani na nchi mwenyeji wake "zimeungana katika azimio letu la kusimama na Ukraine", huku uvamizi wa Urusi ukifikia siku yake ya 12.
Marekani ilikuwa ikiimarisha "ulinzi wetu wa pamoja", anasema, hivyo Marekani na washirika wako tayari "kukabiliana na tishio lolote" - ikiwa ni pamoja na kutuma vikosi vingine 7,000 vya Marekani huko Ulaya, na kuweka upya vingine "kuipa nguvu Nato ". Katibu Blinken alisisitiza dhamira "takatifu" ya Marekani kwa kifungu cha 5 cha Nato - "shambulio dhidi ya mtu mmoja ni shambulio kwa wote" - akisisitiza: "Tutalinda kila nchi iliyo kwenye mwamvuli wa Nato."
Zelensky aapa kuwaadhibu wanaofanya ukatili dhidi ya Ukraine
Chanzo cha picha, Getty Images
Rais Volodymyr Zelensky amesema kila mtu atakayefanya ukatili dhidi ya raia wa Ukraine ataadhibiwa.
Amesema raia wa Ukraine hawatasamehe au kusahau, na kuwashutumu wanajeshi wa Urusi waliovamia na kufanya mauaji ya makusudi.
"Hakutakuwa na mahali pa utulivu Duniani kwako. Isipokuwa kaburi," rais alisema. Maafisa wa Ukraine wanasema Urusi inalenga shabaha kwa raia kote nchini, zikiwemo hospitali, vitalu na shule.
Lakini Urusi inakanusha kuwalenga raia, ikisema kuwa inatekeleza "operesheni maalum ya kijeshi" dhidi ya "wazalendo wa Kiukreni" na "Wanazi mamboleo".
Naibu Waziri Mkuu wa Ukraine Olha Stefanishyna aliiambia BBC kwamba, baada ya "upinzani mkali" kutoka kwa jeshi la Ukraine, kulikuwa na "operesheni kubwa" ya Urusi dhidi ya raia.
Siku ya Jumapili pekee, familia ya watu wanne waliuawa wakati vikosi vya Urusi vilipofyatua makombora kwa watu waliokuwa wakikimbia mzozo katika mji wa Irpin, kaskazini-magharibi mwa Kyiv.
Na katika mji wa bandari wa Mariupol, uhamishaji ulioahidiwa ulifutwa siku za Jumamosi na Jumapili huku kukiwa na mashambulizi mapya.
Baraza la jiji nchini humo lilisema uvamizi wa makombora wa Urusi ulifanya harakati salama za uhamishaji zisiwezekane. Urusi imevilaumu vikosi vya Ukraine.
Zaidi ya watu 4,300 wamekamatwa katika maandamano ya kupinga vita kote Urusi siku ya Jumapili, mashirika ya kutetea haki za binadamu na mamlaka ya Urusi yanasema.
Watu wapatao 1,700 walizuiliwa huko Moscow pekee, shirika la habari la Ria linaripoti, likinukuu wizara ya mambo ya ndani.
Kundi la haki za OVD-Info linasema kamata kamata hiyo ilifanyika katika miji 53.
Ingawa maandamano yamezidi kuzuiliwa katika miaka ya hivi karibuni, mikutano mingi imefanyika kote Urusi tangu uvamizi huo.
Katika siku 11 zilizopita, zaidi ya watu 10,000 walizuiliwa kwenye maandamano, OVD-Info inasema.
Maria Kuznetsova, msemaji wa OVD-Info, aliliambia shirika la habari la Reuters kutoka Tbilisi nchini Georgia. "Tunaona maandamano makubwa leo - hata katika miji ya Siberia, ambapo ni mara chache tuliona idadi kama hiyo ya kukamatwa."
Urusi inasema inafungua njia mpya za kibinadamu katika miji mingi ya Ukraine, ikiwa ni pamoja na mji mkuu wa Kyiv, siku ya Jumatatu ili kuruhusu raia kuondoka - inakuja siku chache baada ya majaribio kama hayo huko Mariupol kushindwa baada ya kuendelea kwa makombora kutoka kwa vikosi vya Urusi wakati wa saa zilizokubaliwa za kusitisha mapigano, kulingana na Ukraine.
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ameishutumu Urusi kwa mauaji ya raia, baada ya shambulio la Urusi Jumapili huko Irpin kuua familia changa.
Maafisa wa ulinzi wa Ukraine wanadai kuwa vikosi vyao vimeuteka tena mji wa mashariki wa Chuhuiv
Kumekuwa na mashambulizi mapya ya Urusi kwenye mji wa bandari wa kusini wa Mykolaiv
Uingereza imesema itatoa $100m ya ziada (£74m) kwa Ukraine kusaidia serikali kuendelea wakati wa uvamizi wa Urusi.
