Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Putin: Nchi za Magharibi zinaharibu uchumi wa dunia, Urusi ndio italeta 'utulivu'

Vita vya Ukraine havina uhusiano wowote na kupanda kwa bei ya nishati, rais wa Urusi aliweka wazi kuwa Ulaya yenyewe imekataa kushirikiana na Urusi.

Moja kwa moja

  1. Mataifa ya NATO yazungumza juu ya kuimarisha ulinzi wa Ukraine

    Mashambulizi makali ya roketi dhidi ya Ukraine yaliyorushwa na Urusi siku ya Jumatatu yamezidi kuzitia nguvu nchi za Magharibi katika azma yake ya kuunga mkono Kyiv katika vita hivi, Waziri wa Ulinzi wa Marekani Lloyd Austin alisema Jumatano katika mkutano wa viongozi wa NATO kwenye makao makuu ya muungano huo mjini Brussels.

    Austin pia alielezea uvamizi wa UAF kama usio wa kawaida, ambao alisema ulibadilisha mienendo ya vita.

    "Huu ni ushindi wa askari jasiri wa Ukraine. Lakini usaidizi wa Kundi la Mawasiliano katika kutoa, mafunzo, na msaada wake ni muhimu sana," mkuu wa Pentagon alisema.

    Kama ifuatavyo kutoka kwa ujumbe wa Twitter wa Waziri wa Ulinzi wa Ukraine Oleksiy Reznikov, kuhusiana na mashambulizi makubwa ya roketi dhidi ya Ukraine mapema wiki hii, mada kuu ya mkutano huo mjini Brussels itakuwa ni kuimarisha ulinzi wa anga wa nchi hiyo.

    Huu ni mkutano wa sita wa Kundi la Mawasiliano la ulinzi wa Ukraine, na wa kwanza tangu Urusi kunyakua maeneo manne ya Ukraine, tangazo nchini Urusi la usajili wa wanajeshi wa ziada na matamshi ya matumizi ya silaha za kinyuklia yanayotolewa na Moscow

  2. Pande Zinazopigana Ethiopia Zahimizwa Kukomesha Vita

    Nchi sita za magharibi zikiwemo Marekani na Uingereza zimesema 'zina wasiwasi mkubwa' na kuongezeka kwa ghasia kaskazini mwa Ethiopia hali inayosababisha kuzorota kwa mgogoro mbaya wa kibinadamu.

    Katika taarifa ya pamoja iliyotolewa Jumatano Australia, Denmark, Ujerumani na Uholanzi zimeungana na Washington na London katika kuzitaka pande zinazopigana-serikali ya Ethiopia na vikosi vya Tigrayan- kusimamisha mara moja mapigano .

    Ghasia nchini humo zimesambaratisha mapatano ya miezi mitano mwezi Agosti na licha ya pande zote mbili kukubali mwaliko wa Umoja wa Afrika (AU) kwa mazungumzo ya amani, mapigano yameendelea kupamba moto huku nchi jirani ya Eritrea ikishiriki kuunga mkono jeshi la Ethiopia-jambo ambalo lililaaniwa na nchi hizo sita.

    "Wahusika wote wa kigeni lazima wakomeshe vitendo vinavyochochea mzozo huu," taarifa ya pamoja ilisema ambayo pia ilishutumu mashambulizi dhidi ya raia. Mapendekezo ya mazungumzo ya awali, yaliyopangwa kufanyika mwishoni mwa juma lililopita nchini Afrika Kusini, yalicheleweshwa kutokana na kile kilichoelezwa kuwa sababu za vifaa.

    Haijulikani ni lini yatafanyika.

    Nchi hizo sita zaidi zilihimiza vikosi vya Addis Ababa na Tigray "kufuata suluhu ya mazungumzo" chini ya mchakato unaoongozwa na AU na kuongeza kuwa vita lazima vitambue "Hakuna suluhu ya kijeshi kwa mzozo huo." Serikali na vikosi vya Tigray hawajajibu taarifa hiyo.

