Urusi yaanza kushambulia miji ya magharibi mwa Ukraine katika mashambulizi mapya

Mapema siku ya Alhamisi, afisa mkuu wa ulinzi wa Marekani alisema kuwa vikosi vya Urusi vimesogea maili tatu (5km) karibu na Kyiv katika muda wa saa 24 zilizopita.

Moja kwa moja

  1. Mzozo wa Ngorongoro: Kaya 86 kutoka jamii za wafugaji kuhamishiwa katika mkoa jirani wa Tanga.

    Wanyama wa porini
    Maelezo ya picha, Wanyama wa porini

    Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa amefichua Alhamisi kuwa amepokea orodha ya wakazi 453 walio tayari kuhamishwa kutoka Hifadhi ya Ngorongoro baada ya serikali kuanza zoezi la hiari la kusajili wanaotaka kuhama.

    Serikali inawaruhusu Wamasai kuishi katika eneo la hifadhi pamoja na wanyamapori, lakini hivi karibuni ilizua wasiwasi juu ya ongezeko la watu, idadi ya makazi, mifugo na shughuli za kibinadamu zinazotishia uendelevu wa eneo lililoorodheshwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi, na Utamaduni (UNESCO) kuwa moja ya Urithi wa Dunia.

    Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu, ilisema kuwa kaya 86 kutoka katika jamii za wafugaji ambazo zimeeleza nia ya kuhama zitahamishiwa Kaskazini Mashariki mwa Tanzania, katika mkoa jirani wa Tanga.

    Akihutubia wazee wa Kimasai zaidi ya 350 wanaofahamika kwa jina la Laigwanan, Waziri Mkuu alisema Mkuu wa Nchi, Samia Suluhu ameeleza masikitiko yake juu ya hatma ya eneo hilo kutokana na kuongezeka kwa mifugo na binadamu wanaoishi kwa Pamoja na wanyamapori.

    Waziri Mkuu Majaliwa alieleza kuwa miaka ya 1960 na 1970 hakukuwa na wasiwasi wowote katika makazi ya Ngorongoro kwa sababu mwaka 1959 kulikuwa na wakazi 8,000 tu katika eneo hilo huku wengi wao wakimiliki mifugo kati ya 20 na 30.

    Alisema hivi sasa idadi ya watu wanaoishi katika makazi hayo inafikia zaidi ya 110,000 huku idadi ya mifugo ikiwa zaidi ya 813,000.

    Soma zaidi:

  2. Kifo cha Jenerali wa Urusi chathibitishwa na maafisa wa nchi za Magharibi

    Ukraine

    Chanzo cha picha, Russia Eastern Military District

    Maafisa wa nchi za Magharibi wamethibitisha kuwa jenerali mwingine mwandamizi wa tatu wa Urusi ameuawa nchini Ukraine.

    Taarifa zinasema Jenerali hiyo anatoka katika wilaya ya kijeshi ya mashariki mwa Urusi.

    Maafisa hao wa Maghaeribi hawakumtaja jenerali huyo, lakini awali jeshi la Ukraine lilisema Meja Jenerali Andrei Kolesnikov, kamanda wa jeshi la 29 la wilaya ya mashariki mwa Urusi, aliuawa.

    Wachambuzi hapo awali walisema kuwa uwepo wa viongozi wa ngazi ya juu wa kijeshi ndani au karibu na uwanja wa vita inaweza kuwa ishara kwamba operesheni za Urusi haziendi kama zilivyopangwa.

  3. Yapi yatakuwa majibu ya Nato iwapo Urusi itaidhibiti Ukraine nzima

    Ukraine

    Jeff Moonowa Lusaka Zambia anauliza: "Ikiwa Urusi itachukua udhibiti wa Ukraine yote, Nato na Marekani watasema nini ama watajibu kitu gani?" Hiyo ni ndoto kwa Nato, ambayo imeimarisha idadi ya wanajeshi katika nchi jirani lakini ambayo, kwa sababu zilizotajwa, haitaki kuingizwa katika vita na Urusi.

    Kuna uvumi kwamba, kabla ya tukio hilo kutokea, Kyiv inaweza kushawishiwa kufanya mpango na Moscow - kwa maneno mengine, kukabidhi baadhi ya wilaya zake kwa ajili ya kukomesha uhasama.

    Hata hivyo, tatizo na hali hiyo ni, kwanza, kwamba Kyiv haitaki kutoa ardhi, na pili, pia kuna hofu kwamba matokeo kama hayo yanaweza kumtia moyo Putin.

