EU, Amnesty International wataka Bobi Wine aachiwe huru

Umoja wa Ulaya ina wasiwasi juu ya vile wanasiasa pamoja na washikadau wa mashirika ya kiraia wanavyonyanyaswa nchini Uganda.

Moja kwa moja

Asha Juma

  1. Mwanafunzi afukuzwa shuleni kwa kujichora tattoo

    Mteja mwenye tattoo ambaye anataka itolewe

    Mzazi amejipata akiwa katika njia panda baada ya kijana wake wa kidato cha tatu kufukuzwa shuleni kwasababu ya Uchoraji wa chale au tattoo iliyochorwa kwenye mkono wake.

    Akizungumza na gazeti la The Star nchini Kenya, Rosemary amesema ameshutuka utawala wa shule ya kaunti ya Kakamega ulipomrejesha kijana wake nyumbani na kudai kuwa ataruhusiwa tu kurejea shuleni tattoo hiyo itakapoondolewa.

    "Nilipowasili shuleni, niliarifiwa na mkuu wa shule kwamba nitarejea nyumbani na mtoto wangu kwasababu ana tattoo na shule haiwezi kumruhusu mtoto wangu kuendelea na masomo," amesema Rosemaryalipozungumza na gazeti la The Star nchini Kenya.

    Mzazi wa mtoto huyo amesema hakujua kuwa mtoto wake ameweka tattoo hadi siku chache kabla ya shule kufunguliwa.

    Mama huyo amesema kuwa alimuona mtoto wake akificha mkono wake na baada ya kumdadisi akagundua kuwa alichora tattoo ya nyayo yenye jina la mama yake.

    Mama huyo amesema alijaribu kuzungumza na shule lakini hakuna aliyetaka kusikiliza maombi yake na amekuwa akijitahidi kutafuta msaada ila bado hajafanikiwa kwasababu mchakato wa kuondoa tattoo hiyo ni gharama kubwa mno na pia kuna hatari ya mkono wa mtoto wake kupooza na kufura.

    Rosemary amesema sasa alichosalia nacho ni imani tu kuwa shule hiyo itampa mtoto wake adhabu ya kufanya kumuwezesha kuendelea na masomo kwasababu tayari ameshalipa ada.

    Tatoo hutolewa namna gani?

    Mteja akiwa anatolewa tattoo kwa kutumia mashine ya Laser

    Kulingana na mtaalamu Munira wa suala la tattoo nchini Tanzania, tattoo hutolewa kwa mfumo wa laser ambao hutumia miale ya moto na Munira anasema wakati mwingine mtu analazimika kutumia laser mbili tofauti hasa inapotokea kuwa tattoo imechorwakwa wino mweusi na mwekundu na tattoo zenye rangi ya bluu, njano, kijani na nyekundi huhitaji laser tofauti na yenye miale yenye moto mwingi zaidi kuliko tattoo iliyochorwa na wino mweusi.

    Mtaalamu Munira anasema, iwapo mtu ana mzio wa aina yoyote au mtu anatumia vidonge vya uzio kwa takriban miezi sita huwa hawaruhusiwi kupata matibabu ya laser.

    Munira pia ameongeza kuwa mtu mwenye kisukari au virusi vya HIV pia hastahili kutolewa tattoo kwa mfumo huo wa laser.

    Mashine ya Laser

    Mfumo huo wa Laser huvunja vunja wino kwa vipande vidogo na baada ya muda hufanya wino huo kuanza kupotea.

    Mtaalam Munira kuna wakati alitumia matone madogo madogo na miale ya rangi ya kijani na ngozi ya mteja ikaanza kuvimba.

    Utoaji wa tattoo hutolewa kwa hatua tofauti kulingana na jinsi tattoo hiyo ilivyochorwa. Na mtu akitolewa tattoo mara ya kwanza haitoki kabisa bali wino hupungua tu.

    Pia utolewaji wa tattoo kwa kweli si jambo rahisi. Anayetolewa anahitaji kuhimili maumivu.

  2. Kuapishwa kwa Biden: Buhari na Atiku wana imani ya uhusiano mwema kati ya Afrika na Marekani

    Muhammadu Buhari

    Rais Muhammadu Buhari wa Nigeria amepongeza hafla ya kuapishwa kwa rais Joe Biden na makamu wake Kamala Harris nchini Marekani na kuonesha matumaini yake kuwa hatua hiyo ni mwanzo wa uhusiano mwema na ushirikiano na Nigeria pamoja na bara la Afrika.

