Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Vifo vya watu 11 vilivyotokana na moto vyathibitishwa na mamlaka za LA

Jumla ya vifo 11 vinavyohusiana na moto vimethibitishwa na Mkaguzi wa kitabibu wa Kaunti ya Los Angeles.

Muhtasari

  • GazaIdadi ya waliouawa vitani Gaza huenda ikawa kubwa zaidi, watafiti wasema
  • Kandanda'Ni kama mechi ya fainali ya kombe la mabingwa'
  • 'Baba yangu anapaswa kufa gerezani' bintiye Dominique Pelicot aiambia BBC
  • Israel na GazaWalowezi wa Israel katika ukingo wa magharibi wauona ushindi wa Trump kama fursa
  • Moto wa nyika Vifo vya watu 11 vilivyotokana na moto vyathibitishwa na mamlaka za LA

Moja kwa moja

Lizzy Masinga

  1. Idadi ya waliouawa vitani Gaza huenda ikawa kubwa zaidi, watafiti wasema

    Idadi ya watu waliouawa katika vita vya Gaza, huenda ikawa kubwa zaidi. Haya ni kwa mujibu wa takwimu rasmi zilizoripotiwa na wizara ya afya inayosimamiwa na kundi la Hamas.

    Takwimu hizo zimechapishwa katika jarida la masuala ya matibabu la Lancet. Tathmini hiyo iliyoongozwa na wataalamu kutoka Uingereza, imeangazia miezi tisa ya kwanza ya vita hivyo, ambavyo vilianza punde tu baada ya kundi la Hamas kushambulia Israel mnamo Oktoba 7 2023.

    Watafiti walitumia data kutoka kwa wizara ya afya ya Palestina, kwa pamoja na kutoka kwa Tathmini nyingine iliyochapishwa katika mitandao iliyoangazia taarifa za jamaa za waliofariki, na vile vile matangazo ya vifo. Ilikadiria kwamba hadi tarehe 30 Juni 2024- Wapalestina 64,260 walifariki baada ya kupata majeraha mabaya, kumaanisha kwamba viwango vya kuripoti vifo rasi vilikuwa hcini na asilimia 41.

    Ubalozi wa Israel nchini Uingereza, umesema kwamba ‘taarifa zozote zinazotokea ndani ya Gaza haziwezi kuaminiwa,’ na kuwasilishwa na Hamas. Umoja wa mataifa umetumia taakwimu za wizara hiy na kuzitaja kama halisi na sawa.

    Takwimu za wizara hiyo hazitofautishi kati ya wapiganaji na raia, ila ripoti ya hivi karibuni ya umoja wa mataifa imesema kwamba idadi kubwa ya vifo vilivyothibitshwa ni vya waathiriwa wa kike na watoto. Israel imesema kwamba takwimu za Hamas haziwezi kuaminika.

    Mwezi agosti, jeshi la Israel lilisema kwamba lilikuwa limewamaliza magaidi 17,000, japo haijabainika wazi jinsi idadi hii ilivyofikiwa.

    Jeshi hilo la IDF linasisitiza kwamba linawalenga wapiganaji pekee na linajaribu kupunguza idadi ya raia wanaouawa katika mashambulizi yake.

    Watafiti kutoka Chuo cha London school of Hygiene and Tropical Mdicine waliangalia ni watu wangapi walijitokeza zaid ya mara moja walipokuwa wakihesasbu idadi ya waliofariki vitani.

    Viwango vya kupishana katika takwimu hizo vinaashiria kwamba idadi ya waliofariki moja kwa moja kutokana na majeraha mabaya katika vita hivyo huenda ikawa kubwa zaidi ya takwimu zilizotolewa na hospitali;takwimu ambazo zilichapishwa na wizara ya afya.

    Wizara ya afya ya Gaza, hutoa taarifa mpya ya jumla ya waliofariki katika vita hivyo, kila siku. Hujumlisha takwimu hizo za vifo kutoka kwa hospitali mbalimbali na vile vile taarifa za vifo zinazotolewa na familia na vile vile taarifa kutoka kwa vyombo vya habari vinavyoaminika.

    Ripoti ya Lancet, inakadiria kwamba idadi ya jumla ya wlaiofariki huenda ikawa kati ya watu 55,298 na 78,528 ikilinganishwa na 37,877 iliyochapishwa na wizara ya afya.

    Takwimu za ripoti hii zinaonyesha kwamba idadi hii ni kubwa zaidi, au huenda ikwa ya chini kulingana na taarifa za kina za Tathmini. Taarifa hiyo pia inasema kwamba asilimia 59 ya wlaiouawa , ni wanawake na watoto na watu wazee.