    Hata hivyo, hivi sasa wachambuzi wengi wanadhani kwamba Urusi itapambana kuishikilia Ukraine kwa muda mrefu.

  4. Mazishi ya kijeshi ya Lviv yajaza huzuni kila kote ya Ukraine

    Ukraine

    Mazishi yanafanyika nchini Ukraine kila siku. Familia tofauti zimekuwa kwenye simanzi, lakini uchungu wa maziko ni wa ulimwengu wote.

    Treni za Lviv zilizobeba majeneza ya wafu zinakutana na walinzi wa heshima wa askari wenzake. Sherehe za maombolezo zinafanyika kwa siku kadhaa. Mazishi huanza na usomaji wa misa kwa wafu katika kanisa la garrison la Watakatifu Petro na Paulo katikati ya jiji. Ni kanisa ambalo lina uhusiano wa muda mrefu na jeshi.

    Wanajeshi watatu waliozikwa leo wameuawa katika mapigano katika mji wa Kherson, kusini mwa Ukraine, ambako vikosi vya Urusi vimekuwa vikijaribu kusonga mbele.

    Waliofariki ni pamoja na Sajenti Dmytro Kabakov, mwenye umri wa miaka 59, Mwanajeshi Mwandamizi Andriy Stefanyshyn, mwenye umri wa miaka 40 na Luteni Taras Didukh, mwenye umri wa miaka 25.

    Pamoja na maziko mengine umakini na hisia zote zililenga kwenye majeneza matatu, yaliyofunikwa kwa bendera ya Ukrane, ambayo yalilala mbele ya madhabahu.

  5. Kwanini Nato haitaki kuweka masharti ya kutoruka kwa ndege

    Kwa nini NATO bado haijachukua hatua

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Kwa nini NATO bado haijachukua hatua

    Kuweka masharti ya kutoruka kwa ndege kunasikika kuwa jambo zuri la kujihami lakini kwa hakika linahusisha hatua ya kijeshi ya kukera.

    Ili kutekeleza sharti hilo, lazima utoe mifumo ya ulinzi wa anga ya adui, lazima urushe makombora kwenye vituo vya rada vya ardhini vinavyoendeshwa na Warusi, na kuwaua, na kisha itabidi uwarushe marubani wao kutoka angani.

    Huo ndio mwanzo wa Vita vya Tatu vya Dunia.

    Najua Rais Zelensky ameiomba tena na tena, na watu wengi hawaelewi kwa nini hilo halifanywi, lakini ingehusisha vikosi vyaanga vya Nato kwenda angani na kupambana na marubani wa Urusi, na hiyo ni hatari.

    Soma zaidi:

  6. Putin asema waliojitolea Mashariki ya Kati wanaweza kupigania Urusi nchini Ukraine

    Wanaume wakipata mafunzo katika Chuo cha Kibinafsi cha Kupambana na Ugaidi katika Jamhuri ya Czech. Kwa hisani ya Chuo cha Kupambana na Ugaidi

    Chanzo cha picha, Submitted photo

    Maelezo ya picha, Kwa hisani ya Chuo cha Kupambana na Ugaidi

    Rais Vladimir Putin ametoa idhini kwa watu wa kujitolea kutoka Mashariki ya Kati kupigania Urusi mashariki mwa Ukraine.

    "Ukiona kuna watu hawa wanataka kwa hiari yao wenyewe, sio pesa, kuja kusaidia watu wanaoishi Donbas, basi tunapaswa kuwapa wanachotaka na kuwasaidia kufikia eneo la migogoro," aliliambia Baraza la Usalama la Urusi.

    Waziri wa Ulinzi Sergei Shoigu alimwambia kuna watu 16,000 wa kujitolea katika Mashariki ya Kati ambao walikuwa tayari kuja Donbas.

    Kumekuwa na uvumi kwamba wanajeshi wa serikali ya Syria walio na vita kali wanaweza kulipwa na Urusi kupigana huko Ukraine.

    Jeshi la anga la Urusi na baadhi ya vitengo maalumu vimekuwa na jukumu muhimu kumuunga mkono Rais wa Syria Bashar al-Assad.

    Hapo awali serikali ya Ukraine ilisema kuwa inaunda kikosi cha waliojitolea raia wa kigeni walio tayari kuisaidiana na jeshi la Urusi katika mapambano.

    Rais Putin aliliambia Baraza hilo kuwa wafadhili wa nchi za Magharibi "walikuwa wakiajiri mamluki kwa ajili ya mzozo wa Ukraine "wazi, na kukiuka kanuni zote za sheria za kimataifa".

