Qatar yafungua anga kuruhusu safari chache za ndege

Chanzo cha picha, Getty Images
Qatar imetangaza kuanza tena kwa safari chache za ndege kwa mara ya kwanza tangu vita vilipoanza wiki moja iliyopita.
Mamlaka ya usafiri wa anga ya nchi hiyo ilisema kuwa anga ya Qatar itafunguliwa kwa sehemu ili kuruhusu tu safari za uokoaji na ndege muhimu za mizigo.
Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Hamad umefafanua kuwa safari nyingine katika siku zijazo zitategemea tathmini inayoendelea ya hali ya usalama.
Maafisa wa Qatar walisema mapema wiki hii kuwa jeshi lilifanikiwa kuzuia jaribio la mashambulizi ya Iran dhidi ya uwanja huo wa ndege.
Wizara ya ulinzi iliripoti kuwa Qatar ilidungua ndege tisa zisizo na rubani siku ya Ijumaa.
Moja ya hizo ilianguka katika eneo lisilo na watu bila kusababisha majeruhi.
Pia unaweza kusoma:


