Waasi wa ADF raia wa Tanzania wakamatwa DRC

Jeshi la taifa la Kongo FARDC limetangaza kuwakamata raia watatu wa Tanzania ambao ni waasi wa ADF waliosajiliwa wilayani Beni mashariki mwa Kongo.

Moja kwa moja

  1. Kituo cha sheria Tanzania chapendekeza waziri kutopewa mamlaka ya kumtangaza mtu kuwa gaidi

    Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kimependekeza kuondolewa kifungu kinachompa mamlaka Waziri wa Mambo ya ndani wa Tanzania kumtangaza mtu kuwa gaidi wa ndani ya nchi.

    Hata hivyo, iwapo sheria hiyo itapitishwa na Bunge la Tanzania, basi Waziri huyo atakuwa na mamlaka kutangaza mtu au kikundi cha watu kuwa wahusika wa ugaidi.

    Mwanasheria ambaye pia ni Mkurugenzi wa Utetezi na Maboresho wa LHRC, Flugence Massawe ameeleza kuwa wabunge wanapaswa kupitia kwa umakini vifungo vya sheria hiyo inayotarajiwakwani itakapopitishwa bila kuchakatwa vyema inaweza kuwa na madhara makubwa kwa taifa.

    Tayari wadau mbalimbali walishapata fursa ya kukutana naKamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kwa ajili ya kuchambua mapendekezo hayo ya Serikali yaliyowasilishwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

    Massawe alisema, “Tumefikia hatua ya kupinga hayo mapendekezo kwasababu tumeona hayana tija kwa taifa letu, kumpa waziri mamlaka hayo ni hatari kwa kuwa anaweza kuyatumia mamlaka hayo vibaya. Nafikiri tungeangalia pia nchini ya Kenya ilivyo, si mtu mmoja tu anatangaza mwingine ni gaidi bali wenzetu wanaketi katika baraza la mawaziri ili kutangaza…

    “…unapompa mtu mmoja mamlaka ya kutangaza gaidi, hata kiuchumi tunaweza kuumia kwani mtu kama mtalii au mwekezaji kutoka nje ataogopa kuja Tanzania. Hii ni hatari sana,” alisema.

  2. Wasi wasi watanda baada ya watu wenye silaha kulenga kituo cha redio Guinea-Bissau

    polisi

    Chanzo cha picha, AFP

    Maelezo ya picha, Wanajesi wakilinda majengo ya serikali

    Sauti nzito za milio ya risasi zilisikika katika mji mkuu wa Guinea Bissau ziliusababisha mkanganyiko na wasi wasi miongoni mwa wafanyakazi wa umma karibu wiki moja baada ya jaribio la mapinduzi .

    Lakini shambulio hilo lililofanywa na watu wenye silaha wasiojulikana halikuwa katika majengo ya ofisi za serikali bali lilitokea katika kituo binafsi cha redio.

    Vifaa vya kituo hicho kinachofahamika kama-Capital Radio – kikiwemo cha kupeperusha matangazo, pamoja na kompyuta viliharibiwa.

    Kituo hicho kina ushirikiano na redio ya kimataifa ya Marekani , Voice of America (VOA), lakini haijawa wazi ni nani aliyefanya shambulio hilo ,au ni kwanini.

    Kituo hicho hicho cha redio kiliwahi kushambuliwa Julai, 2020.

    Baada ya kusikia milio ya risasi, baadhi ya wafanyakazi wa umma walionekana wakitoroka kwenda nyumbani.

    Takriban watu 11 waliuawa Jumanne wiki iliyopita wakati wanajeshi walipofanya jaribio la mapinduzi ya kumng’oa madarakani Rais Umaro Sissoco Embaló, kulikana na maafisa.

    Rais ametangaza uchunguzi juu ya jaribio la mapinduzi.

  3. Waasi watatu wa ADF raia wa Tanzania wakamatwa DRC

    Ingabo za DR Congo, FARDC, zikambitse mu gace ka Beni aho ziri mu mirwano n'inyeshyamba za ADF

    Chanzo cha picha, FARDC

    Maelezo ya picha, Vikosi vya DR Congo, FARDC, vikipiga kambi katika eneo la eni kwa mapambano dhidi ya ADF

    Jeshi la taifa la Kongo FARDC limetangaza kuwakamata raia watatu wa Tanzania ambao ni waasi wa ADF waliosajiriwa wilayani Beni mashariki mwa Kongo.

    Raia hao wa Tanzania, walikamatwa Jumapili hii, Februari 6, 2022 wakati wa doria zilizofanywa na askari wa Kongo katika bonde la Mwalika, katika eneo la Beni Kivu Kaskazini.