    Pia alikubaliana na pendekezo la Shoigu kwamba kukamata silaha za Magharibi - haswa makombora ya Javelin na makombora ya kutungulia ndege ya Stinger - yanaweza kukabidhiwa wapiganaji wanaoiunga mkono Urusi huko Donbas.

    Soma zaidi:

  7. Vita vya Ukraine: Msafara mkubwa wa Urusi umewekwa tena karibu na Kyiv - picha za satelaiti

    Wanaotaka kujitenga wanaoungwa mkono na Urusi mashariki mwa Ukraine wana siraha nzito

    Chanzo cha picha, AFP

    Maelezo ya picha, Wanaotaka kujitenga wanaoungwa mkono na Urusi mashariki mwa Ukraine wana siraha nzito

    Picha za satelaiti zilizopigwa na kampuni moja ya Marekani zinaonyesha msafara mkubwa wa kijeshi wa Urusi karibu na mji mkuu wa Ukraine, Kyiv, "umetumwa upya na kutawanywa kwa umbali mrefu".

    Msafara huo ulionekana mara ya mwisho karibu na Uwanja wa Ndege wa Antonov, kaskazini-magharibi mwa Kyiv, na mwenendo wake unaweza kuashiria msukumo mpya kuelekea mjini.

    Kampuni iliyopiga picha hizo, Maxar Technologies, ilisema sehemu za msafara huo ulikuwa katika maeneo ya miji jirani.

    Sehemu zingine ziko kaskazini zaidi, na makombora sasa yakiwa katika mkao wa kuwa tayari kurushwa.

    Upelekaji huo upya wa zana hizo za kivita unawadia wakati vikosi vya Urusi nchini Ukraine vimeanza kushambulia maeneo mapya yaliyolengwa katika maeneo tofauti ya nchi:

    • Uwanja wa ndege na kiwanda cha injini ya ndege vimelengwa huko Lutsk, kaskazini-magharibi
    • Milipuko pia ilipiga viwanja vya ndege huko Ivano-Frankivsk, kusini-magharibi, kulingana na maafisa wa ulinzi wa Urusi
    • Huko Dnipro, ngome kuu mashariki mwa Ukraine, mtu mmoja ameripotiwa kufariki dunia katika mashambulizi ya anga

    Soma zaidi:

  8. Kenya yaondoa masharti yaliyowekwa kupambana na corona

    Waliochanjwa waruhusiwa kwenda maeneo ya kuabudu

    Chanzo cha picha, AFP

    Maelezo ya picha, Waliochanjwa waruhusiwa kwenda maeneo ya kuabudu

    Wizara ya Afya ya Kenya imeondoa agizo la ulazima wa nchi nzima kuvaa barakoa ikiwa ni mwongozo uliorekebishwa na kutolewa hii leo.

    Katika agizo hilo jipya, Kagwe amesema karantini ya lazima, na kutengwa kwa kesi zilizothibitishwa za Covid-19 kumesimamishwa mara moja, na kuongeza kuwa wagonjwa wasio na dalili pia hawatahitaji kutengwa.

    Aidha, ukomo wa idadi ya watu katika maeneo ya kuabudu kwa wale waliopata chanjo pia imeondolewa, Waziri wa afya nchini Kenya Mutahi Kagwe amesema.

    Uchunguzi wa joto la lazima na uvaaji wa barakoa katika maeneo ya wazi na ya umma pia umeondolewa, isipokuwa kwa mikusanyiko ya ndani.

    Hatua hii inafuatia kupungua kwa kiwango cha maambukizi ya Covid-19 na visa vikali nchini.

    Wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika leo, Waziri wa Afya Mutahi Kagwe amesema viwango vya kuthibitisha kuwa na Covid-19 vimesalia chini ya 5% kwa mwezi mmoja uliopita.

    Hata hivyo waziri huyo wa afya amehamasisha umuhimu wa kuvaa barakoa na kuendeleza hatua ya kutokaribiana. Pia amesema kuwa hatua ya kuwekwa karantini itasitishwa.

    “Wakenya wanahimizwa kuvaa barakoa wanapohudhuria hafla za ndani. Tunapaswa pia kuona ukaguzi wa hali ya joto katika maeneo ya umma ukisimamishwa,” alisema, na kuongeza kuwa mikutano ya ndani ya kibinafsi sasa itaanza bila ukomo wa watu.

