Washirika wa Ukraine kuzungumzia mpango wa amani wa Marekani kwenye mkutano wa G20

Chanzo cha picha, PA Media
Washirika wa Ukraine watajitahidi "kuimarisha" mpango wa Marekani wa kumaliza vita na Urusi watakapokutana katika mkutano wa G20 nchini Afrika Kusini, Waziri Mkuu wa Uingereza Sir Keir Starmer amesema.
Mkutano huo unaanza siku moja baada ya Rais Volodymyr Zelensky kuonya Ukraine inakabiliwa na "moja ya nyakati ngumu zaidi katika historia yetu" juu ya shinikizo la kukubali mpango huo - maelezo yaliyofichuliwa ambayo yameonekana kupendelea Moscow.
Zelensky alizungumza kwa njia ya simu na Sir Keir na viongozi wa Ufaransa na Ujerumani siku ya Ijumaa. Baadaye, Waziri Mkuu alisema "marafiki na washirika" wa Ukraine walisalia kujitolea kupata "amani ya kudumu milele".
Si Rais wa Marekani Donald Trump au Rais wa Urusi Vladimir Putin wanaohudhuria mkutano wa G20.
Soma zaidi:







