Korea Kusini yaitaka Iran kuonesha msimamo wake kuhusu shambulio dhidi ya meli ya mafuta katika Mlango bahari wa Hormuz
Korea Kusini imeitaka Iran kueleza msimamo wake kuhusu shambulio la hivi karibuni dhidi ya moja ya meli zake za mafuta karibu na Mlango Bahari wa Hormuz.
Kwa mujibu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Korea Kusini, Waziri wa Mambo ya Nje Cho Hyun alizungumza kwa simu na mwenzake wa Iran, na Seoul pamoja na Tehran zitaendelea kuwasiliana na kushauriana ili kuhakikisha usalama wa Mlango wa Hormuz.
Afisa mmoja wa Korea Kusini hapo awali alisema kuwa kuna uwezekano mdogo sana kwamba shambulio hilo lilifanywa na nchi nyingine tofauti na Iran.
Kwa mujibu wa maafisa wa Seoul, meli ya mizigo HMM Namo ilipigwa na “makombora mawili yasiyotambulika” tarehe 4 Mei.
Shambulio hilo liliharibu meli hiyo na kusababisha moto katika chumba cha injini.
Meli hiyo ilikuwa ikisafiri chini ya bendera ya Panama na inaendeshwa na kampuni ya usafirishaji ya Korea Kusini, HMM.
Wizara ya Mambo ya Nje ya Korea Kusini ilitangaza Ijumaa, Mei 15, kwamba imeirejesha meli hiyo iliyoharibiwa nchini humo.
Unaweza kusoma;