Bei ya mafuta imepanda hadi kiwango cha juu zaidi tangu 2008 baada ya Marekani kusema kuwa inajadili vikwazo vinavyowezekana kwa usambazaji wa Urusi na washirika wake.
Habari za hivi punde, Urusi kusitisha mashambulizi ili kuruhusu raia kuondoka Ukraine
Chanzo cha picha, Reuters
Urusi itatoa nafasi ya huduma ya kibinadamu katika miji mingi ya Ukraine Jumatatu ili kuruhusu raia kuondoka, vyombo vya habari vya serikali vinaripoti.
Usitishaji huo wa mapigano utafanyika kuanzia saa 10:00 kwa saa za huko kwa mujibu wa Wizara ya Ulinzi ya Urusi, huku njia za uokoaji zikiwekwa katika mji mkuu wa Kyiv, pamoja na Kharkiv, Mariupol na Sumy.
Miji yote hii kwa sasa iko chini ya operesheni kubwa ya uvamizi wa Urusi.
Maafisa wa Kiukreni bado hawajathibitisha hili.
Mwishoni mwa juma, juhudi mbili za kufungua njia ya kuruhusu raia kuhama kutoka Mariupol kusini-mashariki mwa nchi hiyo zilisambaratika.
Maafisa wa Ukraine walisema hii ni kwa sababu Urusi iliendelea kuushambulia mji huo wakati wa saa zilizokubaliwa za kusitisha mapigano.
Raia wataelekea Belarus na Urusi
Njia za uokoaji zilizotangazwa na shirika la habari la RIA Novosti la Urusi zinaonesha raia wataweza kuondoka hadi Urusi na Belarus.
Njia ya kutoka Kyiv itaongoza hadi kwa mshirika wa Urusi Belarus, na raia kutoka Kharkiv watapita njia inayoelekea Urusi.
Njia ya kutoka miji ya Mariupol na Sumy itaelekea miji mingine ya Ukraine hadi Urusi, shirika la habari la AFP linaripoti.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Wanafunzi
wa Nigeria, Ghana na Somalia ni miongoni mwa mamia ya raia wa kigeni waliokwama
katika mji wa kaskazini-mashariki wa Sumy nchini Ukraine ambao umekuwa
ukishikiliwa na majeshi ya Urusi kwa siku kadhaa.
Hakuna
chakula sokoni, mashine za benki hazifanyi kazi na wanafunzi wanakunywa theluji
iliyoyeyushwa baada ya kukosa maji.
Mwanafunzi
wa Kihindi, Vipin Yadav, ambaye ni sehemu ya kundi lililokwama katika jiji
hilo, anakadiria takriban wanafunzi 1,300 wa kigeni bado wamenaswa huko - ikiwa
ni pamoja na watu kutoka Bangladesh, Pakistan na Uturuki.
Katika
mahojiano kwa njia ya simu, Bw Yadav aliambia mwandishi wa BBC Danny Aeberhard
kwamba hakuna chakula kwa muda wa siku nne hadi tano zilizopita.
Serikali
za Nigeria na Ghana zimekuwa zikiwarudisha nyumbani raia wao wanaokimbia mzozo
nchini Ukraine. Vikundi vya kwanza vilirudi nyumbani wiki iliyopita.
Zaidi ya
wanafunzi 1,000 wa Ghana walikuwa wakiishi Ukraine hadi Urusi ilipovamia nchi
hiyo. Taifa hilo la Afrika Magharibi hadi sasa limefanya misheni mbili za
kuwarejesha makwao.
Nigeria
inatarajiwa kuwahamisha raia 5,000 waliovuka kutoka Ukraine hadi nchi jirani za
Romania, Poland na Hungary.
Maafisa
wa ulinzi wa Ukraine wanadai kuwa vikosi vyao vimeuteka tena mji wa mashariki
wa Chuhuiv.
Katika taarifa
kuhusu operesheni iliyotumwa kwenye
Facebook Jumapili usiku, Mkuu wa jeshi la Ukraine alisema kwamba vikosi vya
Kyiv viliuteka mji huo kutoka kwa wanajeshi wa Urusi na kuvisababishia hasara
kubwa vikosi vya Moscow wakati wa vita.
Maafisa
wa Ukraine pia walidai kuwa makamanda wawili wa ngazi za juu wa Urusi waliuawa
wakati wa vita vya kuwania mji huo, ambao una idadi ya watu wapatao 31,000.