    Kulingana na taarifa ya msemaji wa secteur (tarafa) ya Sokola 1 Kivu Kaskazini, Kapteni Athony Mwalushayi ; waasi hao wamekiri kuwa walisajiriwa kwa nia mbaya na raia wa Kongo ambaye aliwadanganya kwamba watafanya kazi katika migodi ya dhahabu, lakini wakajikuta katika kikundi cha waasi wa ADF.

    Akizungumza na BBC, Kapteni Athony Mwalushayi amesema, waasi hao raia wa Tanzania wako sasa mikononi mwa idara husika ili waandelee kuchunguzwa.

    Waasi

    Chanzo cha picha, AFP

    Maelezo ya picha, Vikosi vya Uganda vimekuwa vikilinda mpaka wake dhidi ya waasi wa ADF

    Mnamo Januari 28, katika eneo hilo hilo la Beni, FARDC pia lilimkamata muasi wa ADF, raia wa Kenya, Salim Muhammad, ambaye alikuwa anasambaza video za ukatili.

    Januari 9, 2022, Benjamin Kisokeranio, mkuu wa tawi la ADF la muasi Jamil Mukulu, alikamatwa Uvira katika jimbo la Kivu Kusini.

  4. Aberdares: Hifadhi iliyowahi kutembelewa na Malkia wa Uingereza yashika moto Kenya

    Mbuga ya wanyamapori ya Aberdare

    Chanzo cha picha, afp/twitter

    Maelezo ya picha, Mbuga ya wanyamapori ya Aberdare

    Kikosi cha wazima moto kimetumwa kusaidia kukabiliana na moto mkubwa ambao umeteketeza eneo kubwa la msitu wa Aberdares katikati mwa Kenya.

    Chanzo cha moto huo ulioanza Jumamosi bado hakijajulikana.

    Moto huo upo ndani ya mbuga ya Taifa ya Aberdares inayohifadhi wanyamapori wakiwemo tembo na faru walio hatarini kuangamia.

    Pia ni eneo ambalo ni maarufu kwa hoteli ya Treetops ambapo Malkia Elizabeth II alikuwepo mnamo mwaka wa 1952- wakati kifo cha babake kinatokea na kuingia kwenye ufalme wa Uingereza)

    Video na picha bado zinaonyesha wenyeji kutoka karibu na mbuga ya kitaifa ya Aberdares wakitumia matawi na ndoo za maji kujaribu kuudhibiti moto mkubwa ulioanza mwishoni mwa juma.

    Wazima moto waliobobea sasa wamesafirishwa kwa ndege hadi eneo hilo huku moto ukiendelea kuharibu maeneo mengi ya ardhi.

    Hadi kufikia sasa chanzo cha moto huo bado hakijafahamika wala kiwango kamili cha uharibifu.

    Aidha, moto huo unajiri wakati nchi ikikumbwa na ukame katika maeneo mbalimbali kufuatia msimu wa mvua kushindwa kunyesha.

    Wanasayansi wamelaumu mabadiliko ya hali ya hewa kwa misimu mirefu ya kiangazi katika sehemu nyingi nchini humo.

    Aberdares ni mfumo wa ikolojia muhimu sana nchini Kenya, nyumbani kwa idadi kubwa ya tembo na faru weusi walio hatarini kutoweka.

    Hata hivyo, hii si mara ya kwanza kushuhudiwa kwa tukio hilo ikikumbukwa kwamba mwaka 2017 na 2018, pia kulitokea moto mkubwa.

  5. Afisa mkuu wa Umoja wa Mataifa atembelea kaburi la halaiki kaskazini mwa Ethiopia

    Naibu katibu mkuu wa UN

    Chanzo cha picha, @fanatelevision

    Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina Mohammed ametembelea maeneo yaliyoathiriwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya serikali na washirika wake na waasi wa Tigray katika eneo la Amhara nchini Ethiopia.

    Bi Mohammed ametembelea kaburi la halaiki Jumapili na mtangazaji wa serikali Fana akatuma picha kwenye Twitter:

    Ruka X ujumbe
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa X ujumbe

    Bi Mohammed pia alifanya mazungumzo na maafisa wa eneo ili kujadili athari za vita vya wenyewe kwa wenyewe.

    Ujumbe wa Umoja wa Mataifa pia umetembelea Mekelle, mji mkuu wa eneo la Tigray.

    Serikali inawatuhumu waasi hao kwa mauaji na uharibifu wa taasisi katika maeneo waliyokuwa wameyadhibiti katika mikoa ya Amhara na Afar, na kwa upande wao wanashutumu vikosi vya serikali kwa ukatili mwingi.

