Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Daktari Mtanzania afariki kutokana na maambukizi ya Ebola Uganda

Daktari raia wa Tanzania mwenye umri wa miaka 37 ambaye amekuwa akisomea Shahada ya Uzamili ya Udaktari katika Upasuaji katika Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala amefariki dunia kutokana na ugonjwa wa Ebola, Chama cha Madaktari wa Upasuaji Uganda kimetangaza.

Moja kwa moja

  1. Habari za hivi punde, Urusi yasema wanajeshi wake wametoroka katika mji muhimu wa mashariki wa Lyman

    Wizara ya ulinzi ya Urusi imesema imewaondoa wanajeshi wake katika mji wa kimkakati wa Lyman mashariki mwa Ukraine.

    "Kwa sababu ya tishio la kuzingirwa askari washirika wameondolewa kutoka Krasnyi Lyman hadi kwenye sehemu nzuri," inasema, ikinukuliwa na mashirika ya habari ya serikali ya Urusi.

    Krasnyi (Nyekundu) Lyman lilikuwa jina la zamani la Soviet la Lyman, ambalo vikosi vya Ukrain vinasema waameingia.

    Urusi inawaita wanajeshi wake "walioshirikiana" na wapiganaji wa ndani wanaoungwa mkono na Moscow.

  2. Mwanamuzi Chike: ‘Mimi sio zilionea au bilionea’

    Mwimbaji wa Nigeria Chike amezungumza na kipindi cha BBC cha This is Africa radio kuhusu shinikizo la kifedha analokumbana nalo baada ya mafanikio yake kimuziki na kutoa albamu yake, The Brother's Keeper.

    Familia yake inamgeukia wakati maamuzi makubwa yanahitajika kufanywa kwa sababu "yeye atalipa", alisema.

    "Mimi sio bilionea au bilionea, mbali na hilo," aliongeza, akisema ana furaha.

    Kwa hakika, jina la albamu yake mpya ni rejeleo la moja kwa moja la jinsi uhusiano wake na marafiki na familia umebadilika kufuatia mafanikio yake kama msanii wa muziki.

    Chike alikuja kujulikana kupitia maonyesho ya talanta ikiwa ni pamoja na The Voice Nigeria, na katika hali isiyo ya kawaida, ameweza kujitengenezea taaluma yake mwenyewe baadae, na nyimbo kadhaa zilizovuma kwa jina lake zimeshinda tuzo ya albamu ya kwanza, Boo of the Booless.

    Lakini pamoja na mafanikio makubwa huja wajibu mkubwa anasema: "Kwa maisha haya mapya sina budi kumtazama kila mtu aliye karibu nami. Huo ndio ukweli sasa hivi."

  3. Idadi ya walioambukizwa Ebola Uganda yafikia 38 - Wizara ya afya

    Idadi ya watu walioambukizwa virusi vya ebola kufikia sasa imefikia watu 38

    Kulingana na ripoti mpya ya wizara ya afya nchini Uganda, aidha idadi ya watu waliofariki kutokana na ugonjwa huo imefikia 8 baada ya watu wengine watatu kufariki.

    Watu hao waliofariki wameripotiwa kutoka eneo la Mubende.

    Daktari Mtanzania aliyekuwa akisoma nchini Uganda ni miongoni mwa waliofariki kutokana na virusi vya Ebola.

    Raia huyo huyo mwenye umri wa miaka 37 alikuwa akisomea Shahada ya Uzamili ya Udaktari katika Upasuaji, akiwa mwanafunzi wa kimataifa.

    Chama cha madaktari wa upasuaji nchini Uganda kimetoa risala za rambirambi kwenye akaunti zao za Twitter.

