'Fedha za USAID hazitumiki ipaswavyo', asema Mshauri wa Usalama wa Kitaifa wa Marekani
Mshauri wa Usalama wa Taifa nchini Marekani Mike Waltz amezungumza na NBC News kufuatia tangazo la Rais Donald Trump la kukata ufadhili wa Shirika la Misaada ya Kimataifa la Marekani (USAID).
Serikali ya Marekani imetangaza kusitisha ufadhili wa miradi ya misaada kwa siku 90 huku ikifanya "mapitio" ili kuhakikisha ufadhili huo unawiana na vipaumbele vya Rais Trump - hatua ambayo imekosolewa na wataalamu wengi wa afya duniani.
Waltz alisema kuwa "fedha hizo zinatolewa ili ziwafakie wanaohitaji usaidizi ", akiongeza kuwa "kati ya wakandarasi wakubwa, wakandarasi wadogo, na wakandarasi wa ndani, fedha hizo hazitumiki ipaswavyo".
"Tunahitaji kuangalia kwa makini (USAID). Tunahitaji kupiga hatua haraka," alisema, akiongeza kuwa lengo lao ni "kurekebisha" na "kuhakikisha kuwa fedha hizo zinatolewa kulingana na sera ya kigeni ya rais Trump.