Rais wa Kenya William Ruto anasema jeshi lake la polisi wa
kulinda amani linatarajiwa kuwasili Haiti kusaidia kuzima ghasia za magenge
zinazoongezeka katika kipindi cha takribani wiki tatu.
Katika mahojiano
ya kipekee na BBC, Bw. Ruto alithibitisha timu ilikuwa tayari Haiti na alikuwa
amekutana na polisi wa eneo hilo ili kupata mipango kabla ya wanajeshi wa Kenya
kutumwa.
Maoni ya Bw Ruto
yalitolewa alipohitimisha safari ya siku tatu Washington DC, ikiwa ni ziara ya
kwanza rasmi ya kiserikali nchini Marekani katika zaidi ya miaka 15.
Wakati wa safari yake, Ikulu ya Marekani ilitoa wito wa
kutumwa haraka kwa kikosi cha kimataifa kinachoongozwa na Kenya, baada ya
wanandoa wa Marekani kutajwa miongoni mwa wamishonari watatu waliouawa nchini
Haiti siku ya Ijumaa.
"Nina timu tayari Haiti ninapozungumza nawe," Bw
Ruto aliiambia BBC Ijumaa.
"Hiyo itatupa sura ya jinsi mambo yanavyoonekana
ardhini, uwezo unaopatikana, miundombinu ambayo imewekwa."
Aliongeza: "Tunapopata tathmini hiyo tuliyokubaliana na
polisi wa Haiti na uongozi wa Haiti, tunaangalia upeo wa kati ya wiki tatu na
pale kuhusu sisi kuwa tayari kupeleka, mara kila kitu kitakapowekwa. "
Mwaka jana, Kenya ilijitolea kuongoza kikosi cha usalama cha
kimataifa kinachoungwa mkono na Umoja wa Mataifa kurejesha utulivu katika
kisiwa cha Caribbean.
Magenge yamechukua sehemu kubwa ya Haiti, na kuleta vurugu
na uharibifu katika jiji lake kuu lililozingirwa, Port-au-Prince kufuatia
mauaji ya Rais Jovenel Moïse mnamo Julai 2021.
Siku ya Ijumaa, wamishonari wawili wa Marekani waliuawa huko
Haiti na magenge.
Bw Ruto aliambia BBC kwamba matukio ya aina hii ndiyo
"hasa" sababu nchi yake ilikuwa inajiandaa kutuma jeshi lake la
polisi.
"Hatupaswi kupoteza watu. Hatupaswi kuwa tunapoteza
wamisionari," alisema.
"Tunafanya hivi ili kuzuia watu zaidi kupoteza maisha
kwa magenge."
Marekani pia ni sehemu ya muungano wa mataifa mbalimbali
unaofanya kazi na Kenya.
"Hali ya usalama nchini Haiti haiwezi kusubiri,"
alisema msemaji wa Baraza la Usalama la Kitaifa siku ya Ijumaa.
Walisema Rais Joe Biden aliahidi kuunga mkono "haraka
ya kutumwa kwa jeshi" katika mazungumzo yake na Rais Ruto.
Bw Ruto alisema kuwa kambi ambapo wanajeshi na vifaa
vitahifadhiwa, inayojengwa kwa ushirikiano na Marekani, inakaribia kwa "70%
kukamilika".