  3. Deontay Wilder anataka pambano na Anthony Joshua lifanyike barani Afrika

    Deontay Wilder anaamini kuwa pambano na Anthony Joshua bado ni "pambano namba moja duniani" huku akijiandaa kurejea uwanjani Jumamosi. Wilder, 36, alipigana mara ya mwisho mwaka mmoja uliopita na anapambana na Robert Helenius huko New York wakati wa kurudi kwake.

    Lengo la uzito wa juu ni kuwa bingwa wa dunia tena, lakini Wilder pia ana mipango mikubwa ya pambano dhidi ya Joshua Muingereza.

    "Ningependa kufanya pambano hilo barani Afrika," aliambia BBC Sport. "Bado ni pambano nambari moja duniani kwa kila mtu. Kila ninapoenda, watu huwa wananizungumzia dhidi ya Joshua."

    Kumekuwa na mapambano kadhaa ya uzani wa juu barani Afrika, pamoja na pambano la Muhammad Ali na George Foreman huko Kinshasa mnamo 1974.

    "Sote tuna mizizi kutoka huko," Wilder alielezea. "Nadhani itakuwa mahali pa kushangaza kuwa nayo, kurudi nyumbani. Kurudi kwa nchi ya mama. Bara lililojaa watu wetu. Ninaweza kuona kuwa pambano la kushangaza, kushinda, kushindwa au sare.

    "Nadhani tutapata heshima na upendo kutoka kwa watu wote huko."

    Wilder alifikiria sana kustaafu baada ya kushindwa mfululizo na Tyson Fury, lakini sasa anasema anapanga kupigana kwa miaka mingine mitatu.

    Joshua na Wilder hapo awali walikuwa kwenye mazungumzo kuhusu pambano lisilopingika mwaka wa 2019 na 2020 wakati wote wawili walikuwa mabingwa wa dunia.

    Wilder alishikilia ubingwa wa WBC huku Joshua akiwa bingwa wa WBA (Super), WBO na IBF. Joshua hivi majuzi alishindwa kuafikiana na bingwa wa WBC, Fury, lakini Wilder ana imani kwamba dili linaweza kutimizwa. Alisema: "Tuko makini na tunawahitaji wawe makini pia. Tulijaribu kupigana na haikufanyika.

    Ni siku na wakati mpya. Mambo yote yanawezekana." Joshua, bingwa wa dunia mara mbili, pia hivi karibuni atakuwa kwenye mchujo baada ya kushindwa mtawalia kwa bingwa Oleksandr Usyk.

  4. Putin: Magharibi inaharibu uchumi wa dunia, Urusi ndio italeta 'utulivu'

    "Magharibi, pamoja na maamuzi yake ya kijasiri, yanahujumu uchumi wa dunia, na kuhatarisha maisha ya mabilioni ya watu," - hivi ndivyo Rais wa Urusi Vladimir Putin alivyotuma ujumbe mkuu wa hotuba yake katika kongamano la kimataifa la "Wiki ya Nishati ya Urusi" huko St. . Petersburg.

    Kwa sababu ya kuyumba kwa bei na usawa wa soko, uchumi wa dunia, mafuta na nishati (FEC) inakabiliwa na mgogoro mkubwa, Putin analalamika, na hii inawezeshwa, kulingana na yeye, na vitendo vya kupindua vya washiriki wa soko binafsi, ambao wanaongozwa tu kwa matamanio yao ya kijiografia.

    Vita vya Ukraine havina uhusiano wowote na kupanda kwa bei ya nishati, rais wa Urusi aliweka wazi kuwa Ulaya yenyewe imekataa kushirikiana na Urusi.