    Bw Kagwe pia amesema hatua za Covid-19 ambazo zimekuwepo kwa miaka miwili iliyopita zimesaidia na kuokoa maelfu ya maisha.

    Pia unaweza kusoma:

  9. Putin awakaribisha watu wanaojitolea kusaidia mapigano nchini Ukraine

    th

    Chanzo cha picha, EPA

    Tunaskia ripoti kwamba Rais wa Urusi Vladimir Putin ameunga mkono mipango ya kutuma wapiganaji wa kujitolea nchini Ukraine.

    Putin, akizungumza katika mkutano wa baraza la usalama la Urusi, alisema wale wanaotaka kujitolea kupigana na vikosi vinavyoungwa mkono na Urusi wanapaswa kuruhusiwa.

    Waziri wa Ulinzi wa Urusi Sergei Shoigu alisema kuna watu 16,000 wa kujitolea katika Mashariki ya Kati ambao walikuwa tayari kuja kupigana na vikosi vinavyoungwa mkono na Urusi, shirika la habari la Reuters linaripoti.

    Raia wengi wameuawa kuliko wanajeshi, asema mkuu wa ulinzi Ukraine

    Vikosi vya Urusi vimewauwa raia wengi zaidi wa Ukraine kuliko wanajeshi katika wiki mbili tangu uvamizi huo uanze, anasema Waziri wa Ulinzi wa Ukraine Oleksii Reznikov.

    "Nataka hii isikike sio tu huko Kyiv lakini ulimwenguni kote," anasema.

    Maoni yake yanakuja huku vikosi vya Urusi vikionekana kupanua mashambulizi yao dhidi ya nchi hiyo - na kuanzisha mashambulizi katika miji ya pande tofauti za nchi.

    Urusi yaishambulia Ukraine:Mengi zaidi

  10. Vita nchini Ukraine: Facebook kuruhusu wito wa ghasia dhidi ya Putin

    th

    Chanzo cha picha, Reuters

    Mmiliki wa Facebook na Instagram ataruhusu watumiaji katika baadhi ya nchi kuitisha vurugu dhidi ya Vladimir Putin na wanajeshi wa Urusi.

    Meta inasema imetoa ruhusa kwa muda kwa baadhi ya matamshi ya vurugu, kama "kifo kwa wavamizi wa Urusi," ambayo kwa kawaida inaweza kuvunja sheria zake.

    Hata hivyo, inasema haitaruhusu wito wa vurugu dhidi ya raia wa Urusi.

    Kujibu, Urusi iliitaka Marekani kusitisha "shughuli za itikadi kali" mtandao huo wa kijamii

    Tangazo hilo lilikuja baada ya shirika la habari la Reuters kusema kuwa limeona barua pepe za ndani zinazoelezea mabadiliko hayo ya sera.

    "Kwa kuzingatia uvamizi unaoendelea wa Ukraine tuliweka ubaguzi wa muda kwa wale walioathiriwa na vita, kuelezea hisia kali dhidi ya vikosi vinavyovamia," msemaji wa Meta aliiambia BBC.

    Chini ya sera hiyo iliyofanyiwa marekebisho, watumiaji katika nchi zikiwemo Urusi, Ukraine na Poland pia wataweza kutoa wito wa kuuawa kwa Rais Putin wa Russia na Rais wa Belarus Lukashenko.

    Barua pepe hizo zinaripotiwa kusema wito wa vifo vya viongozi hao utaruhusiwa isipokuwa kama zitakuwa na malengo mengine, au kujumuisha eneo au mbinu.

    Wito wa unyanyasaji dhidi ya Warusi pia unaruhusiwa wakati chapisho linarejelea wazi uvamizi wa Ukraine, barua pepe ziliripotiwa kusema

    "Tunazitaka mamlaka za Marekani kusitisha shughuli za itikadi kali za Meta, kuchukua hatua za kuwafikisha wahusika kwenye vyombo vya sheria," ubalozi wa Urusi nchini Marekani ulisema kupitia Twitter

    "Watumiaji wa Facebook na Instagram hawakuwapa wamiliki wa majukwaa haya haki ya kuamua vigezo vya ukweli na kugombanisha mataifa dhidi ya kila mmoja," iliongeza.

    Ruka X ujumbe
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa X ujumbe

    Urusi yaishambulia Ukraine:Mengi zaidi

  11. Tanzania yazindua chanjo ya homa ya manjano huku kukiwa na mlipuko wa ugonjwa huo

    th

    Chanzo cha picha, AFP

    Wizara ya afya ya Tanzania imezindua zoezi la utoaji chanjo ya homa ya manjano baada ya mlipuko wa ugonjwa huo kuripotiwa katika nchi jirani ya Kenya.