BBC
haiwezi kuthibitisha madai haya kwa uhuru.
Chuhuiv
iko katika eneo la kimkakati karibu maili 23 kutoka mji wa pili kwa ukubwa
nchini Ukraine Kharkiv, ambao umekuwa chini ya mashambulizi ya makombora makubwa kutoka kwa
vikosi vya Urusi kwa zaidi ya wiki.
Bei ya mafuta yapanda hadi kiwango cha juu zaidi tangu 2008
Chanzo cha picha, Getty Images
Bei ya
mafuta imepanda hadi kiwango cha juu zaidi tangu 2008 baada ya Marekani kusema
kuwa inajadili vikwazo vinavyowezekana kwa bidhaa za Urusi na washirika wake.
Brent
crude - alama ya kimataifa ya mafuta - ilipanda hadi zaidi ya $139 kwa pipa,
kabla ya kurudi chini hadi chini ya $130.
Masoko
ya nishati yametikiswa katika siku za hivi karibuni kutokana na hofu ya
usambazaji iliyosababishwa na uvamizi wa Urusi nchini Ukraine.
Wateja
tayari wanahisi athari ya gharama ya juu ya nishati kadiri bei ya mafuta na
bili za za majumbani zinavyoongezeka.
Masoko
ya hisa barani Asia yalishuka siku ya Jumatatu, huku kampuni za Nikkei za Japan
na Hang Seng huko Hong Kong zikishuka kwa zaidi ya 3%.
Siku ya
Jumapili, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken alisema utawala wa
Biden na washirika wake wanajadili vikwazo vya usambazaji wa mafuta ya Urusi.
Baadaye,
Spika wa Baraza la Wawakilishi la Marekani, Nancy Pelosi alisema baraza hilo
"linachunguza" sheria ya kupiga marufuku uagizaji wa mafuta ya Urusi
na kwamba Bunge la Congress wiki hii lilinuia kupitisha msaada wa $10bn
(£7.6bn) kwa Ukraine ili kukabiliana na uvamizi wa kijeshi wa Urusi.
"Kwa
sasa Bunge linachunguza sheria dhabiti ambazo zitatenga zaidi Urusi kutoka kwa
uchumi wa kimataifa," Bi Pelosi alisema katika barua.
Maoni
hayo yametolewa huku shinikizo zikiongezeka kwa Ikulu ya White House na mataifa
mengine ya Magharibi kuchukua hatua kali dhidi ya Moscow kutokana na uvamizi
wake nchini Ukraine.
Vikwazo
vya mafuta vya Urusi vitakuwa ongezeko kubwa katika kukabiliana na uvamizi wa
Ukraine na kunaweza kuwa na athari kubwa kwa uchumi wa dunia.
"Wakati
Marekani inaweza tu kusukuma marufuku ya uagizaji wa mafuta kutoka Urusi, Ulaya
haiwezi kumudu kufanya hivyo. Cha kusikitisha zaidi ni kwamba [kiongozi wa
Urusi Vladimir] Putin, ikiwa atasukumwa ukutani, anaweza kuzima usambazaji wa
gesi Ulaya, kukata njia ya nishati barani," Vandana Hari katika shirika la
ushauri la masoko ya nishati Vanda Insights aliambia BBC.
Ikiwa
unajiunga nasi, haya ndiyo ambayo huenda umekosa wakati uvamizi wa Urusi nchini
Ukraine unapoingia siku yake ya 12:
• Seneta
Marco Rubio, mgombea wa ngazi ya juu zaidi wa Republican katika Kamati ya
Ujasusi ya Seneti, aliiambia CNN Jumapili kwamba kuweka eneo la kutopaa ndege juu ya Ukraini bila shaka kutamaanisha
"kuanzisha Vita vya Tatu vya Dunia"
•
Maafisa wa ulinzi wa Uingereza wamesema wanaamini kuwa vikosi vya Urusi
vilipata mafanikio kidogo zaidi katika muda wa saa 48 zilizopita, huku
wanajeshi wake wakikabiliwa na upinzani mkali wa Ukraine na usaidizi duni wa
vifaa.
• Lakini
makamanda wa Ukraine wameonya kwamba vikosi vya Urusi vimekuwa vikijipanga upya
na vinajiandaa kufanya mashambulizi ya kila namna kwenye mji mkuu Kyiv.
• Vikosi
vya Moscow vimekuwa vikishambulia kwa nguvu miji ya pembezoni mwa jiji na
kusambaza tena tanki za mafuta zilizohamishwa kutoka Belarusi kwa ajili ya
kujiandaa kwa shambulio hilo, maafisa walisema.