    "Tuna kitu cha kufanya nayo, watatulaumu tena," Putin alisema, akilalamika kuwa ni Ulaya ambayo ilikuwa imeachana na biashara na Urusi na "kuweka vikwazo vya aina fulani." Putin pia anasisitizwa kuwa Russia inatofautiana na nchi za Magharibi kwa kuwa siku zote inatekeleza wajibu wake.

    Wakati huo huo, rais Putin alisema, Moscow haitasambaza mafuta kwa nchi ambazo zimeweka kikomo cha bei kwa malighafi ya Urusi. Putin alisema yuko tayari kuipatia Ulaya gesi zaidi katika msimu wa vuli na baridi, lakini alibainisha kuwa "mpira uko upande wa Umoja wa Ulaya." "Kama wanataka, wafungue bomba, na ndivyo hivyo," alisema.

    Kulingana na yeye, inawezekana kutengeneza mabomba ya gesi yaliyoharibiwa ya Nord Stream, lakini tu katika kesi ya uendeshaji zaidi wa haki ya kiuchumi na ikiwa njia ni salama.

    Kamba zote mbili za bomba kuu la gesi la Urusi kwenda Uropa, Nord Stream, zilianza kutiririka katika sehemu tatu mwishoni mwa Septemba. Huko Ulaya, wanashuku hujuma kwenye mabomba ya gesi ya chini ya maji yaliyojaa gesi, ambayo sasa hayafanyi kazi na yamekuwa silaha ya vita vya nishati vya Kremlin dhidi ya EU.

    Katika hotuba yake, rais wa Urusi kwa mara nyingine tena aliilaumu Marekani kwa hujuma hii, kwa sababu Wamarekani wanadaiwa kuwa na uwezo huo wa kiufundi, wanataka kudhoofisha uwezo wa kiuchumi wa Ulaya na kuteka soko la nishati la Ulaya.

    Kwa kiwango gani jukwaa huko St. Petersburg linaweza kuchukuliwa kuwa "kimataifa" ni vigumu kuhukumu. Kati ya wadau wakuu katika soko la nishati duniani mwaka huu, ni Rais wa UAE Mohammed bin Zayed Al Nahyan pekee aliyekuja St. Petersburg.

  5. India yasitisha uzalishaji wa dawa ya kifua inayohusishwa na vifo vya watoto

    Mamlaka nchini India imeamuru kampuni ya kutengeneza dawa kuacha kutengeneza dawa za kikohozi baada ya ripoti kuwa huenda zinahusishwa na vifo vya makumi ya watoto nchini Gambia.

    Waziri wa afya katika jimbo la Haryana, Anil Vij, alisema ukaguzi katika kiwanda cha Maiden Pharmaceuticals uligundua ukiukwaji kadhaa wa vigezo na masharti.

    Shirika la Afya Duniani wiki iliyopita lilisema dawa zinazozalishwa na kampuni hiyo zilikuwa na kiasi kisichokubalika cha dutu za kemikali ambazo zinaweza kusababisha uharibifu wa figo.

    Maafisa nchini Gambia wanasema wanachunguza vifo vya watoto 66 ambavyo vinahusishwa na chapa nne za dawa za kikohozi zilizoagizwa kutoka India.

    Maiden Pharmaceuticals wiki iliyopita walisema wameshtushwa na kusikitishwa na tukio hilo na wanashirikiana na uchunguzi.

  6. Elon Musk akanusha kuongea na Rais wa Urusi Vladimir Putin kuhusu vita ya Ukraine

    Elon Musk amekanusha ripoti kuwa alizungumza na Vladimir Putin kabla ya kuchapisha kura ya maoni kwenye ukurasa wake wa Twitter na mapendekezo yake ya kukomesha uvamizi wa Urusi nchini Ukraine.

    Ian Bremmer, mkuu wa kitengo cha ushauri wa masuala ya hatari ya kisiasa cha Eurasia Group, alidai kuwa Bw Musk alimweleza kibinafsi kuhusu mazungumzo na Bw Putin.

    Lakini Bw Musk sasa amekanusha hili.