    Waziri Ummy Mwalimu amewaagiza watendaji wa hospitali ya rufaa ya mkoa kuanza kutoa chanjo kwa wale wote wanaosafiri nje ya nchi.

    th

    Wizara ya afya ya Kenya ilitangaza mlipuko wa homa ya manjano wiki jana.

    Watu 15 waliripotiwa kuugua ugonjwa huo na watu watatu walithibitishwa kufariki.

    Waziri Mwalimu amewaagiza wataalam wanaosimamia masuala ya afya mipakani kuangalia uwezekano wa kutoa vyeti vya chanjo ya kielektroniki ili kukabiliana na changamoto ya vyeti feki.

    Pia ametoa wito kwa watanzania kuchukua tahadhari ili ugonjwa huo usiingie nchini na kuhakikisha mazingira yanakuwa safi ili kuzuia mbu kuzaana

    th
  12. Nigeria yanasa mamia ya magunia ya nyama ya punda

    TH

    Chanzo cha picha, AFP

    Maafisa wa forodha wa Nigeria wanasema wamenasa magunia 1,390 ya nyama ya punda katika jimbo la kaskazini-magharibi la Kebbi karibu na mpaka na Niger.

    Uchunguzi wa awali ulionyesha takriban punda 1,000 walichinjwa na nyama zao kuwekwa kwenye magunia, kulingana na Joseph Attah, mkuu wa forodha katika eneo hilo.

    Aliitaja ‘’biashara haramu ya wanyamapori’’ ambayo inakiuka sheria za Nigeria.

    Magunia hayo yalikuwa yakisafirishwa kwa lori ambalo halikufahamika mara moja lilikoelekea.

    Dereva wa lori hilo na mshukiwa mwingine mmoja wamekamatwa na watafunguliwa mashtaka, maafisa walisema.

    Nigeria imekuwa ikijitahidi kukabiliana na mauaji ya punda na biashara haramu ya sehemu zao huku idadi ya wanyama hao ikiendelea kupungua kwa kasi.

    Hapo awali, maafisa wa Nigeria walisema sehemu za mwili wa punda - ikiwa ni pamoja na ngozi - zilisafirishwa kwa magendo hadi nchi za Asia ikiwa ni pamoja na Uchina ambako inaaminika zilitumika kutengeneza dawa za asili na vipodozi.

  13. Mashambulizi ya Urusi yanasonga magharibi, katika miji mipya

    th

    Chanzo cha picha, Ukraine State Emergency Services

    Tumeona safu mpya ya mashambulizi kutoka kwa wanajeshi wa Urusi asubuhi ya leo - makombora yakipiga viwanja vya ndege katika miji ya magharibi ya Lutsk na Ivano-Frankivsk.

    Pia wameshambulia ngome ya kati-magharibi ya Dnipro kwa mara ya kwanza tangu uvamizi huo uanze zaidi ya wiki mbili zilizopita.

    Wakimbizi kutoka miji iliyokumbwa na mashambulizi ya mabomu wamekuwa wakikimbilia magharibi mwa Ukraine wakiamini kuwa ni salama zaidi. Makumi ya maelfu wamepitia Lviv - kitovu kikubwa cha raia. Mashambulizi ya Ijumaa yanalenga miji ya pande zote mbili.

    Meya wa Ivano-Frankivsk amethibitisha kushambuliwa kwa makombora na Urusi katika mji wake kusini-magharibi mwa Ukraine.

    Katika ujumbe wa Facebook, alisema: "Adui alimpiga Frankivsk."

    Aliwataka watu kutoshiriki picha na video za milipuko hiyo na alionekana kupendekeza mfumo wa kengele wa mgomo wa makombora haufanyi kazi.

    Na aliwaonya wakazi wa wilaya za Krykhivtsi, Chukalovka, Opryshivtsi, Gorodok wasiondoke majumbani

    "Kaa nyumbani kwa usalama wako! Wakati hatari itapita - nitakufahamisha," anaongeza.