    Unaweza kusoma pia:

    • Mzozo wa Ethiopia wa Tigray: Lalibela yachukuliwa tena - serikali
    • Mgogoro wa Ethiopia wa Tigray: Jinsi TPLF ilivyolizidi maarifa jeshi la Ethiopia
  6. Kenya: Waziri awaonya walimu dhidi ya kuwachapa viboko wanafunzi

    wanafunzi

    Waziri wa elimu nchini Kenya amewakumbusha watu kwamba adhabu ya viboko imesalia kuwa marufuku katika shule za nchini humo.

    Akiwa ziarani katika eneo la pwani, George Magoha amesema walimu watakaopatikana wakiwapiga wanafunzi watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.

    Kauli yake inajiri siku chache baada ya mwanafunzi katika eneo hilo kupigwa kwasababu ya kula chapati tano ikiwa ni zaidi ya zile ambazo walikuwa wamepangiwa kula.

    Kipigo hicho kilimfanya mwanafunzi huyo wa kiume kupata majeraha kwenye figo na sehemu zake za siri na kulazwa hospitalini.

    Mwalimu mkuu wa shule hiyo na mwalimu mwingine walikamatwa.

    Maafisa elimu mkoani humo walifunga shule hiyo baada ya ukaguzi kuonesha haijasajiliwa na ina masuala ya usafi.

    Waziri Magoha amesema shule ambazo zina masuala ya kufuata sheria zitafungwa na wanafunzi kuchukuliwa katika shule za jirani.

  7. Rwanda: Mitaa kadhaa yaboreshwa miundo mbinu kuwavutia watalii

    th

    Chanzo cha picha, John Gakuba

    Manispaa ya jiji la Kigali ,Rwanda, inaendelea na harakati za kupanua maeneo ya vivutio vya watalii kwa kufunga baadhi ya mitaa na kuirembesha kwenye maeneo maarufu kama ''free car zone''.

    Mtaa wa Biryogo ujulikanao tangu zama kama uswahilini ni kati ya maeneo takriban 100 yanayolengwa na serikalikuboreshwa miundo mbinu yake mbali mbali na mengineo kama kupandwa kwa miti ,maua na mtandao usiolipiwa.

    Kulingana na mwandishi wa BBC kutoka Kigali John Gakuba kati kati ya barabarazilizopambwa kwa rangi mbali mbali mithili ya mwendo wa zigzag, wateja wameketi chini ya miavuli na wengine wamekaa barazani wakishiriki chai aina tofauti za vitafunwa .

    th

    Chanzo cha picha, John Gakuba

    Mitaa ya Biryogo ambayo imekuwa na kunawiriina historia ya kuwa chimbuko la jamii ya waislamu nchini Rwanda.

    kuna wateja kutoka maeneo mbali mbali ya jiji wanakuja kuvinjari na kupata burudani, mkao kwa sehemu kubwa ukiambatana rika mahusiano ama maslahi.

    Saa za jioni jioni ndipo watu wengi hukusanyika hasa katika mazingira haya huku vijana wa kujitolea waliovalina sare moja wakifuatilia utekelezaji wa masharti ya kuepuka maambukizi dhidi ya uviko-19.

    Baadhi ya wamiliki wa nyumba kwenye mitaa hii wameelezea hofu kuhusu majaliwa yao kuishi katika jiji lenye kasi ya maedeleo na uwezekano wa kulihama jiji kutokana na kukosa uwezo wa kujenga ama kukarabati nyumba maskani yao.

    TH

    Chanzo cha picha, John Gakuba

    Lakini kwa upande mwingine wanajipa moyo kwani wamepewa vibali vya kukarabati nyumba zao ama vibanda vilivyochakaa kutoka kwa utawala wa manispaa ya jiji la Kigali.

    Kulingana na afisa mwandamizi wa manispaa ya jiji la Kigali anayehusika na sanaa na uchoraji, Muhirwa Solange, manispaa ya Kigali imeshapata maeneo takriban mia jijini hapa ambapo kutawekwa maeneo ya vivutio vya watalii car free zone na mkaazi atawajibika kutumia nguvu zake za kifedha kukarabati mazingira yake kukiwemo maskani.

  8. Ujerumani yafikiria kusitisha operesheni yake ya kijeshi nchini Mali

    th

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Waziri wa ulinzi wa Ujerumani amedokeza kuwa hakuna uwezekano kuwa nchi hiyo itaweza kudumisha wanajeshi wake nchini Mali, huku hali ya wasiwasi ikiongezeka kati ya watawala wa kijeshi nchini humo na washirika wa kimataifa.