    Mapema wiki hii, wizara ya afya ilisema kuwa wahudumu sita wa afya walipimwa na kukutwa na virusi vya Ebola. Inasemekana wengine waligusana na muathiriwa wa kwanza wa ebola

    Wahudumu wengi wa afya walioshughulikia kesi ya kwanza walikuwa wanafunzi. Baadaye walitangaza kuwa walikuwa kwenye mgomo, wakitaja ukosefu wa vifaa vya kujikinga na marupurupu yakujiweka hatarini..

    Siku ya Ijumaa, wizara ilitangaza kuwa mlipuko wa Ebola ulikuwa umeenea hadi wilaya ya nne.

    Takwimu rasmi zinaonyesha kuwa jumla ya kesi zilizothibitishwa zimefikia thelathini na tano, na vifo vinane.

    Watu wawili hadi sasa wamepona ugonjwa huo wa virusi, kulingana na mamlaka ya afya.

    Rais Yoweri Museveni amefutilia mbali kufungiwa kwa maeneo yaliyoathiriwa.

    Mlipuko wa Ebola nchini Uganda unahusisha aina adimu ya virusi vya Sudan ambayo hakuna chanjo yake.

  4. Bilionea wa teknolojia Elon Musk azindua aina mpya ya roboti yenye umbo la binaadamu

    Roboti ya Optimus iliokuwa jukwaani katika hafla hiyo ilionekana ikipungia watu mkono na kunyanyua magoti yake.

    Afisa mkuu mtendaji amesema roboti hiyo inaendelea kufanyiwa kazi lakini huenda ikauzwa kwa umma katika miaka michache ijayo.

    Roboti za Tesla zitafanyiwa majaribio katika kazi za mkono kwenye viwanda vya kutengeneza magari, wahandisi wa kampuni hiyo wanasema.

    Roboti hiyo ilisukumwa kwenye jukwaa katika hafla ya kila mwaka ya kampuni ya Tesla kwenye maonyesho ya intelijensia bandia.

    Watu walionyeshwa video ya Optimu akifanya kazi nyepesi kama vile kumwagilia mimea maji, akibeba maboxsi na kunyanyua vyuma.

    Musk amesema roboti hizo zitaundwa kwa wingi kwa bei ya chini ya $20,000 (£17,900), na zitapatikana sokoni katika muda wa miaka mitatu hadi mitano ijayo.

    Mmiliki huyo wa kampuni ya Tesla amezungumzia "mustakabli wenye neema". "Ni mageuzi muhimu ya ustaarabu kama tunavyooufahamu," aliongeza kusema.

  5. Erik ten Hag: 'Ninamuamini Maguire'

    Meneja wa Manchester United Erik ten Hag anasema bado anamuamini Harry Maguire licha ya beki huyo kukosolewa

    Maguire amekuwa akidhihakiwa na baadhi ya mashabiki wake kwenye majukumu ya klabu na nchi msimu huu na alifanya makosa katika ufungaji wa mabao mawili ya Ujerumani katika sare ya 3-3 ya England siku ya Jumatatu.

    "Ninamuunga mkono kwa sababu ninamwamini," alisema Ten Hag.

    "Inamhusu. Nina hakika anaweza kufanya hivyo. Ataligeuza hili. Nina hakika sana kuhusu hilo."

    Ten Hag amewapendelea Lisandro Martinez na Raphael Varane kama safu yake ya ulinzi ya kati, huku mchezaji Bruno Fernandes akivalia kitambaa cha unahodha mbele ya Maguire katika wiki za hivi karibuni.

    Maguire amecheza mechi tatu pekee za Premier League msimu huu.

    "Hata baada ya kutokuwa kwenye timu, alifanya mazoezi vizuri," alisema mkufunzi Ten Hag kuhusu mchezaji huyo mwenye wa umri wa miaka 29 .

    "Lakini muhimu zaidi, ubora ulikuwepo. Unaona kazi yake, takribani mechi 50 akiwa na England. Amefanya vizuri sana kwa Leicester na Manchester United. Unachokiona ni kwamba ana uwezo wa juu."

