Mpango wa kuahamisha wakazi Mariupol wasitishwa baada ya raia kuuawa karibu na Kyiv

Jaribio la pili la kuwahamisha watu waliokwama katika mji wa Mariupol uliozingirwa nchini Ukraine limekwama.

Moja kwa moja

  1. Putin na Macron wazungumza tena kwa simu

    Putin na Macron

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Rais wa Urusi Vladimir Putin na mwenzake wa Ufaransa Emmanuel Macron

    Rais wa Urusi Vladimir Putin na mwenzake wa Ufaransa Emmanuel Macron walizungumza tena kwa simu Jumapili, katika simu iliyochukua saa moja na dakika 45, ofisi ya rais wa Ufaransa inasema.

    Bado hatujapewa maelezo ya kile kilichojadiliwa. Viongozi hao walizungumza kwa njia ya simu siku ya Alhamisi, katika mazungumzo ambayo yalimwacha Macron na hisia kwamba lengo la Putin lilikuwa kuchukua Ukraine nzima, kulingana na afisa wa Ufaransa.

    Macron ni mmoja wa viongozi kadhaa wa dunia ambao wamezungumza na Putin siku za hivi karibuni wakitumai kukomesha mapigano nchini Ukraine.

    Mapema Jumapili, Putin alizungumza na Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan, ambaye aliomba kusitishwa kwa haraka kwa uhasama.

    Kulingana na msomaji wa Kremlin wa wito huo, Putin alimwambia Erdogan kwamba wapatanishi wa Ukraine wanapaswa kuzingatia "mbinu ya kujenga" zaidi katika mazungumzo, "kwa kuzingatia kikamilifu ukweli unaojitokeza".

    "Ilisisitizwa kuwa kusimamishwa kwa operesheni hiyo maalum kunawezekana tu ikiwa Kyiv itasimamisha shughuli za kijeshi na kutekeleza matakwa ya Urusi," ilisema Kremlin. Urusi imekuwa ikiita uvamizi wake "oparesheni maalum".

    • Urusi na Ukraine: No-fly zone-Inacho maanisha na kwanini nchi za magharibi haziwezi kuchukua hatua
    • Urusi na Ukraine: Nini kitatokea ikiwa Urusi itadhibiti maeneo yote ya Ukraine?
    • Ukraine ilitoka vipi kuwa nchi ya tatu kwa nguvu za nyuklia duniani hadi hali yake ya sasa
  2. Uvamizi wa Ukraine: Papa Francis apinga 'oparesheni maalum' ya Urusi

    Papa Francis amesema mzozo wa Ukraine "sio operesheni ya kijeshi bali ni vita", na kuitaja Ukraine kuwa "nchi iliyouawa" ambapo "mito ya machozi na damu inatiririka".

    Kauli yake inakemea msimamo rasmi wa Urusi inayosukumwa na Kremlin, ambayo inasisitiza uvamizi wake wa Ukraine ni "operesheni maalum ya kijeshi" iliyoanzishwa "kuondoa wanajeshi" Ukraine.

    Wiki iliyopita Papa alitoa wito wa kukomeshwa kwa mzozo huo, akitaka njia za kibinadamu zifunguliwe ili kuruhusu raia kukimbia.

    • Urusi na Ukraine: Nini kitatokea ikiwa Urusi itadhibiti maeneo yote ya Ukraine?
    • Ukraine ilitoka vipi kuwa nchi ya tatu kwa nguvu za nyuklia duniani hadi hali yake ya sasa
    • Urusi na Ukraine: No-fly zone-Inacho maanisha na kwanini nchi za magharibi haziwezi kuchukua hatua
  3. Uvamizi wa Ukraine: Wakazi watoroka kupitia njia ya wanajeshi wa Urusi

    Ajaza huyu anasaidiwa kuondoka Irpin, katika eneo la Kyiv

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Ajuza huyu anasaidiwa kuondoka Irpin, katika eneo la Kyiv

    Mji wa Irpin, kilomita 20 (maili 12) kaskazini-magharibi mwa Kyiv, umejikuta katikati ya makabiliano kati ya vikosi vya Urusi na Ukraine katika siku za hivi karibuni.