    "Nimezungumza na Putin mara moja tu na hiyo ilikuwa takriban miezi 18 iliyopita. Mada ilikuwa ilikua vyombo vya anga," Bw Musk alituma katika Twitter.

    Wiki iliyopita, Mkurugenzi Mtendaji wa Tesla aliwaomba wafuasi wake milioni 107.7 kupiga kura juu ya njia za kutatua vita vya Ukraine.

    Mapendekezo hayo yalijumuisha pendekezo la kufanyika kwa kura katika sehemu za Ukraine zinazokaliwa na Urusi ambazo Kremlin inasema imeziambatanisha. Maoni yake yalikaribishwa na Moscow.

    Bilionea huyo alisema: "Urusi inaondoka ikiwa hayo ni mapenzi ya watu."

    Rais Putin tayari ametangaza mikoa minne ya Ukraine kuwa sehemu ya Urusi, kufuatia kile kinachoitwa kura ya maoni iliyolaaniwa kuwa ni ya udanganyifu na Kyiv na washirika wake wa Magharibi. Urusi haidhibiti kikamilifu eneo lolote kati ya hizo nne.

    Bw Musk pia alipendekeza ulimwengu unapaswa "rasmi" kutambua Crimea - iliyochukuliwa kinyume cha sheria na Moscow mwaka 2014 - kama sehemu ya Urusi.

    Katika chapisho, Bw Bremmer aliandika kwamba Bw Musk alimwambia rais wa Urusi "amejitayarisha kufanya mazungumzo", lakini tu ikiwa Crimea itaendelea kuwa chini ya udhibiti wa Urusi, ikiwa Ukraine itakubali aina ya kutoegemea upande wowote, na ikiwa Kyiv itatambua unyakuzi wa Urusi wa Luhansk, Donetsk. , Kherson na Zaporizhzhia.

    Bw Bremmer alisema bosi wa SpaceX alimwambia kuwa Bw Putin alisema malengo haya yatatimizwa "hata iweje" na kwamba kuna uwezekano wa shambulio la nyuklia ikiwa Ukraine itavamia Crimea.

    Lakini Bw Musk amekanusha ripoti hizo.

  7. TikTok yajinufaisha kupitia maudhui ya familia zinazoombaomba

    Familia zisizo na makazi katika kambi za Syria zimekuwa zikiomba kuchangiwa kupitia mtandao wa TikTok huku kampuni hiyo ikichukua hadi 70% ya mapato, uchunguzi wa BBC uligundua.

    Watoto wanachapisha maudhui ya moja kwa moja kwenye programu ya mtandao wa kijamii kwa saa nyingi, wakiomba zawadi za kidijitali zenye thamani ya pesa taslimu.

    BBC iliona machapisho hayo yakipata hadi $1,000 (£900) kwa saa, lakini iligundua kuwa watu waliokuwa kwenye kambi walipokea sehemu ndogo tu ya pesa hiyo.

    TikTok ilisema itachukua hatua za haraka dhidi ya aina hiyo ya kuomba omba Kampuni hiyo ilisema aina hii ya maudhui hayaruhusiwi kwenye jukwaa lake, na ilisema kamisheni yake kutokana na zawadi za kidijitali ilikuwa chini ya 70%.

    Lakini ilikataa kuthibitisha kiasi halisi. Mapema mwaka huu, watumiaji wa TikTok walishuhudia machapisho yakirushwa moja kwa moja ya familia katika kambi za Syria, wakiomba msaada kutoka kwa watazamaji wengine Katika kambi za kaskazini-magharibi mwa Syria, BBC iligundua kuwa mtindo huo ulikuwa ukiwezeshwa na wale wanaojiita "wafanyabiashara wa kati wa TikTok", ambao walizipatia familia simu na vifaa vya kurusha maudhui moja kwa moja.

