Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Zuio la kuvua dagaa Ziwa Victoria linavyowaathiri wafanyabiashara Tanzania
Zuio la kuvua dagaa Ziwa Victoria linavyowaathiri wafanyabiashara Tanzania
Zuio la kuvua dagaa kwa siku nane kila baada ya wiki tatu katika Ziwa Victoria Nchini Tanzania limesababisha uhaba mkubwa wa dagaa katika maeneo mbalimbali.
Zoezi hili hufanyika na mamlaka ya ziwa hilo, ili kuruhusu dagaa kuzaliana kutokana na athari za mabadiliko ya tabianchi na uvuvi haramu.
Lakini baadhi wanahoji kwanini zoezi hilo linahusisha dagaa peke yake na kuacha aina nyingine ya Samaki ziwani humo?
Mwandishi wa BBC David Nkya ametembelea Ziwa Victoria Mkoani Mwanza Kaskazini Magharibi mwa Tanzania na kuandaa taarifa ifuatayo.