    Mji wa Irpin, uliopo kilomita 20, kaskazini -magharibi mwa Kyiv, umejipata katikati ya mapigano kati ya vikosi vya Urusi na Ukraine katika siku za hivi karibuni.

    Ni mji muhimu wa kimkakati uliopo karibu na uwanja wa ndege wa Hostomel, na msafara mkubwa wa magari ya Urusi yamepiga kambi karibu na mji mkuu.

    Nyumba za makazi na barbara zimeharibiwa vibaya kutokana na mashambulio ya angani. Vikosi vya Ukraine pia vipelipua madaraja katika juhudi za kudhibiti wanajeshi wa Urusi, ripoti zinaashiria.

    Treni ndiyo njia kuu ya kutoroka, kulingana na shirika la habari la Reuters, lakini mji huo unakabiliwa na mashambulizi ya mara kwa mara. Maafisa wa Ukraine walisema Jumamosi kwamba wanajeshi wa Urusi walilipua sehemu ya njia ya reli kwenye njia ya kuwahamisha kutoka Irpin.

    Umati wa watu umekuwa ukijaribu kutoka nje ya mji, licha ya madaraja kuharibiwa

    Chanzo cha picha, Reuters

    Wenyeji wanasema ndege za kivita za Urusi zinazunguka angani, na zimeshambulia kwa mabomu maeneo ya makazi

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Wenyeji wanasema ndege za kivita za Urusi zinazunguka angani, na zimeshambulia kwa mabomu maeneo ya makazi
  4. Uvamizi wa Ukraine: Zaidi ya watu milioni 1.5 wametoroka Ukraine - UN

    Zaidi ya watu milioni 1.5 wanaokimbia Ukraine wamevuka na kuingia katika nchi jirani katika siku 10 zilizopita, kamishna mkuu wa Umoja wa Mataifa wa wakimbizi Filippo Grandi anasema.

    Imekuwa mgogoro wa wakimbizi unaokua kwa kasi barani Ulaya tangu Vita vya Pili vya Dunia.

    Huku hayo yakijiri Naibu Waziri Mkuu wa Uingereza Dominic Raab amesema mzozo wa Ukraine unatarajiwa kudumu miezi kadhaa, ikiwa sio miaka, akizungumza na kituo cha habari cha Sky News, Bw. Raab alisema washirika wanahitaji kuonyesha "nguvu ya kimkakati" ili kuhakikisha kuwa Vladimir Putin wa Urusi anashindwa.

    • Urusi na Ukraine: Nini kitatokea ikiwa Urusi itadhibiti maeneo yote ya Ukraine?
    • Ukraine ilitoka vipi kuwa nchi ya tatu kwa nguvu za nyuklia duniani hadi hali yake ya sasa
    • Urusi na Ukraine: No-fly zone-Inacho maanisha na kwanini nchi za magharibi haziwezi kuchukua hatua
  5. Habari za hivi punde, Uvamizi wa Ukraine: Mapigano yasitishwa upya Mariupol - halmashauri ya jiji

    Mapigano yamesitishwa kwa muda huko Mariupol, mji wa bandari ulio kusini mwa Ukrainia, kuanzia saa 10:00-21:00 saa za huko (08:00-19:00 GMT), kulingana na baraza la jiji.

    Raia wataweza kuhama jiji hilo kwa njia iliyokubaliwa kutoka 12:00 saa za Urusi (10:00 GMT).

    Mpango sawia na huo uliotangazwa siku ya Jumamosi ulisambaratika muda mfupi baada ya kutangazwa, kutokana na mashambulizi mapya ya mabomu.