• Katika
mji wa kusini-mashariki wa Mariupol, mashambulizi ya makombora ya Urusi yameua
makumi ya watu na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amewaonya wanajeshi wa
Moscow kwamba vikosi vyake vitamfuatilia mwanajeshi yeyote atakayefanya uhalifu
wa kivita hadi kaburini.
• Vikwazo
vya kiuchumi vinaendelea kulenga uchumi wa Moscow, huku Netflix, American
Express, KPMG na PricewaterhouseCoopers zikiwa miongoni mwa kampuni kuu za hivi
punde zaidi kusitisha huduma nchini Urusi.
Chanzo cha picha, Reuters
Marekani
imeripotiwa kumpa Zelensky simu salama
ya moja kwa moja hadi kwa Biden
Timu za
kijasusi za Marekani zinaripotiwa kufanya kazi ili kukatiza mashambulizi ya
kidijitali ya Urusi na mawasiliano, gazeti la New York Times linaripoti.
Kulingana
na gazeti la Times, wafanyakazi wa Kamandi ya Mtandao ya Marekani iliyoko
Marekani na Ujerumani wanatoa taarifa za kijasusi kutoka kwa picha za satelaiti
na miingiliano ya kielektroniki kwa wanajeshi wa Ukraini ndani ya "saa
moja au mbili" baada ya kukusanywa.
Marekani
pia imempatia Rais wa Ukraine Zelensky vifaa vya mawasiliano vilivyosimbwa kwa
njia fiche, na kumwezesha kumpigia simu Biden kwa njia salama, linaripoti
Times. Siku ya Jumamosi, Zelensky alipiga simu ya dakika 35 na Biden.
Siku ya
Alhamisi, katibu wa habari wa Ikulu ya White House, Jen Psaki alisema Marekani
ilikuwa ikishiriki taarifa za kijasusi na Ukraine "katika muda
halisi". Hakuna maelezo zaidi yaliyotolewa.
Maafisa
wa ulinzi wa Ukraine wameonya kuwa Urusi inatayarisha vikosi vyake kufanya
mashambulizi ya kila namna kwenye mji mkuu wa Kyiv.
Taarifa ya
Jenerali wa jeshi la Ukraine ilisema
kuwa vikosi vya Moscow vimeanza kukusanya rasilimali kwa ajili ya kushambulia
mji huo, huku vifaru na vitengo vya askari wa miguu vikiwa vinasonga mbele
kuelekea mji wa karibu wa Irpin kuweka msingi.
Taarifa
hiyo iliongeza kuwa makamanda wa Urusi wamekuwa wakivipatia vikosi vyao mafuta
yaliyosafirishwa kutoka Belarus kupitia eneo la kutengwa la Chernobyl.
Kwingineko,
maafisa waliripoti kuwa jeshi la Urusi lilikuwa likielekeza nguvu zake katika
kuzunguka miji ya mashariki ya Kharkiv, Chernihiv, Sumy na mji wa kusini wa
Mykolayiv.
Chanzo cha picha, Getty Images
Urusi
inaripotiwa kuwaajiri mamluki wa Syria
Urusi
inawaajiri Wasyria wenye ujuzi katika mapigano ya mijini kupigana nchini
Ukraine huku Moscow ikijiandaa kwa mapigano makali ya barabara hadi mtaa katika
harakati zake za kuteka miji mikubwa ya Ukraine, maafisa wa Marekani
wameliambia jarida la Wall Street Journal.
Maafisa
wa kijasusi walikataa kueleza chapisho hilo ni wapiganaji wangapi wamekubali
kujiunga na vita, lakini wakasema baadhi yao tayari wamesafiri hadi Urusi na
wanajiandaa kutumwa Ukraine.
Kulingana
na chapisho huko Deir Ezzor, Syria, Urusi imetoa wafanyakazi wa kujitolea
kutoka nchi hiyo mishahara ya kati ya $200 na $300 "kwenda Ukraine na
kufanya kazi kama walinzi" kwa miezi sita kwa wakati mmoja.
Maafisa
huko Moscow wanasemekana kuamini kutumwa kwa wapiganaji waliopata uzoefu kwa zaidi ya muongo mmoja wa vita vya mijini
katika Vita vya wenyewe kwa wenyewe vya Syria kunaweza kuongeza nguvu katika
vita vyao vya kunyakua miji muhimu ya Ukraine, ikiwa ni pamoja na mji mkuu wa
Kyiv.
Maveterani
wa kijeshi wa Israel wameripotiwa kujitokeza kupigania Ukraine.