Ukungu watatiza safari za ndege kwa muda Kenya

Chanzo cha picha, PUBLIC DOMAIN VIA WIKIPEDIA COMMONS
Ndege kadhaa zilitatizika kutua katika uwanja mkuu wa ndege Nairobi hii leo kutokana na ukungu mkubwa uliotanda asubuhi.
Baadhi zililazimika kugeuza njia kuelekea katika viwanja vingine vya ndege kutokana na hali hiyo ya hewa iliofanya kuwa vigumu mtu kuona mbele kutokana na ukubgu huko.
Baadhi ya wasafiri walichelewa kufika na baadhi safari zao kutatizika kwa waliokuwa wakiunganisha safari au kubadili ndege kuingia nyingine kutoka uwanja huo wa JKIA.
Ndege kadhaa zilizotarajiwa kutua Nairobi zilibidi kuelekezwa kwingine ikiwemo Mombasa, Pwani ya Kenya.
Katika ujumbe kwenye mtandao wa Twitter shirika la ndege la Kenya Airways, limesema usafiri wa ndege umetatizika kutokana na hali bali ya hewa iliotatiza marubani kuona vizuri.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 1

Lakini sio tu kwa viwanja vya ndege baadhi ya watu walilamika katika mitandao ya kijamii namna hali hiyo ya hewa ilivyowaathiri usafiri wa barabarani:
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 2
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 3
Kenya Airways inamilikiwa kwa 48.9% naserikali na 7.8 % na kampuni ya ndege Air France-KLM.
Ndege 25 za nchi za nje huhudumu nje ya uwanja mkuu wa ndege Nairobi, ikiwemo Turkish Airlines, Emirates, South African Airways na Ethiopian.














