Moja kwa moja, Israel yasema iko tayari kuendelea na vita na Iran "kwa muda mrefu iwezekanavyo

Katika taarifa mpya kutoka kwa msemaji wa jeshi Avichay Adraee, amesema Hezbollah imeanzisha operesheni mpya, na Israeli itajibu.

Muhtasari

Moja kwa moja

Na Asha Juma

  1. Mafuta yafikia dola 100 kwa pipa licha ya makubaliano ya kutoa kiasi kikubwa cha akiba

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Bei ya mafuta imeendelea kupanda siku ya Alhamisi licha ya nchi husika kukubali kutoa kiasi kikubwa cha mafuta kutoka akiba yao ya dharura wanapojaribu kupunguza athari za vita vya Iran.

    Mafuta ghafi yalipanda kwa karibu 9% hadi kufikia dola 100 ($74.79) kwa pipa moja barani Asia hata baada ya wanachama wote 32 wa Shirika la Nishati la Kimataifa (IEA) kusema watatoa mapipa milioni 400 kutokana na wasiwasi wa usambazaji.

    Siku ya Jumatano, Iran ilionya kwamba mafuta yanaweza kufikia dola 200 kwa pipa huku mashambulizi yake dhidi ya meli yakizidi katika Mlango-Bahari wa Hormuz, njia muhimu ya maji kwa usafirishaji wa mafuta.

    Msemaji wa Kikosi cha Revolutionary Guard Corps (IRGC) alisema meli yoyote inayohusiana na Marekani, Israel au washirika wao italengwa.

    Soma zaidi:

  2. Mashambulizi ya meli eneo la Ghuba yaongezeka

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Mamlaka ya Ulinzi wa Raia na ambulensi ya Oman inazima moto uliotokea kwenye maeneo kadhaa ya kuhifadhia mafuta katika bandari ya Salalah, vyombo vya habari vya serikali vinasema.

    Vyombo hivyo vilisema kwamba maeneo ya mafuta yalishambuliwa na ndege zisizo na rubani.

    Operesheni za kuzima moto ziliendelea, Shirika la Habari la Oman linaloendeshwa na serikali liliripoti, lakini "huenda ikachukua muda" kuudhibiti moto huo.

    Mamlaka ya Iraq yasema mtu mmoja amefariki baada ya meli za mafuta kushambulia

    Milipuko imeripotiwa kwenye meli mbili za mafuta za kigeni katika Ghuba ya Uajemi karibu na bandari ya Basra.

    Mkuu wa Kampuni Kuu ya bandari za Iraq anasema imewaokoa wafanyakazi 38 kutoka kwenye meli hizo, na mtu mmoja amefariki, katika maoni yaliyonukuliwa na shirika la habari la Iraq. Shughuli za utafutaji na uokoaji zinaendelea.

    Tovuti za kufuatilia meli zinaonyesha meli mbili za mafuta zinazoshukiwa kushambuliwa zikiwa zimezungukwa na boti za uokoaji.

    Chanzo cha usalama cha Iraqi huko Basra kiliambia CNN kwamba boti ya Iran iliyojaa vilipuzi inadhaniwa kushambulia meli hizo mbili, hata hivyo, chanzo hicho kiliongeza kuwa uchunguzi unaendelea.

    Mamlaka ya Iraq yasema bandari za mafuta zimesimamisha shughuli zake kufuatia shambulio hilo.

    Hapo awali, jeshi la wanamaji la Oman liliwaokoa mabaharia 20 kutoka kwenye meli yenye bendera ya Thailand iliyoshambuliwa katika Mlango-Bahari wa Hormuz, yapata maili 13 za baharini (kilomita 24) kutoka pwani ya Oman, kulingana na shirika la habari la serikali la nchi hiyo.

    Soma zaidi:

  3. Israel yasema iko tayari kuendelea na vita na Iran "kwa muda mrefu iwezekanavyo

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Msemaji wa jeshi la Israeli amesema kwamba nchi hiyo iko tayari kuendelea na vita na Iran "kwa muda mrefu iwezekanavyo", Reuters inaripoti.

    Jeshi la Israeli limefanya kile inachokiita wimbi kubwa la mashambulizi kote Beirut jioni hii.

    Katika taarifa mpya kutoka kwa msemaji wa jeshi Avichay Adraee, amesema Hezbollah imeanzisha operesheni mpya, na Israeli itajibu.

    Viongozi wa Israeli wasema vita vinaweza kuendelea kwa muda usiojulikana

    Ni hisia ambayo imeonekana kutoka kwa maafisa wengi wa Israeli kufikia sasa, ikiwa ni pamoja na taarifa kutoka kwa Waziri wa Ulinzi Israel Katz, ambaye alisema kwamba vita "vitaendelea bila kikomo cha muda wowote".

    Katz alisema mzozo huo utaendelea kwa muda mrefu iwezekanavyo, na hadi malengo yote ya operesheni ya pamoja ya Israeli na Marekani yatakapotimia, kulingana na Reuters na The Times of Israel.

    Soma zaidi:

  4. Hujambo msomaji wetu. Karibu katika matangazo yetu mubashara ya tarehe 12/03/2026.