Afrika wiki hii kwa picha: 20-26 Oktoba 2017

Mkusanyiko wa picha bora kutoka Afrika na kuwahusu Waafrika maeneo mengine duniani wiki hii.

Members of the Legio Maria Church react while being affected by tear gas during clashes between the police and opposition supporters in Mathare, Nairobi, Kenya - Thursday 26 October 2017

Chanzo cha picha, AFP

Waumini hawa wa madhehebu ya Legio Maria wanaonekana wakiathiriwa na mabomu ya kutoa machozi wakitembea mtaani Mathare, Nairobi wakati wa makabiliano kati ya waandamanaji na polisi siku ya uchaguzi wa marudio Alhamisi.

Wydad Casablanca fans celebrate a goal against USM Alger during the CAF Champions league semi-final on 21/10/2017 at Casablanca's Mohamed VI stadium in Casablanca.

Chanzo cha picha, AFP

Uwanja wa Mohamed VI mjini Casablanca nchini Morocco hali ilikuwa hivi mashabiki wa Wydad Casablanca walipokuwa wanatazama timu hiyo yao ikilaza USM Alger ya Algeria na kufika fainali Ligi ya Klabu Bingwa Afrika.

Models display creations by Amede at the Lagos Fashion and Design Week in Lagos 25/10/2017

Chanzo cha picha, AFP

Wanamitindo hawa waliovalia mavazi ambayo ni ubunifu wa Amede kutoka Nairobi walishiriki katika maonesho ya Mitindo na Mavazi ya Lagos siku ya Jumatano. lengo la maonesho hayo ni kusaidia na kuvumisha tasnia ya mitindo ya mavazi Nigeria na Afrika kwa jumla.

Two men take a selfie during Kenya's Mashujaa Day (Heroes' Day) celebrations at Uhuru park in Nairobi 20/10/2017

Chanzo cha picha, Reuters

Na nchini Kenya, Wakenya hawa walikuwa na ujumbe wa amani taifa hilo lilipokuwa likijiandaa kwa uchaguzi wa marudio ambao ulisusiwa na upinzani. Walionekana wakijipiga selfie wakati wa maadhimisho ya Sikukuu ya Mashujaa ambayo huadhimishwa kila tarehe 20 Oktoba.

A man holds a burning stick as opposition supporters demonstrate at a burning barricade in Kibera, Nairobi, 25/10/2017

Chanzo cha picha, AFP

Lakini kulitokea makabiliano kati ya polisi na wafuasi wa upinzani kabla ya uchaguzi huo kufanyika - hapa mfuasi wa upinzani anaonekana akiandamana katika mtaa wa Kibera jijini Nairobi siku ya Jumatano kabla ya uchaguzi kufanyika Alhamisi...

A man watches as protesters clash with riot police attempting to disperse supporters of Kenyan opposition leader Raila Odinga in Kibera slums of Nairobi. 26/10/2017

Chanzo cha picha, Reuters

Kulitokea vurugu zaidi Alhamisi, siku ya uchaguzi yenyewe. Hapa, mwanamume anaonekana akitazama kwa mbali wafuasi wa upinzani wakikabiliana na polisi...

African migrants sit on the side of a road as they wait for work in Misrata, Libya 22/10/2017

Chanzo cha picha, Reuters

Na wahamiaji hawa kutoka nchi mbalimbali za Afrika wanaonekana kando ya barabara Jumamosi katika mji wa Misrata nchini Libya wakisubiri kazi.

A South Sudanese refugee girl is seen at the Nguenyyiel refugee camp during a visit by US Ambassador to the UN Nikki Haley (not pictured) to the Gambella Region, Ethiopia October 24, 2017.

Chanzo cha picha, Reuters

Msichana mkimbizi kutoka Sudan Kusini naye anaonekana hapa akiwa kambi ya wakimbizi ya Nguenyyiel siku ya Jumanne, wakati wa ziara ya balozi wa Umoja wa Mataifa katika eneo la Gambella, Ethiopia.

Graca Machel, ex UN Secretary-General Kofi Annan (R) and ex Chile President Ricardo Lagos (C) take part in a Mandela Walk Together event in Westminster, Central London, Britain, 23/10/2017.

Chanzo cha picha, EPA

Na Matembezi ya Pamoja ya Mandela yalifanyika Westminster, London, siku ya Jumatatu na kuhudhuriwa na mjane wake Graca Machel na katibu mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa Kofi Annan pamoja na watu wengine mashuhuri.

Tom Morgan, from Bristol-based company The Adventurists, flies in a chair with large party balloons tied to it near Johannesburg, South Africa 20/10/2017

Chanzo cha picha, Reuters

Na mtali huyu kutoka Uingereza Tom Morgan anaonekana akipaa juu ya Afrika Kusini siku ya Ijumaa. Alisafiri 25km (maili 15.5 ) akiwa amefungwa kwenye kiti cha watalii na kuinuliwa juu na puto 100 za gesi aina ya helium.

South African surfer Mike Schlebach surfing, Cape Town, South Africa - Monday 23 October 2017

Chanzo cha picha, EPA

Na mteleza kwenye mawimbi Mike Schlebach wa Afrika Kusini anaonekana akishiriki mashindano ya kuteleza kwenye mawimbi baharini pwani ya mji wa Cape Town siku ya Jumatatu. Baadhi ya mawimbi yalikuwa na urefu wa 5m (16ft).

Picha kwa hisani ya AFP, EPA, PA na Reuters