    Vikosi vinavyoungwa mkono na Urusi vilikamata Volnovakha, ripoti zinasema

    Huku mashambulizi mapya yakiripotiwa kote Ukraine, sasa kuna ripoti kwamba watu wanaotaka kujitenga wanaoungwa mkono na Urusi wameuteka mji muhimu wa kimkakati wa Volnovakha, kaskazini mwa bandari iliyozingirwa ya Mariupol, shirika la habari la RIA limenukuu wizara ya ulinzi ya Urusi ikisema.

    th

    Urusi yaishambulia Ukraine:Mengi zaidi

  14. Vifo vya Covid huenda ni mara tatu zaidi kuliko ilivyoripotiwa

    th

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Zaidi ya watu milioni 18 - mara tatu zaidi ya rekodi rasmi zinaonyesha - labda wamekufa kwa sababu ya Covid, watafiti wanasema.

    Ripoti yao inakuja miaka miwili hadi siku tangu Shirika la Afya Ulimwenguni lilipotangaza janga hilo kwa mara ya kwanza.

    Timu inayochunguza vifo vya ziada vilivyotokana na Covid-19 katika Chuo Kikuu cha Washington cha Marekani kiliziangazia nchi na maeneo 191 kwa kile wanachokiita idadi ya kweli ya vifo ulimwenguni.

    Vifo vingine vilitokana na virusi, wakati vingine vilihusishwa na maambukizi.

    Hii ni kwa sababu kuambukizwa Covid kunaweza kuzidisha hali zingine za matibabu zilizokuwepo, kama vile ugonjwa wa moyo au mapafu, kwa mfano.

    Kipimo kilichotumiwa kinaitwa vifo vya ziada - ni watu wangapi wamekuwa wakifa kuliko inavyotarajiwa ikilinganishwa na miaka ya hivi karibuni, kabla ya janga hilo kukumba.

    Ili kukokotoa hili, watafiti walikusanya data kupitia utafutaji wa tovuti mbalimbali za serikali, Hifadhidata ya Vifo vya Dunia, Hifadhidata ya Vifo vya Binadamu, na Ofisi ya Takwimu ya Ulaya.

    Viwango vya vifo vilivyokithiri vinakadiriwa kutofautiana sana kulingana na nchi na eneo, lakini kiwango cha jumla cha kimataifa kilichohesabiwa katika utafiti huo ni vifo 120 kwa kila watu 100,000.

    Hiyo itamaanisha takriban vifo milioni 18.2 vimetokea kwa sababu ya Covid katika miaka miwili kati ya 2020 na mwisho wa 2021 - mara tatu zaidi ya milioni 5.9 rasmi ambayo imerekodiwa.

    Makadirio ya vifo vya ziada yalihesabiwa kwa muda wote wa utafiti wa kipekee, na si kwa wiki au mwezi, kwa sababu ya kuchelewa na kutofautiana katika kuripoti data ya kifo cha Covid ambayo inaweza kubadilisha sana makadirio, wachunguzi walisisitiza.

    Kulingana na utafiti huo, ambao umechapishwa katika gazeti la The Lancet, viwango vya juu zaidi vilikuwa katika nchi za kipato cha chini katika Amerika ya Kusini, Ulaya na Kusini mwa Jangwa la Sahara. Lakini vifo pia vilikuwa vya juu katika nchi zingine zenye mapato ya juu, kama vile Italia na sehemu za Amerika.

    Nchi tano zilizo na makadirio ya juu ya viwango vya vifo vya ziada ni:

    • Bolivia

    • Bulgaria

    • Eswatini

    • Makedonia Kaskazini

    • Lesotho

    Tano ziliozkuwa na viwango vya chini kabisa ni:

    • Iceland

    • Australia

    • Singapore

    • New Zealand

    • Taiwan

  15. Habari za hivi punde, Lutsk na Dnipro zashambuliwa kwa mara ya kwanza - ripoti

    Kumekuwa na ripoti za milipuko katika miji ya pande tofauti za nchi katika muda wa nusu saa iliyopita.

    Televisheni za Kiukreni na vyombo vya habari vinaripoti milipuko huko Lutsk kaskazini-magharibi, na vile vile huko Dnipro - jiji la bara lililoko kwenye mto Dnieper na ngome kuu katikati mwa mashariki mwa Ukraine.

    Hakuna hata moja ya miji hii ambayo imeshambuliwa kwa makombora ya moja kwa moja hapo awali.

    Ving'ora vya mashambulizi ya anga vilisikika katika miji kadhaa nchini Ukraine saa chache kabla ya milipuko hiyo.

    th

    Urusi yaishambulia Ukraine:Mengi zaidi

  16. Jussie Smollett ahukumiwa siku 150 jela katika kesi shambulio la uwongo

    th

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Muigizaji wa Marekani Jussie Smollett amehukumiwa kifungo cha siku 150 jela baada ya jopo la mahakama kugundua kuwa alidanganya polisi kuhusu kuwa mhasiriwa wa uhalifu wa chuki.