  8. Urusi yaiweka Meta katika orodha ya mashirika ya kigaidi

    Mamlaka ya Urusi imeongeza Meta - inayomiliki Facebook na Instagram - kwenye orodha ya mashirika ya kigaidi na itikadi kali, shirika la Interfax la nchi hiyo linaripoti.

    Jukwaa hizo mbili zilipigwa marufuku nchini Urusi mnamo Machi kwa propaganda maarufu kama "Russophobia".

    Ilifuata tangazo la Meta kwamba ingeruhusu machapisho kama vile "kifo kwa wavamizi wa Urusi" lakini sio vitisho vya kuaminika dhidi ya raia.

    Meta ilikata rufaa dhidi ya marufuku hiyo lakini ikapitishwa na mahakama ya Moscow mwezi Juni. Marufuku hiyo haikuhusu WhatsApp, ambayo Meta pia inamiliki. Hisia za ukatili Kampuni kubwa ya kiteknolojia ya Marekani imekanusha madai kwamba inakuza hisia za chuki dhidi ya Urusi.

    Mnamo Machi, afisa wa Meta aliiambia BBC ilikuwa ikifanya ubaguzi wa muda kwa sera zake za kawaida, "kwa kuzingatia uvamizi unaoendelea wa Ukraine", kuruhusu wale walioathiriwa "kuelezea hisia za vurugu kwa majeshi yanayovamia".

    Kampuni imefikiwa kwa maoni kuhusu maendeleo ya hivi karibuni Kulingana na Interfax, kuwekwa kwenye orodha ya mashirika yenye msimamo mkali inamaanisha benki zinaweza kufungia fedha za Meta nchini Urusi.

    Makundi mengine kwenye orodha hiyo ni pamoja na Taliban na vyama vya upinzani vya Urusi.

    Twitter pia imewekewa vikwazo nchini Urusi.

    Urusi imekabiliwa na kutengwa kimataifa na vikwazo vikali vya kiuchumi tangu kuivamia Ukraine na imejibu kwa kubana njia za kueneza upinzani.

    Imepitisha sheria zinazozuia kile kinachoweza kuripotiwa nchini - kuadhibiwa kwa vifungo virefu gerezani. Moja ya mashirika machache huru ya habari yaliyosalia nchini humo, gazeti la Novaya Gazeta, lilisimamisha shughuli zake mwezi Machi, baada ya kupokea onyo kutoka kwa shirika la uangalizi wa vyombo vya habari nchini Urusi.

  9. Waliolipua daraja la Crimea wakamatwa huku milipuko mipya ikisikika

    Urusi inasema inawazuilia watu wanane kuhusiana na mlipuko wa Jumamosi kwenye daraja muhimu linalounganisha Urusi na Crimea.

    Idara yake ya usalama ya FSB imesema watano kati ya waliokamatwa ni Warusi, huku wengine wakiwa ni raia wa Ukraine na Armenia.

    FSB imeshutumu idara za usalama za Ukraine kwa kuhusika na shambulio hilo.

    Hayp yanajiri huku milipuko ikiripotiwa katika miji ya Kherson, Zaporizhzhia na Nikopol Ukraine.

    Mwandishi wa BBC aliyeko Kyiv Hugo Bachega anasema milipuko mitano imesikika huko Kherson, mojawapo ya miji mikubwa inayokabiliwa na uvamizi wa Urusi, huku kukiwa na ripoti ambazo hazijathibitishwa kuwa mfumo wa ulinzi wa anga katika mji huo umeanzishwa

    Alisema haijabainika ni nini kilisababisha milipuko hiyo.

    Mlipuko huo kwenye Daraja la Crimea ulikuwa pigo kubwa Rais wa Urusi Vladimir Putin, ambaye alifungua daraja hilo mnamo 2018, miaka minne baada ya Urusi kunyakua Crimea.

    Rais Putin alikiita "kitendo cha kigaidi", akisema vikosi vya kijasusi vya Ukraine vilikuwa na lengo la kuharibu kipande muhimu cha miundombinu ya kiraia ya Urusi.