    Luke Shaw, mchezaji mwenza wa Manchester United na Uingereza, alisema mapema wiki hii kwamba Maguire amekosolewa "zaidi ya nilivyowahi kuona hapo awali kwenye soka".

  6. Wanajeshi wa UKraine wauzingira mji uliotekwa na Urusi

    Kundi kubwa la Wanajeshi wa Urusi huko Lyman "limezingirwa" na makazi karibu na mji huo yamekombolewa tena, anasema Serhiy Cherevatyi, msemaji wa vikosi vya Ukraine mashariki.

    Aliiambia TV ya Ukraine "data zetu zinaonyesha kwamba karibu wanajeshi 5,000 hadi 5,500 wa Urusi waliokuwa Lyman wamezingirwa na vikosi vya Ukraine", lakini alisema idadi hiyo ilikuwa chini kwa kwa sababu ya mashambulizi ya hivi karibuni ambapo wanajeshi "wengi" wa Urusi waliuawa au kujeruhiwa.

    Cherevatyi alisema majaribio yote yanayoendelea ya wanajeshi wa Urusi "yameshindwa". Pia alizungumza juu ya umuhimu wa Lyman, ambao, iwapo utachukuliwa na wanajeshi wa Ukraine, ingewaruhusu kusonga mbele kwenye Kreminna na Severodonetsk, ambazo zote ni ngome kuu zinazoshikiliwa na Urusi.

    "Pia ni muhimu sana kisaikolojia, kwa sababu - kama Rais Zelensky alivyosema jana - vikosi vya Ukraine vinaanza kuingia kwa nguvu katika maeneo yaliotekwa - na sio kutetea tu."

    Hata hivyo operesheni ya kijeshi "bado haijaisha," alihitimisha.

    Video sasa imeibuka inayodaiwa kuwaonyesha wanajeshi wa Ukraine wakiinua bendera ya taifa ya nchi hiyo yenye rangi ya buluu na njano kwenye lango la mji huo, ambapo maelfu ya wanajeshi wa Urusi wanaripotiwa kuzingirwa.

  7. Habari za hivi punde, Ecowas yalaani mapinduzi ya kijeshi Burkina Faso

    Majirani wa Burkina Faso wamelaani mapinduzi ya wazi ya Ijumaa, wakisema "haikuwa sawa" kwa waasi wa jeshi kunyakua mamlaka wakati nchi hiyo ilipokuwa ikitafuta utawala wa kiraia.

    Kundi la eneo la Ecowas lilielezea kuondolewa kwa kiongozi Luteni Kanali Paul-Henri Damiba kama "kinyume cha katiba".

    Hii ni mara ya pili mwaka huu jeshi la nchi hiyo kunyakua madaraka.

    Mara zote mbili, viongozi wa mapinduzi walisema walilazimika kuingilia kati kwa sababu usalama wa taifa ulikuwa mbaya sana.

    Burkina Faso inadhibiti 60% pekee ya eneo lake, wataalam wanasema, na ghasia za Kiislamu zinazidi kuwa mbaya.

    Akiwa amezungukwa na wanajeshi waasi, kiongozi huyo wa jeshi alitangaza kwenye TV ya taifa Ijumaa jioni kwamba wamemfukuza kiongozi wa kijeshi Lt Kanali Paul-Henri Damiba, kuivunja serikali na kusimamisha katiba.

    Ibrahim Traoré alisema kushindwa kwa Luteni Kanali Damiba kukabiliana na waasi wa Kiislamu ndio sababu ya mapinduzi hayo .

  8. Biden: "Marekani imejiandaa kikamilifu kutetea kila inchi moja ya eneo la Nato".

    Rais Joe Biden ameionya Urusi kwamba Marekani haitatishwa na vitisho vya kizembe baada ya Vladmir Putin kutangaza kunyakua maeneo manne ya Ukraine inayokaliwa kwa mabavu.