    Nyota huyo wa zamani wa Empire, mwenye umri wa miaka 39, alipatikana na hatia mwezi Desemba kwa mashtaka matano ya kufanya fujo baada ya kutoa taarifa za uongo kuhusu shambulio hilo la uwongo.

    Adhabu hiyo pia inajumuisha miezi 30 ya muda wa uangalizi na $145,000 (£110,000) kama marejesho na faini.

    Kufuatia hukumu hiyo, Smollett alisema: "Sikufanya hivi!"

    Kesi hiyo ilitokana na tukio la miaka mitatu iliyopita ambapo Smollett alisema alishambuliwa na watu wawili.

    Muigizaji huyo, ambaye ni mweusi na mpenzi wa jinsia moja alisema washambuliaji walimzomea na kauli mbiu ya Trump, wakamtupia "dutu ya kemikali" na kumfunga kitanzi shingoni alipokuwa akitembea usiku wa manane Januari 2019.

    Mamlaka ilifungua uchunguzi, lakini mnamo Februari mwaka huo, polisi walimshtaki Smollett kwa kuwasilisha ripoti ya uwongo kwa polisi, akidai alikuwa amefanya shambulio hilo.

    Katika kesi ya mwaka jana, jopo la wanasheria wanaume sita na wanawake sita iliyosikilizwa kutoka kwa ndugu Abimbola na Olabinjo Osundairo, ambao walitoa ushahidi kwamba Smollett aliwalipa kuandaa shambulio hilo na kuwalipa dola 3,500 kutekeleza shambulio hilo.

    Smollett alikabiliwa na kifungo cha hadi miaka mitatu jela kwa kila moja ya makosa matano. Siku 150 za kwanza za kipindi chake cha uangalizi kitawekwa kizuizini, kuanza mara moja.

    Ni lazima pia alipe $120,106 kwa jiji la Chicago na $25,000 kama faini kiwango cha juu kinachoruhusiwa na sheria.

    Wakati wote wa kesi hiyo, Smollett alishikilia kuwa alikuwa mwathirika wa uhalifu.

  17. IS yathibitisha kifo cha kiongozi wake Quraishi na kumtaja mrithi wake

    th

    Chanzo cha picha, US DEPARTMENT OF STATE

    Maelezo ya picha, Abu Ibrahim al-Qurayshi alikuwa mwanajihadi mkongwe wa Iraq ambaye jina lake halisi lilikuwa Amir Mohammed al-Mawla.

    Kundi la Islamic State (IS) limemtaja kiongozi mpya baada ya kuthibitisha kifo cha Abu Ibrahim al-Qurayshi.

    Ujumbe wa sauti uliotumwa mtandaoni ulisema Abu al-Hassan al-Hashemi al-Qurayshi sasa ni "khalifa", bila kutoa maelezo zaidi kuhusu utambulisho wake.

    Ujumbe huo haukutaja jinsi, wapi au lini Abu Ibrahim al-Qurayshi alikufa.

    Marekani imesema mwanajihadi huyo wa Iraq alijilipua na kuua familia yake wakati wa shambulio la kikosi maalum kwenye maficho yake kaskazini-magharibi mwa Syria tarehe 3 Februari.

    Rais Joe Biden alisema kifo chake "kiliondoa tishio kubwa la kigaidi kwa ulimwengu", akimtuhumu kwa kusimamia kuenea kwa washirika wa IS duniani kote na kuwa "kikosi kinachoendesha" mauaji ya kimbari ya watu wa Yazidi.

    Ujumbe wa sauti wa Alhamisi uliwasilishwa na msemaji mpya wa IS, Abu Umar al-Muhajir, ambaye alifichua kuwa mtangulizi wake Abu Hamza al-Qurayshi pia alifariki hivi karibuni.

    Muhjair alisema hawezi kufichua jina halisi la kiongozi huyo mpya, lakini aliwataka wafuasi wake kuapa utii kwake.

    Kumekuwa na uvumi kwamba mgombea anayewezekana zaidi alikuwa mtu wa Iraqi anayeitwa Bashar Khattab Ghazal al-Sumaidai, anayejulikana pia kama Abu Khattab al-Iraqi, Hajji Zaid na Ustath Zaid.

