Okoth Obado akamatwa na maafisa wa kitengo cha upelelezi katika kesi ya mauaji ya Sharon Otieno Kenya

Sharon

Chanzo cha picha, SHARON OTIENO/FACEBOOK

Maelezo ya picha, Marehemu Sharon Otieno
Muda wa kusoma: Dakika 2

Polisi nchini Kenya imemkamata Gavana Okoth Obado wa jimbo la migori magharibi mwa nchi hiyo.

Obado ataaendelea kuzuiliwa huku uchunguzi kuhusiana na kifo cha mwanafunzi wa chuo kikuu, Sharon Otieno ukiendelea.

Maafisa kutoka kitengo cha upelelezi wa uhalifu wa jinai, DCI wamemhoji kwa saa kadhaa leo.

Obado amekanusha madai ya kuhusika na mauaji ya mwanafunzi huyo ambaye inasadikiwa alikuwa mpenzi wake.

Polisi inasema Gavana huyo wa jimbo la Migori magharibi mwa Kenya atafikishwa mahakamani mjini Nairobi siku ya Juma tatu.

Ruka X ujumbe
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe

Wiki iliyopita, Obado aliwaambia polisi mjini Kisumu kwamba yeye binafsi angelipenda kuwajua wauaji wa Sharon ni kina nani.

Wakili wake Obado, Cliff Ombeta anasema mteja wake hana hatia na kwamba amewaeleza polisi kila kitu alichofahamu kuhusiana na kesi hiyo.

Kupatikana kwa mwili wa Sharon

Mwili wa Sharon ulipatikana ukiwa umetupwa kichakani eneo la Oyugis, Homa Bay mnamo 5 Septemba.

Kuuawa kwa kudungwa visu

Mtaalamu mkuu wa upasuaji wa maiti Kenya Johansen Oduor, baada ya kuuchunguza mwili wa marehemu, alisema mwanamke huyo huenda alifariki kutokana na kuvuja damu sana.

Alikuwa amedungwa kisu mara nane.

Mwili huo pia ulikuwa na alama za kukabwa shingoni, na alama nyingine zinazoashiria kwamba alijaribu kujiokoa.

Dkt Oduor alisema kuna uwezekano kwamba Sharon alibakwa.

Sharon

Chanzo cha picha, SHARON OTIENO/FACEBOOK

Ilitokeaje hadi yeye na mwandishi wakatekwa?

Sharon anadaiwa kukutanishwa na mwandishi Barrack Oduor na diwani wa zamani wa eneo la Kanyidoto, Homa Bay Lawrence Mula ambaye alimfahamisha kwamba alikuwa na rafiki yake aliyetaka usaidizi wake kama mwanahabari.

Ni siku hiyo ambapo Sharon alikutana mara ya kwanza na Oduor ambapo alimwambia kwamba Gavana wa Migori Okoth Obado alikuwa amemtelekeza baada yake kubeba mimba yake.

Familia yake imesitisha kwa muda usiojulikana mipango ya mazishi ya marehemu na Jumatano waliwaambia wanahabari kwamba wanasubiri matokeo ya uchunguzi kuhusu kifo chake.