    Rais Buhari amewapongeza viongozi hao na Marekani kwa ujumla kwa hafla hiyo iliyofanyika kwa amani ambayo inaadhimisha ‘umuhimu wa mwanzo mpya wa kuakisi demokrasia kama mfumo wa serikali na kwa ulimwengu mzima kwa ujumla’.

    Rais Muhammadu amesema yeye na wenzake wamefurahishwa na kuchaguliwa kwa Biden na pia wanajivunia kumuona mwanamke wa kwanza mweusi makamu rais katika historia ya Marekani mwenye asili ya Afrika na Asia.

    Aliyekuwa rais wa Nigeria Atiku Abubakar

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Wakati huohuo, aliyekuwa rais wa Nigeria Atiku Abubakar pia naye ametuma ujumbe wa kheri njema kumpongeza rais wa 46 wa Marekani Joe Biden.

    Bwana Atiku Abubakar ametoa wito kwa rais mpya Joe Biden kuisaidia Nigeria kukabiliana na changamoto za kiusalama.

    Katika ujumbe wake kwenye mtandao wa twitter: Atiku alisema ana imani kuwa ukurasa mpya wa uongozi uliofunguliwa na Marekani, utarejesha heshima na hadhi ya nchi hiyo kama msingi wa demokrasia duniani.

    Ruka X ujumbe
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa X ujumbe

    Kuapishwa kwa Joe Biden kunafuatia wiki kadhaa za vurugu zilizotokea nchini Marekani kwasababu ya rais aliyeondoka madarakani Donald Trump ambaye alipinga matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika Novemba kiasi cha wafuasi wake kuvamia majengo ya bunge mapema mwezi huu.

  3. Kijana amteka nyara baba yake na kudai alipwe fidia

    Nigeria

    Chanzo cha picha, AFP

    Polisi wamemkamata mwanamume, 20, Abubakar Amodu ambaye alipanga njama na genge moja ya kumteka nyara baba yake na akapokea milioni 2 za Nigeria kama fidia.

    Amodu ni miongoni mwa watu 25 waliokamatwa na afisa wa ofisi ya uhusiano mwema katika polisi ya Nigeria, CP Frank Mba, kwa makosa kadhaa waliotekeleza mjini Abuja.

    Kijana huyo aliyekamatwa pamoja na wahalifu wengine, alifaya kazi na baba yake ambaye ni mfugaji.

    Kijana huyo aliwaambia wanahabari kuwa baba yake alikuwa anafuga ngombe na kwamba alipewa ngombe 15 na akaamua kuondoka nyumbani.

    Alitoa ushahidi vile alivyoanza urafiki na genge hilo la wahalifu waliomshauri kumteka nyara baba yake kwasababu hiyo alikuwa njia pekee ya kumuwezesha kutengeneza pesa kwa njia rahisi na kutajirika kwa haraka.

    Kijana huyo anakiri kwamba, binafsi alipokea milioni mbili pesa taslim za Nigeria kama fidia iliyotumwa ili baba yake aachiwe huru.

  4. Wanafunzi washitakiwa kwa tuhuma za kumnyanyasa mwenzao kingono

    DEEPER LIFE HIGH SCHOOL, UYO

    Chanzo cha picha, DEEPER LIFE HIGH SCHOOL, UYO

    Mahakama ya watoto nchini Nigeria kusini mwa mji wa Uyo umeanza kusikiliza kesi ya wavulana wawili ambao wanashutumiwa kwa madai ya kumnyanyasa kingono mwanafunzi wa miaka 11.

    Wanafunzi wawili – wote wenye umri wa miaka 13 – walishitakiwa kwa kutekeleza vitendo vichafu na kwa kumshambulia kijana mdogo kinyume na sheria.

    Walishtakiwa Jumatano pamoja na watu wengine watano wakiwemo walimu na mkuu wa shule ambaye wamesimishwa kazi.

    Hata hivyo wote wamekanusha mashitaka hayo.

    Watu wengine hawakuruhusiwa kuingia mahakamani wakati kesi hiyo inaendelea.

    Mama wa mwathirika alionekana kwenye mitandao ya kijamii mwaka jana akilalamimikia unyanyasaji wa kingono katika shule anayosoma mtoto wake.