  6. Je, kusimamishwa kwa Visa na Mastercard kuna umuhimu gani?

    Huduma za Apple Pay nchini Urusi tayari zimetekelezwa

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Huduma za Apple Pay nchini Urusi tayari zimetekelezwa

    Kama ambavyo tumekuwa tukiripoti, makampuni makubwa ya malipo ya Visa na Mastercard yanajiondoa kwenye soko la Urusi kupinga uvamizi wake nchini Ukraini. Kwa pamoja, makampuni hayo mawili yanadhibiti 90% ya malipo ya mikopo na benki duniani, nje ya Uchina.

    Lakini hatua hiyo itakuwa na athari kwa Warusi wa kawaida?

    Benki kuu za Urusi tayari zimepunguza athari kwa wateja wao. Benki kuu ya Urusi ilisema kadi zote za benki za Visa na Mastercard zinazotolewa na benki za Urusi zitaendelea kufanya kazi kama kawaida nchini Urusi.

    Na Sberbank ilishikilia hilo, ikiongeza kwamba kadi zitafanya kazi "kutoa pesa, kufanya uhamisho kwa kutumia nambari ya kadi, na kwa malipo ya nje ya mtandao na pia katika maduka ya mtandaoni ya Urusi".

    Kadi zitaendelea kufanya kazi Urusi, benki hiyo ilisema, kwa sababu malipo yote nchini Urusi yanafanywa kupitia mfumo wa kitaifa na hayategemei mifumo ya kigeni.

    Hata hivyo, kadi za Mastercard au Visa zilizotolewa na Urusi hazitafanya kazi nje ya nchi, na kadi zilizotolewa na nchi za kigeni hazitafanya kazi nchini humo.

    • Mzozo wa Ukraine: Ni vikwazo gani vilivyowekwa dhidi ya Urusi?
    • Mzozo wa Ukraine: Swift ni nini na kwa nini kuipiga marufuku Urusi ni muhimu sana?
  7. Urusi imepoteza ndege 88 tangu kuanza kwa vita - Ukraine

    Mwanajeshi wa Ukraine

    Chanzo cha picha, EPA

    Maelezo ya picha, Mwanajeshi wa Ukraine

    Wizara ya ulinzi ya Ukraine imechapisha ripoti yake ya kila siku kuhusu mzozo huo. Haya hapa mambo muhimu:

    • Vikosi vya Urusi vimepoteza ndege na helikopta 88 tangu vita kuanza
    • Marubani kadhaa wa Urusi wamekamatwa.
    • Wanajeshi wa Ukraine wanaendelea kuulinda mji wa bandari wa Mariupol kusini-mashariki.
    • "Kiasi kikubwa" cha vifaa vya Urusi vilikamatwa katika mkoa wa Mykolaiv - kusini, karibu na Odesa.
    • Wanajeshi wa Urusi "wamevunjwa moyo" na nguvu ya upinzani Waukraine

    BBC haijafanikiwa kuthibitisha madai ya wanajeshi wa Ukraine wanadai. Urusi imetoa maelezo machache ya hasara iliyopatwa vikosi vyake nchini Ukraine lakini wataalam wa kijeshi wanatathmini kwamba imeshangazwa na nguvu ya upinzani wa Ukraine na imekumbwa changamoto ya kupata njia za usambazaji bidhaa na ari ya askari.

  8. Vita nchini Ukraine: Rais Zelensky awasihi Waukraine kuendelea na mashambulizi

    Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky

    Rais Volodymyr Zelensky amewaambia raia wa Ukraine "wamestahimili pigo" la uvamizi wa Urusi huku akiwataka raia kuendelea na mapigano.

    Nje ya mji mkuu wa Kyiv, msafara mkubwa unaoenea zaidi ya maili 40 (64km) umesalia kukwama nje ya mji huo na maafisa wa ulinzi wa Ukraine wanasema wamekuwa wakilenga maeneo maalum ndani ya msafara huo pale wanapoweza.