    Soma:

  10. Mzozo wa Tigray: Vikosi vya Tigray vyashutumiwa kwa mauaji ya kiholela Amhara

    Wakaazi wa eneo la eneo la Amhara nchini Ethiopia ambalo lilichukuliwa tena na wanajeshi wa serikali hivi karibuni wamewashutumu wapiganaji kutoka eneo la Tigray kwa unyanyasaji ikiwa ni pamoja na mauaji ya kiholela.

    Wilaya ya Raya Kobo ilishikiliwa kwa wiki tano na vikosi vya Tigray. Wakazi hao waliambia BBC kwamba watu wanaoshukiwa kuwa wanaviunga mkono vikosi vya serikali walilengwa.

    Pande zote za mzozo kaskazini mwa Ethiopia hapo awali zimeshutumiwa kwa kukiuka haki za kimataifa za binadamu.

    Uchunguzi wa pamoja uliofanywa mwaka jana na Tume ya Haki za Kibinadamu ya Ethiopia (EHRC) na Ofisi ya Haki za Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa ulisema kunaweza pia kuwa na ushahidi wa uhalifu wa kivita.

    Unyongaji usio wa kimahakama, utesaji, ubakaji, na mashambulizi dhidi ya wakimbizi na watu waliokimbia makazi yao ulirekodiwa. Hata hivyo, mara kadhaa wamekanusha.

  11. Marekani yarejesha Nigeria kazi 23 za sana zilizoporwa

    Marekani imerudisha vipande 23 vya vitu vilivyoporwa nchini Nigeria. Shaba za Benin zilikabidhiwa kwa ujumbe wa Nigeria katika hafla iliyofanyika Jumanne huko Washington.

    Waziri wa Habari na Utamaduni wa Nigeria Lai Mohammed, ambaye alipokea kazi za sanaa, aliipongeza Marekani na taasisi zake kwa kurudisha nyumbani kazi za sanaa "zinazothaminiwa sana".

    "Vitu hivi vya sanaa ni asili ya utamaduni uliozizalisha. Watu hawapaswi kukataliwa kazi za mababu zao. Ni kutokana na hili kwamba tunafurahishwa na urejeshwaji wa leo," alisema.

    Wizara ya habari ilisema kwamba kazi za sanaa zilizorejeshwa "zinajumuisha 21 kutoka kwa Smithsonian na moja kutoka kwa Jumba la Sanaa la Kitaifa na Shule ya Ubunifu ya Rhode Island".

    Kurejesha nyumbani ni sehemu ya makubaliano ya nchi mbili ya mali ya kitamaduni ili kuzuia uagizaji haramu wa baadhi za sanaa za Nigeria nchini Marekani. Lonnie G.

    Bunch III, katibu wa Smithsonian, alisema taasisi hiyo "imenyenyekezwa na kuheshimiwa kwa kuchukua nafasi ndogo katika kuhamisha umiliki wa kazi za sanaa hadi Nigeria", kwa kuzingatia kuzingatia maadili.

    Bidhaa hizo zilikuwa sehemu ya maelfu ya kazi za sanaa zinazojulikana kama Bronze za Benin zilizoibwa kutoka kwa Ufalme wa Benin katika Nigeria ya sasa na wakoloni wa Uingereza mnamo 1897.

    Vitu hivyo vilisambazwa kwa makumbusho na taasisi mbalimbali kote Ulaya na Marekani. Nigeria inatazamiwa kupokea zaidi ya vitu hivyo vya sanaa kutoka Uholanzi, Chuo Kikuu cha Aberdeen huko Scotland, Mexico, Chuo Kikuu cha Cambridge nchini Uingereza na Ujerumani.