  5. Uchaguzi Uganda 2021: Museveni aanza safari ya kushukuru wapiga kura

    Rais Yoweri Museveni amekuwa madarakani kwa miaka 35

    Chanzo cha picha, AFP

    Rais wa Uganda Yoweri Museveni, leo anaanza safari ya kutoka kijijini kwao akielekea mji wa Kampala akiwa anasimama katika vituo kadhaa kwenye miji mbalimbali kutoa shukrani kw wananchi.

    Rais Museveni – aliyeshinda tena uchaguzi wa urais wiki iliyopita ili kuongoza kwa muhula wa sita – atasimama katika vituo saba akiwa njiani kurejea kampala.

    Msemaji wa serikali Ofwono Opondo ameandika taarifa za kina juu ya safari hiyo kwenye mtandao wa Twitter:

    Ruka X ujumbe
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa X ujumbe

    Safari hiyo ya Rais inawadia wakati wito umetolewa kwa serikali kuondoa kifungo cha nyumbani dhidi ya kiongozi wa upinzani Robert Kyagulanyi, maarufu kama Bobi Wine, ambaye anapinga matokeo ya uchaguzi.

    Marekani imetoa wito wa kufanyika kwa uchunguzi katika madai ya wizi wa uchaguzi yaliyoibuliwa na upande wa upinzani ambao bado haujafanikiwa kuwasilisha ombi rasmi la kupinga matokeo.

    Ofisi za upinzani zilivamiwa na jeshi na maafisa wa chama hicho wanasema nyenzo walizokuwa wanazikusanya kwa ajili ya kupinga matokeo ya uchaguzi walinyang’anywa na maafisa hao.

  6. Tanzania yasema haijapata taarifa rasmi ya vikwazo vya Marekani

    Waziri wa mambo ya Nje wa Marekani Mike Pompeo

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Wizara ya Mambo ya Nje ya Tanzania imesema haijapata taarifa rasmi ya maafisa kadhaa wa nchi hiyo kuwekewa vikwazo vya kuingia Marekani.

    Jumanne wiki hii, aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Mike Pompeo alitangaza kuwawekea vikwazo maafisa wa Tanzania ambao hawakutajwa majina kwa kile alichokiita “kuvuruga uchaguzi wa Oktoba 28.”

    Gazeti la Mwananchi la nchini Tanzania hii leo limemnukuu Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Tanzania Emmanuel Buhohela kuwa hawana taarifa rasmi kutoka Marekani juu ya suala hilo.

    “Hatujapata taarifa rasmi zaidi ya kuona katika mitandaoni na hatuwezi kufanyia kazi vitu vya mitandaoni. Wizara yetu ina utaratibu mzuri wa mawasiliano na Balozi na hatujaletewa taarifa rasmi,” Buhohela ameiambia Mwananchi.

    Gazeti hilo pia limemnukuu Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Tanzania (NEC), Jaji Semistocles Kaijage ambaye akisema kuwa maelezo ya taarifa hiyo hayapo wazi na haijaeleza “uchaguzi umeingiliwa kivipi.”

    Soma zaidi:

  7. Mke wa Rais wa Zimbambwe atoa wito wa maombi na kufunga

    Auxillia Mnangagwa alikuwa mama wa taifa wa Zimbabwe November 2017

    Chanzo cha picha, AFP

    Mama wa taifa nchini Zimbabwe ametoa wito kwa wanawake nchini humo kuungana naye katika ibada ya kufunga na maombi kwa siku tatu kwasababu ya janga la virusi vya corona.

    Auxillia Mnangagwa amesema kuwa atafunga na kuomba kuanzia Alhamisi hadi Jumamosi nchini Zimbabwe akiomba "kuepukana na janga hilo".

    Mama wa taifa hilo amesihi wanawake kuhakikisha familia zinazingatia sheria za kuzuia ugonjwa wa corona.

    "Tunahitajika kuwa na mpango madhubuti majumbani kuhakikisha usafi wa mara kwa mara ili kila mmoja nyumbani anajua umuhimu wa kuvaa barakoa sahihi, cha msingi zaidi kuwepo na kuzingatia kila mmoja anakuwa salama na familia kusalia nyumbani," taarifa hiyo inasema.