    "Mnahitaji kutoka nje na kutoa uovu huu nje ya miji yetu," alisema.

    Katika taarifa zingine:

    • Kumekuwa na mapigano makali kaskazini-magharibi mwa mji wa Kyiv katika mji uitwao Irpin, karibu na uwanja wa ndege wa kimkakati wa Hostomel na mkuu wa msafara wa Urusi.
    • Raia wamekuwa wakikimbia eneo hilo kwa miguu kujaribu kutafuta usalama
    • Maafisa wa Ukraine wanasema usitishwaji wa mapigano ulikubaliwa kuruhusu raia kuondoka mji wa bandari wa Mariupol ulioko kusini mwa nchi hiyo na ulidumu kwa dakika kadhaa siku ya Jumamosi kabla ya mashambulizi kuanza tena.
    • Urusi inachukulia eneo la kusini kuwa muhimu kwa mafanikio ya uvamizi wake na watu katika bandari ya Odesa wanaogopa kushambuliwa na Urusi kutoka baharini.
    • Miji ya Kharkiv na Sumy katika eneo la mashariki pia imekuwa ikishambuliwa upya kwa mabomu.
    • Urusi ilisema imesonga mbele kwa kilomita 7 (maili nne) katika mkoa wa Donbas, ikichukua miji na vijiji kadhaa.

    Taarifa zaidi kuhusu mzozo wa Ukraine:

    • Urusi na Ukraine: No-fly zone-Inacho maanisha na kwanini nchi za magharibi haziwezi kuchukua hatua
    • Urusi na Ukraine: Nini kitatokea ikiwa Urusi itadhibiti maeneo yote ya Ukraine?
    • Ukraine ilitoka vipi kuwa nchi ya tatu kwa nguvu za nyuklia duniani hadi hali yake ya sasa
  9. Uvamizi wa Ukraine: Urusi inalipua miji ili kuvunja ari ya Waukraine - Uingereza

    Mji wa Kharkiv umeshambuliwa vikali na vikosi vya Urusi

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Mji wa Kharkiv umeshambuliwa vikali na vikosi vya Urusi

    Mashambulizi ya Urusi katika maeneo yenye watu wengi nchini Ukraine ni juhudi za kuvunja ari, kulingana na wizara ya ulinzi ya Uingereza.

    Katika ripoti yake ya kila siku ya kijasusi, MoD inasema nguvu ya upinzani wa Ukraine inaendelea kushangaza Urusi, ambayo imejibu kwa kulenga miji ikiwa ni pamoja na Kharkiv, Chernihiv na Mariupol.

    Inalinganisha mkakati wa Urusi na kampeni zake nchini Syria mwaka wa 2016 na Chechnya mwaka 1999, wakati jeshi la Urusi lilipofanya mashambulizi makali ya maeneo yaliyojengwa.

    Ripoti hiyo pia inasema kwamba maendeleo ya Urusi yamepunguzwa na Ukraine kulenga laini zake za usambazaji.

    Inalinganisha mkakati wa Urusi na kampeni zake nchini Syria mwaka wa 2016 na Chechnya mwaka 1999, wakati jeshi la Urusi lilipofanya mashambulizi makali ya maeneo yaliyojengwa.Ripoti hiyo pia inasema kwamba maendeleo ya Urusi yamepunguzwa na Ukraine kulenga laini zake za usambazaji.

    Soma:

    • Urusi na Ukraine: No-fly zone-Inacho maanisha na kwanini nchi za magharibi haziwezi kuchukua hatua
    • Urusi na Ukraine: Nini kitatokea ikiwa Urusi itadhibiti maeneo yote ya Ukraine?
    • Ukraine ilitoka vipi kuwa nchi ya tatu kwa nguvu za nyuklia duniani hadi hali yake ya sasa
  10. Karibu katika matangazo ya moja kwa moja leo Jumapili 06.03.2022