    Rais Biden alilaani "maneno ya kizembe na vitisho" vya mwenzake wa Urusi, lakini akaongeza kuwa Putin "hatatutisha".

    "Marekani na washirika wake hawatatishika," Biden alisema katika Ikulu ya White House.

    Kisha alizungumza na kiongozi wa Urusi moja kwa moja, akinyoosha kidole chake kwenye kamera, na kusema kwamba "Marekani imejiandaa kikamilifu, pamoja na washirika wetu wa Nato, kutetea kila inchi moja ya eneo la Nato".

    "Bwana Putin, usielewe vibaya ninachosema: kila inchi."

    Muda mfupi baadaye, afisa mkuu wa usalama wa taifa wa Biden alisema kulikuwa na nafasi ya Moscow kutumia silaha za nyuklia, lakini hakuonekana kuwa na tishio la karibu.

  9. Daktari Mtanzania afariki kutokana na maambukizi ya Ebola Uganda

    Daktari Mtanzania aliyekuwa akisoma nchini Uganda amefariki kutokana na virusi vya Ebola, waziri wa afya wa Uganda Dkt Jane Ruth Aceng amethibitisha.

    Raia huyo huyo mwenye umri wa miaka 37 alikuwa akisomea Shahada ya Uzamili ya Udaktari katika Upasuaji, akiwa mwanafunzi wa kimataifa.

    Chama cha madaktari wa upasuaji nchini Uganda kimetoa risala za rambirambi kwenye akaunti zao za Twitter.

    Haijabainika jinsi Dkt Mohammed Ali aliambukizwa lakini kifo chake kinajiri saa chache baada ya Wizara ya Afya siku ya Ijumaa kutangaza kwamba idadi ya waliofariki kutokana na mlipuko wa Ebola nchini imeongezeka hadi saba.

    “Ni kwa masikitiko makubwa tumepokea taarifa za kufariki kwa Dk Mohammed Ali, raia wa Tanzania mwenye umri wa miaka 37 ambaye alikuwa akisomea Shahada ya Uzamili ya Upasuaji katika Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala. Dk. Ali alishindwa katika vita dhidi ya Ugonjwa wa Virusi vya Ebola,” Chama cha Madaktari wa Upasuaji Uganda kiliandika kwenye Twitter Jumamosi.

    Waziri wa Afya, Dk Jane Ruth Aceng alisema Dk Ali alipimwa na kuwa na Ebola Septemba 26, 2022 na alifariki dunia alipokuwa akipatiwa matibabu katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Fort Portal. Alikufa saa 3 asubuhi siku ya Jumamosi.

    “Dk Ali ndiye Daktari wa kwanza, na mhudumu wa afya wa pili kuugua Ebola. Wa kwanza alikuwa mkunga kutoka Kliniki ya St Florence, kisa kinachowezekana, kwa sababu alifariki kabla ya kupimwa,” Dkt Aceng alituma ujumbe wa Twitter Jumamosi.

    Lakini mapema wiki hii, wizara ya afya ilisema kuwa wahudumu sita wa afya walipimwa na kukutwa na virusi vya Ebola. Inasemekana wengine waligusana na muathiriwa wa kwanza wa ebola

    Wahudumu wengi wa afya walioshughulikia kesi ya kwanza walikuwa wanafunzi. Baadaye walitangaza kuwa walikuwa kwenye mgomo, wakitaja ukosefu wa vifaa vya kujikinga na marupurupu yakujiweka hatarini..

    Siku ya Ijumaa, wizara ilitangaza kuwa mlipuko wa Ebola ulikuwa umeenea hadi wilaya ya nne.

    Takwimu rasmi zinaonyesha kuwa jumla ya kesi zilizothibitishwa zimefikia thelathini na tano, na vifo vinane.

    Watu wawili hadi sasa wamepona ugonjwa huo wa virusi, kulingana na mamlaka ya afya.