    Christine Lambrecht alisema anahisi kwamba wanajeshi wa Ujerumani hawahitajiki tena nchini Mali ambako wamekuwa wakisaidia katika vita dhidi ya wapiganaji wa jihadi.

    Ujerumani ina takriban wanajeshi 1,200 huko kama sehemu ya mpango wa kukabiliana na ugaidi na kulinda amani.

    Ni ishara zaidi kwamba operesheni ya kimataifa - inayoongozwa na Ufaransa - kukabiliana na ugaidi huko iko katika hatari ya kusambaratika.

    Ufaransa imeongoza ukosoaji wa watawala wa kijeshi huko Bamako baada ya kufutilia mbali mipango ya uchaguzi na kusema wanataka kusalia madarakani kwa miaka kadhaa.

    Mwezi Desemba, nchi 16 - nyingi zaidi za Ulaya - zililaani uamuzi wa Mali kufanya kazi na wanakandarasi wa kijeshi wa kibinafsi kutoka kundi la Wagner la Kirusi.

    Hatua hiyo inaweza kubadilisha kwa kiasi kikubwa mwitikio wa jumla kwa tishio la wapiganaji wa jihadi katika eneo la Sahel.

  9. Rais Museveni aondoa zuio la boda boda kuhudumu usiku

    Rais Yoweri Museveni wa Uganda, hatimaye ameondoa zuio la usiku kuanzia saa moja hadi saa kumi na moja asubuhi kwa waendesha boda boda nchini humo.

    Tangu kufunguliwa sehemu zote za uchumi nchini Uganda mnamo mwezi Januari 2022, boda boda waliendelea kuzuiwa kutembea usiku kuthibiti kueneo kwa ugonjwa wa corona sharti ambalo lilikuwa limewekwa tangu zuio la kwanza la mwaka 2020.

    Ruka X ujumbe
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa X ujumbe

    Rais Museveni jana katika sherehe ya maadhimisho ya miaka 41 ya jeshi lake lilipozindua harakati za kuondoa utawala uliokuwepo wakati huo zilizofanyika mjini Mbale mashariki mwa Uganda, alitangaza kuondoa zuio la boda boda kuanzia leo saa kumi na mbili jioni.

    Boda boda ni usafiri wa haraka nchini Uganda, na baada ya kuruhusiwa tena kuanza kwa shughuli za kiuchumi, watu wengi wanaofanya kazi nyakati za usiku walihitaji usafiri wa boda boda.

    Sasa kuanzia leo, boda boda zitafanya kazi saa 24.

  10. Senegal yatangaza likizo ya umma baada ya kushinda kombe la Afcon

    TH

    Chanzo cha picha, AFP

    Rais wa Senegal Macky Sall ametangaza Jumatatu kuwa siku ya mapumziko kusherehekea ushindi wa timu ya taifa wa Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon).

    Rais ambaye alikuwa nje ya nchi amefutilia mbali awamu ya mwisho ya safari yake ili kuwakaribisha nyota hao wa soka kurejea nchini siku ya Jumatatu.

    Rais Sall ataitunuku timu hiyo Jumanne katika ikulu ya rais, televisheni ya RTS ilisema.

    Senegal ilishinda fainali ya kwanza ya Afcon baada ya kushindwa mara mbili katika fainali mwaka 2002 na 2019.

    Waliishinda Misri 4-2 kwa mikwaju ya penalti na kupata ushindi wao baada ya fainali kumalizika bila bao kufuatia muda wa nyongeza.

    Wakati huo huo, raia wameendelea kusherehekea usiku kucha kuamkia Jumatatu katika miji mbalimbali nchini Senegal kufuatia ushindia wa Kombe la Mataifa ya Afrika.

    Video zinaonesha mashabiki wa timu hiyo wakiwa wanapeperusha bendera ya taifa hilo wakiwa wanacheza densi pamoja na ujumbe kutoka kila pembe uliokuwa unamiminika kwenye mitandao ya kijamii.

    Ruka X ujumbe, 1
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa X ujumbe, 1

    Msisimko huo haukuweza kufichika hata katika sehemu za burudani:

    Ruka X ujumbe, 2
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa X ujumbe, 2

    Kwenye barabara mbalimbali, watu walisherehekea ushindi huo kwa aina yake

    Ruka X ujumbe, 3
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa X ujumbe, 3

    Senegal iliishinda Misri kwa mikwaju ya penalti 4-2 na kutwaa ushindi wa kwanza wa Afcon baada ya kushindwa mara mbili katika fainali zilizopita.