    Nchi hiyo ya Afrika Magharibi inasema hivi karibuni itazindua maonyesho ya kimataifa ya kusafiri na vitu vya kale ''katika namna ambayo itajishindia marafiki zaidi na kukuza nia njema kwa Nigeria na makabila ambayo yamezizalisha".

  12. Mtoto wa Kenya aliyefanyiwa upasuaji kutoa jembe lililosakama kichwani amefariki

    Mama ya mtoto wa miaka miwili aliyelazwa hospitali kubwa ya rufaa ya Kenyatta jijini Nairobi ili kufanyiwa pasuaji wa kutoa jembe lililokuwa limesakama kwenye fuvu la kichwa chake amethibitisha kuwa amefariki.

    Juhudi za madaktari wa Kenyatta jijini Nairobi kuokoa maisha ya mtoto huyo hazikufaulu.

    Haya yanajiri kufuatia malalamiko ya umma yaliotolewa mitandaoni kwamba mtoto huyo alikosa kupokea matibabu katika Hospitali hiyo ya Kitaifa ya Kenyatta, zaidi ya saa 24 baada ya kuhamishwa kutoka hopitali nyengine ya serikali.

    Katika taarifa yake hospitali hiyo ya Kenyatta imefafanua kwamba mtoto huyo alikuwa amepoteza damu nyingi na hali yake ilihitajika kuimarika kabla ya kufanyiwa upasuaji.

    Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta ndiyo hospitali kuu ya umma nchini kenya, lakini mara nyingi imeshutumiwa kwa uhaba wa vifaa muhimu vya madaktari kutumia kuwahudumia wagonjwa Pamoja na kuchelewa kutoa huduma.

    Bado haijabainika jinsi mtoto huyo mdogo alivyopata jeraha hilo la jembe kwenye fuvu la kichwa chake.

  13. Vita vya Ukraine: 'Wimbi jipya la ugaidi' linataka vikwazo zaidi asema Zelensky

    Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amezitaka nchi kuiwekea Urusi vikwazo zaidi ili kukabiliana na "wimbi jipya la ugaidi" baada ya mashambulizi ya Jumatatu dhidi ya nchi yake.

    Watu 19 waliuawa na wengine wengi kujeruhiwa huku makombora ya Urusi yakipiga maeneo tofauti nchini.

    Kufuatia mashambulizi zaidi siku ya Jumanne, Bw Zelensky alitoa wito kwa nchi za Magharibi kutafuta njia mpya za kutumia shinikizo la kisiasa kwa Urusi na kuunga mkono Ukraine.

    Wito huo ubakuja baada ya mkutano wake na viongozi wa mataifa saba tajiri zaidi duniani G7 kwa mazungumzo ya dharura.

    G7- ambayo inajumuisha Canada, Ufaransa, Ujerumani, Italia, Japan, Uingereza na Marekani - iliahidi kuendelea kutoa msaada wa "kifedha, kibinadamu, kijeshi, kidiplomasia na kisheria" kwa nchi yake "kwa muda mrefu iwezekanavyo".

    Bw Zelensky alisema: "Kwa wimbi jipya la ugaidi lazima kuwe na wimbi jipya la uwajibikaji kwa Urusi - vikwazo vipya, aina mpya za shinikizo la kisiasa na aina mpya za msaada kwa Ukraine."

    "Serikali ya kigaidi lazima inyimwe hata mawazo kwamba wimbi lolote la ugaidi linaweza kuleta chochote.

    "Rais wa Urusi Vladimir Putin alisema mashambulizi hayo yalikuwa ya kulipiza kisasi mlipuko wa Jumamosi kwenye daraja muhimu linalounganisha Urusi na Crimea.

    Nchi za Magharibi tayari zimeweka vikwazo dhidi ya biashara za Urusi pamoja na washirika wa Rais Putin tangu uvamizi wa Ukraine mwezi Februari.

    Maelezo zaidi:

  14. Hujambo na karibu kwa matangazo ya moja kwa moja leo Jumatano 12.10.2022.