Uturuki inasema Jamal Khashoggi 'aliuawa' alipoingia ubalozi wa Saudi Arabia nchini Uturuki

File photo of Jamal Khashoggi (8 May 2012)

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha, Jamal Khashoggi hajaonekana tangu siku ya Jumanne

Hofu inazidi kuongezeka kufuatia kutoweka kwa mwandishi wa habari Jamal Khashoggi baada ya maafisa wa Uturuki kusema wanaamini ameuawa.

Bw Khashoggi, raia wa Saudi Arabia alitoweka baada ya kuingia ubalozi wa Saudi Arabia mjini Insabul siku ya Jumanne.

Afisa mmoja wa Uturuki aliiambia BBC kuwa uchanguzi wa awali ulionyesha kuwa aliuawa huko.

Saudi Arabia imekana madai hayo na kusema kuwa imeanza kumtafuta.

Mwandishi wa BBC mjini Istabul Mark Lowen, alisema hii itachangia uhusiano kati ya Saudi Arabia na Uturuki kuwa mbaya zaidi.

Saudi consulate in Istanbul, Turkey (3 October 2018)

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Ubalozi wa Saudi Arabia unasema Khashoggi aliondoka ubalozini humo l

Maafisa wa Uturuki wameanzisha uchunguzi na wamekuwa wakizungumza na vyombo vya habari.

Hata hivyo hawajatoa ushahidi kwa madai yao, wala kueleza ni jinsi gani aliuawa.

Alionekana mara ya mwisho lini?

Jamal Khashoggi ni mkosoaji mkubwa wa mwanamfalme wa Saudi Arabia Mohammed bin Salman. Ana zaidi ya wafuasi milioni 1.6 katika mtandao wa Twiter na amelifanyia kazi gazeti la the Washington Post .

Siku ya Jumanne alikuwa kwenye ubalozi kupata stakabadhi za kumtaliki mke wake wa zamani ili apate kufunga ndoa na mchumba wake raia wa Uturuki Hatice Cengiz.

Ms Cengiz alisema alisubiri nje kwa saa 11 lakini hakutoka ndani ya ubalozi huo.

Alisema Bw Khashoggi alihitajika kusalimisha simu yake ambayo ni sheria kwenye balozi nyingi. Alimuambia ampigie simu mshauri wa Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan ikiwa hangerudi kutoka ubalozi huo.

Jamal Khashoggi's fiancée Hatice waits in front of the Saudi consulate in Istanbul on 3 October 2018

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha, Mchumba wa Jamal Khashoggi Hatice alisubiri nje ya ubalozi siku ya Jumatano