    Zimbabwe imethibitisha kufariki dunia kwa watu 879 kutokana na virusi vya corona, ikiwemo maafisa wa serikali na wiki hii Waziri wa mambo ya nje Sibusiso Moyo amefariki dunia.

    Nchi hiyo imethibitisha maambukizi 29,408 ya virusi vya corona huku watu 19,253 wakipona.

  8. Jose Chameleone ashindwa uchaguzi wa umeya

    Jose Chameleone

    Lord Meya Erias Lukwago wa chama cha FD ameweza kutetea kiti chake cha Meya wa jiji la Kampala kwa kuwapiku wapinzani wake 10, akiwemo msanii Joseph Mayanja maarufu kama Jose Chameleone na mgombea wa chama cha NUP Nabila Nagayi.

    Msimamizi wa kituo cha kupiga kura Ruwaga kitongoji cha jiji la Kampala ndiye aliyekuwa mhusika mkuu katika uhesabu wa kura kwenye matokeo ya uchaguzi wa meya wa jiji la Kampala.

    ''Ndugu zangu sina cha kuwaambia nina furaha kubwa watu wangu, hapa nyumbani na wakazi wote wa jiji la Kampala asanteni sana, sana''.

    Lukwago ameshinda karibu kata zote tano za wilaya ya Kampala kwa mujibu wa matokeo ya mwanzo yaliotolewa katika kata zote.

    Wakati huo huo Mahakama kuu mjini Kampala leo inatarajiwa kusikiliza ombi la Robert Kyagulanyi kuachiwa huru na vikosi vya ulinzi vinavyomzuia nyumbani kwake.

  9. EU, Amnesty International wataka Bobi Wine aachiwe huru wake

    Bobi

    Umoja wa Ulaya (EU) umesema ina wasiwasi juu ya wanasiasa pamoja na washika dau wa mashirika ya kiraia wanavyonyanyaswa nchini Uganda.

    Taarifa kutoka kwa Baraza la Mawaziri la Umoja wa Ulaya imesema vitendo vya vikosi vya usalama ambavyo havikubaliki vilisababisha vurugu kabla ya uchaguzi.

    Umoja wa Ulaya umetoa wito kwa serikali ya Uganda kuzuia vikosi vyake vya usalama, kuchunguza unyanyasaji na kuwajibisha wote waliokiuka hatia.

    Wakati huohuo, shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limetoa wito kwa mamlaka za Uganda kuagiza polisi na wanajeshi wake kuondoka mara moja katika makazi ya mgombea wa upinzani Bobi Wine ambayo wamekuwa wakiyazingira na kumzuia Bobi Wine pamoja na mke wake Barbara Itungo Kyagulanyi kutotoka nje.

    bob

    Chanzo cha picha, Getty Images

    ‘’Huku ni kukamata watu kiholela’’, Shirika la Amnesty International limesema ikiwa ni siku saba tangu Bobi Wine na mke wake wazuiliwe kutoka nje ya makazi yao.

    Robert Kyagulanyi na mke wake Barbara wamewekewa kifungo cha nyumbani bila kujulishwa makosa yao wala kufikishwa mahakamani.

    ‘’Kuzuiwa kwake kumefanya iwe changamoto kwa Bobi Wine kupinga matokeo ya uchaguzi katika kile ambacho kimejitokeza kuwa njama za kukizuia chama cha NUP kufika mahakamani kwa wakati,” amesema Deprose Muchena, Mkurugenzi wa Amnesty International eneo la Mashariki na Kusini mwa Afrika.

    ''Sio uhalifu kusimama kama mgombea urais wala kutaka kupinga matokeo ya uchaguzi mahakamani. Kuendelea kuzuiliwa kunachochewa kisiasa na ni ukiukaji wa haki za binadamu. Ni lazima kuondolewe mara moja na bila ya masharti yoyote,” Shirika la Amnesty International limesema.

    Polisi wamekuwa wakimzuia Bobi Wine kuondoka nyumbani kwake tangu Ijumaa baada ya kuanza kupinga matokeo ya uchaguzi uliofanyika Januari 14.

    Rais Yoweri Museveni alitangazwa mshindi baada ya kuibuka na asilimia 58.64 ya kura zilizopigwa huku Bobi Wine ambaye ndio mpinzani wake mkuu akipata asilimia 34.83 ya kura.

  10. Hujambo na karibu katika matangazo yetu ya moja kwa moja hii leo ikiwa ni tarehe 21/01/2021