Rais wa Rwanda Paul Kagame amefadhaishwa na kushindwa kwa Arsenal

Chanzo cha picha, Getty Images
Rais wa Rwanda na shabiiki wa Arsenal Paul Kagame ameelezea kughabishwa kwake na hatua ya Gunners kushindwa na klabu ya mpya iliyopandishwa daraja katika mechi ya ufunguzi ya Ligi kuu ya Uingereza.
Brentford, iliyorejea katika ligi hiyo baada ya miaka 74 iliishabanga Arsenal mabao 2-1.
Bw Kagame mara kwa mara huangazia Gunners - klabu ambayo serikali yake ilifadhili.
Baada ya mechi hiyo aliandika katika mtandao wake wa Twitter: "Hatupaswi tu kutoa udhuru au Kukubali upuzi. Timu lazima iiundwe kwa lengo la kushinda kushinda na kushinda."
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe
Katika ujumbe mwingine alitaka wawe na "mpango utakaozaa matunda" ma kulalamika kwamba "mashabiki hawahitaji kuzoea hali hii".
Tanngu mwaka 2018, serikali ya Rwanda imekuwa na makubaliano ya udhamini yenye utata ya thamani ya zaidi ya pauni milioni 30 ($ 42m), ambayo inajumuisha nembo ya "Tembelea Rwanda" inaoonyeshwa kwenye mikono ya fulana ya Arsenal.
Wakosoaji wamesema ni mfano wa kiongozi wa kimabavu wa nchi masikini, ya Kiafrika inayofadhili kilabu tajiri cha mpira. Lakini serikali ya Rwanda inasema udhamini huo zaidi ya unajilipa kupitia mapato ya utalii..

Chanzo cha picha, Reuters
Matokeo ya mechi Jumamosi
Katika mechi za EPL zilizochezwa leo Jumamosi;
Manchester United 5-1 Leeds United
Burnley 1- 2 Brighton
Chelsea3 - 0 Crystal Palace
Everton3- 1 Southampton
Leicester 1-0 Wolves
Watford 3-2 Aston Villa