    Kocha Aliou Cissé ambaye kama mchezaji alikosa penalti muhimu katika kushindwa kwa fainali ya 2002 na alikuwa kocha wakati timu hiyo iliposhindwa katika fainali miaka mitatu iliyopita alisifiwa mtandaoni:

    Ruka X ujumbe, 4
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa X ujumbe, 4

    Senegal na Misri zitakutana tena katika mechi nyingine mwezi ujao kwenye mchujo wa kuwania kufuzu kwa Kombe la Dunia 2022 nchini Qatar.

  11. Programu ya makombora ya Korea Kaskazini ilifadhiliwa kupitia sarafu za kidigitali zilizoibiwa- UN

    th

    Chanzo cha picha, Reuters

    Mashambulizi ya mtandaoni ya Korea Kaskazini yameiba mamilioni ya dola za sarafu ya digitali ili kufadhili programu za makombora nchini humo, ripoti ya Umoja wa Mataifa iliyoarifu vyombo vya habari inasema.

    Kati ya 2020 na katikati ya 2021 wavamizi wa mtandao waliiba zaidi ya dola milioni50 (£37m) ya mali ya kidigitali, wachunguzi walibaini.

    Mashambulizi kama haya ni "chanzo muhimu cha mapato" kwa programu ya nyuklia na makombora ya balestiki ya Pyongyang, walisema.

    Matokeo hayo yaliripotiwa kukabidhiwa kwa kamati ya vikwazo ya Umoja wa Mataifa siku ya Ijumaa.

    Mashambulizi hayo ya mtandaoni yalilenga takribani ubadilishanaji wa awamu tatu wa sarafu za kimtandao huko Amerika Kaskazini, Ulaya na Asia.

    Ripoti hiyo pia ilirejelea utafiti uliochapishwa mwezi uliopita na kampuni ya usalama ya Chainalysis ambayo ilisema mashambulizi ya mtandaoni ya Korea Kaskazini yangeweza kuingiza mali ya kidigitali zenye thamani ya dola milioni 400 mwaka jana.

    Na mnamo mwaka 2019, UN iliripoti kwamba Korea Kaskazini ilikuwa imekusanya takribani dola bilioni mbili kwa programu zake za maangamizi makubwa kwa kutumia mashambulio ya kisasa ya mtandao.

    Korea Kaskazini imepigwa marufuku na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kufanya majaribio ya nyuklia na kurusha makombora ya balistiki.

    Hata hivyo ripoti ya Umoja wa Mataifa inasema licha ya vikwazo ilivyowekewa, Korea Kaskazini imeweza kuendelea kutengeneza miundombinu yake ya nyuklia na makombora ya balestiki.

  12. Viongozi wa Afrika walalamikia 'wimbi la mapinduzi' barani

    th

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Viongozi wa Afrika wamelalamikia "wimbi" la mapinduzi, baada ya kutokea mapinduzi ya kijeshi mara tano katika mwaka uliopita.

    Idadi ya mapinduzi barani Afrika imekuwa ikipungua, kwa ajili ya kuenea kwa chaguzi na uhamishaji wa madaraka kwa njia ya amani.

    Nchi mbili ambazo jeshi limenyakua mamlaka hivi karibuni - Burkina Faso na Mali - zimekuwa zikijitahidi kuzuia uasi wa Kiislamu.

    Wiki iliyopita, kulikuwa na jaribio la mapinduzi nchini Guinea-Bissau, ambalo rais alilaumu magenge ya ulanguzi wa dawa za kulevya.

    Nchi hiyo iko kwenye sehemu kuu ya usafiri kati ya nchi zinazozalisha kokeini katika Amerika ya Kusini na masoko ya Ulaya.

    Wiki iliyopita, Rais wa Ghana Nana Akufo-Addo alisema mapinduzi nchini Mali yamekuwa "ya kuambukiza", na kuwafanya maafisa wa kijeshi katika majirani zake wa Afrika Magharibi, Guinea na Burkina Faso, kuiga mfano huo.

    Wakati mapinduzi ya Afrika Magharibi yakikaribishwa na watu wengi katika nchi hizo, hatua ya jeshi kuchukua madaraka nchini Sudan mnamo Oktoba 2021 imesababisha maandamano makubwa mitaani ya kudai kurejeshwa kwa utawala wa kiraia.

    Haya yamekabiliwa na nguvu zisizo na huruma, ambapo makumi ya waandamanaji wameuawa.

  13. Hujambo na karibu kwa matangazo yetu ya leo ya moja kwa moja.