    IS wakati fulani ilishikilia kilomita za mraba 88,000 (maili za mraba 34,000) kutoka mashariki mwa Iraq hadi magharibi mwa Syria na kuweka utawala wake wa kikatili kwa karibu watu milioni nane.

    Kundi hilo lilifurushwa kutoka eneo lake la mwisho mwaka 2019, lakini Umoja wa Mataifa unakadiria kuwa bado lina wapiganaji kati ya 6,000 na 10,000 nchini Syria na Iraq ambao wanaendelea kufanya mashambulizi ya kugonga na kukimbia, kuvizia na milipuko ya mabomu kando ya barabara.

    Kifo cha Abu Ibrahim al-Qurayshi katika jimbo la Syria linaloshikiliwa na upinzani la Idlib kimekuja siku chache baada ya shambulio kubwa la IS kwenye jela inayodhibitiwa na Wakurdi katika mji wa kaskazini-mashariki wa Syria wa Hassakeh - operesheni muhimu zaidi ya kundi hilo kuwahi kutokea kwa miaka mingi.

    Takriban walinzi 121, wapiganaji wa wanamgambo wanaoongozwa na Wakurdi na raia waliuawa katika wiki moja ya makabiliano makali, pamoja na wafungwa 374 na washambuliaji wa IS, maafisa walisema.

    Mapema wiki hii, kundi la waangalizi lilisema kuwa IS ndiyo iliyohusika na shambulio dhidi ya basi la kijeshi katika jangwa la kati la Syria na kusababisha vifo vya wanajeshi 15 wa serikali.

  18. Majeshi ya Urusi yazingira Kyiv na miji mingine-Ukraine inahofia kitakachofuata

    TH

    Chanzo cha picha, Reuters

    Picha za satelaiti za msafara wa Urusi karibu na Kyiv zinaonekana kuonyesha vikosi vikitumwa tena katika maeneo ya karibu, na hivyo kuashiria msukumo mpya kuelekea mji mkuu wa Ukraine.

    Kulingana na Maxar Technologies, sehemu ya msafara huo - ambao ulionekana mara ya mwisho kaskazini-magharibi mwa Uwanja wa Ndege wa Antonov ulio karibu - umehamia katika miji inayozunguka.

    Maxar ilisema kuwa picha zinaonyesha sehemu zingine za msafara wa kaskazini zimejipanga karibu na Lubyanka, na kuweka sehemu za mizinga karibu.

    Mapema siku ya Alhamisi, afisa mkuu wa ulinzi wa Marekani alisema kuwa vikosi vya Urusi vimesogea maili tatu (5km) karibu na Kyiv katika muda wa saa 24 zilizopita.

    TH

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Wanajeshi wanaonekana wamekusanyika kati ya miti karibu na Lubyanka
    TH

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Ushahidi wa harakati za askari huko Ozera, kaskazini-mashariki mwa Uwanja wa Ndege wa Antonov
    TH

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Satelaiti pia zilinasa moto uliokuwa ukiwaka katika eneo la viwanda katika mji wa kaskazini wa Chernihiv
    TH

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Wakimbizi kutoka Kyiv wanaonekana na shehena ya magari wakisubiri kuvuka daraja lililoharibika huko Irpin

    Matukio ya hivi karibuni

    Ikiwa unajiunga nasi, au unataka muhtasari, haya ni matukio ya hivi punde kuhusu uvamizi wa Urusi nchini Ukraine:

    • Marekani imeonya kwamba vikosi vya Urusi vimezunguka miji 'mingi' ya Ukraine na kuharibu miundombinu muhimu

    • Katika jiji moja kama hilo, Mariupol, Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu imeonya kwamba vifaa vinapungua

    • Urusi, kwa upande wake, imeripotiwa kusema itafungua njia za kibinadamu kati ya Ukraine na Urusi

    • Mazungumzo ya amani kati ya mawaziri wa mambo ya nje wa Urusi na Ukraine nchini Uturuki yalipata mafanikio kidogo, na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron alisema haoni uwezekano mdogo kwamba mazungumzo hayo yatasababisha kusitishwa kwa mapigano hivi karibuni.

    • Serikali za Marekani na Uingereza zimeeleza tena wasiwasi kuwa huenda Urusi ikatumia silaha za kemikali au za kibayolojia

    • Wataalamu wa masuala ya kiuchumi wametabiri kuwa uchumi wa Urusi utapungua hadi 15% huku vikwazo vikiendelea kuiathiri

    Urusi yaishambulia Ukraine:Mengi zaidi