Sheria ya kikomo cha umri wa kugombea urais yaidhinishwa na mahakama Uganda

Museveni

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Uuamuzi huu una maana kuwa rais Yoweri Kaguta Museveni atakua huru kugombea katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2021
Muda wa kusoma: Dakika 3

Mahakama ya katiba nchini Uganda imeidhinisha mageuzi ya katiba yaliondoa kikomo kwa umri wa kugombea urais.

Majaji wanne kati ya watano wa jopo la majaji wamesema mageuzi hayo hayakiuki katiba, na pia hayendi kinyume na hsri aya muongozo wa bunge nchini.

Awali umri wa mwisho kwa kugombea ilikuwa miaka 75.

Hii ina maana Rais wa nchi hiyo Yoweri Kaguta Museveni atakua huru kugombea katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2021.

Kikao cha kutoa uamuzi huo uliowasilishwa katika mahakama kuu huko Mbale kilianza kwa naibu jaji mkuu, Alfonse Owiny-Dollo, kuanza kwa kuomba radhi kwa mahakama kuchelewa kuanza kwa muda uliopangwa awali.

Ruka X ujumbe, 1
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 1

Masuala matatu makuu ambayo mahakama ilitakiwa kuyatolewa maamuzi ni:

Hata hivyo mahakama imekataa kuongeza miaka ya wabunge waliotaka kusalia madarakani kwa miaka 7 badala ya mitano ya sasa.

Katika uamuzi wake Jaji Cheborion Barishaki ameeleza kwamba kuongezwa kwa muhula wa kuhudumu bunge kutoka miaka mitano hadi miaka saba itakuwani hatua ya kibinfasi na inakwenda kinyume na maadili ya uongozi bora:

Ruka X ujumbe, 2
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 2

Ameeleza kwamba kwa kutowashauri raia kuhusu kuongeza muhula wa kuhudumu, wabunge wamejilimbikizia uongozi ambao unatolewa kikatiba kwa watu kuamua ni nani wanaemtaka awaongoze.

Maelezo ya video, Wabunge wapigana makonde Uganda

Na kwa kuongeza muda wa wabunge kuhudumu kwa miaka miwili zaidi, viongozi hao wamewanyima raia nafasi za uchaguzi mwaka 2021, uliopangiwa uchaguzi mkuu nchini.

"Katiba ni ya kuwatumikia watu na sio kwa namna nyingine yoyote," alisema.

Kesi hii imewasilishwa baada ya watu kutoridhia hatua ya mageuzi hayo ya katiba yaliokumbwa na mzozo mwaka jana, yaliochangia kuondolewa kwa kikomo cha umri wa kugombea urais, na kuongezwa muda wa kuhudumu nyadhifa za kisiasa kutoka miaka mitano hadi misaba.

Je uamuzi huo umefuatiliwaje?

Kulishuhudiwa maandamano makubwa kupinga hatua hiyo katika sehemu tofauti nchini
Maelezo ya picha, Kulishuhudiwa maandamano makubwa kupinga hatua hiyo katika sehemu tofauti nchini

Raia nchini Uganda Alhamisi walifuatilia kwa makini uamuzi huo ukipitishwa kutoka mahakama ya katiba Mable kupitia vyombo vya habari na hata pia mitandao ya kijamii.

Na wakati uamuzi ukiendelea kusomwa kuhusu kuidhinishwa kwa kikomo cha umir wa kugombea urais - hatua inayoonekana ambayo huenda ikamruhusu Rais Yoweri Museveni kuendelea kuhudumu madarakani kwa zaidi ya utawla wake wa miongo mitatu, haya ndio baadhi ya yaliozungumzwa mitandaoni:

Ruka X ujumbe, 4
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 4

Ruka X ujumbe, 5
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 5

Kumekuwa na pingamizi kwa pendekezo la kuibadili katiba mwaka jana sio tu miongoni mwa raia nchini, lakini pia upinzani, viongozi wa kidini na hata baadhi ya wafuasi katika chama tawala Uganda.

Kulishuhudiwa maandamano makubwa kupinga hatua hiyo katika sehemu tofauti nchini na kusababisha Polisi kuingilia kati na kujaribu kuzima ghasia zilizozuka.