    Vita vya gaza vimechochewa na shambulizi la Hamas nchini Israel ambapo watu 1200 waliuawa na wengine 251 kutekwa nyara na kuzuiliwa Gaza.

    Israel ilinzisha operesheni kali ya kivita kujibu hatua hiyo ya Hamas. WIzara ya afya, imesema kwamba watu 46,006 wengi wao wakiwa raia wameuawa katika shambulizi hilo la Israel.

    Unaweza kusoma;

  2. ‘Ni kama mechi ya fainali ya kombe la mabingwa’

    Arne Slot huenda ni mgeni kwa mashindano ya kombe la FA, lakini anafahamu vyema kwamba mechi ya leo ni jambo kubwa, hasa kwa mashabiki na wachezaji wa klabu ya soka ya Accrington Stanley.

    ‘Ni wakati muhimu sana kila mechi na timu tunayocheza dhidi yake, lakini kwa sababu timu hii ni ya daraja la chini, “Slot alisema alipozungumza na wanahabari katika uwanja wa mazoezi wa klabu hiyo, siku ya Ijumaa. “watajikakamua.

    Wanajiandaa kwa mechi kama hii kwa wiki kadhaa sasa.

    ‘Unapojiandaa kucheza katika fainali ya ligi ya mabingwa, kila mmoja huwa na hamu kubwa na wako tayari. Na kwa vijana hawa , wanahisi mechi hii ni kama fainali ya ligi ya mabingwa, na kwa hivo tune uelewa mkubwa kulihusu jambo hilo.’ ‘Mara tisa kati ya kumi, dakika 25 za kwanza au nusu saa ndizo za muhimu kabisa na ni ngumu katika mechi kwa sababu watakuwa bado na wasiwasi mkubwa.

    ‘Ni kibarua kwetu kuwa tayari kukabiliana na Liverpool, na kucheza mechi bora kabisa kuzidi mengine yote maishani mwetu,’ Waandishi wa spoti wa BBC wanatabiri kwamba mechi hiyo itakwisha 4-0 kwa upane wa Liverpool.

    Mwandishi Chris Sutton anasema kwamba japo mechi hii ni kubwa sana kwa timu ya Accrington, huwezi kuwateta sana kushinda dhidi ya klabu inayoongoza jedwali la ligi kuu ya England, hata wakiwasilisha kikosi chao bora kabisa dhidi ya Liverpool.

  3. ‘Baba yangu anapaswa kufa gerezani’ bintiye Dominique Pelicot aiambia BBC

    Ilikuwa mwendo wa mbili unusu, usiku wa jumatatu Novemba 2020 ambapo Caroline Darian alipokea simu ambayo ilibadili kila kitu.

    Kwenye upande wa pili wa simu hiyo, alikuwa mama yake Gisele Pelicot. “Aliniambia kwamba aligunduwa asubuhi hiyo kwamba baba yangu Dominique alikuwa anampa dawa kwa muongo mmoja, kwa ajili ya kuwapa wanaume tofauti uwezo wa kumbaka,”

    Dariana anakumbuka haya akimuelezea kwa undani mtangazaji Emma Barnett katika mahojiano ya kipekee na kituo cha redio cha BBC Radio 4 .

    “Kwa wakati huo, Nilipoteza hali niliyoifahamu ya kawaida maishani mwangu,” asema Dariana ambaye sasa ni mwenye umri wa miaka 46. “Ninakumbuka, nilipiga kelele, nikalia, n ahata nikamtusi baba,” alisema. “ Ilikuwa kama , tetemeko la ardhi ana Tusnami imenikuta.”

    Dominique Pelicot alihukumiwa kifungo cha miaka 20 gerezani, baada ya kupatikana na hatia mwishoni mwa kesi ambayo imetambulika kama ya kihistoria iliyosikizwa kwa miezi mitatu unusu mwaka wa 2024.

    Zaidi ya miaka minne baadaye, Darian anasema kwamba baba yake anapaswa ,” Kufa akiwa gerezani.”

    Wanaume Hamsini, ambao Dominique Pelicott aliwasajili kupitia mitandao, ili kumdhulumu kingono mke wake Gisele ambaye alikuwa amepoteza fahamu pia walihukumiwa kifungo cha gerezani.

    Alikamatwa na polisi baada ya kupatikana akirekodi kisiri ndani ya mavazi ya wanawake katika duka kuu moja, hali iliyowaelekeza polisi kupanua uchunguzi wao dhidi yake.

    Kwenye kompyuta ndogo ya kupakata ya mzee huyo na hata kwenye simu yake ya mkononi, polisi walipata malefu ya video na picha za mke wake Gisele, akiwa amepoteza fahamu na akibakwa na watu wasiojulikana.

    Mbali na kuangazia masuala ya kubakwa na dhuluma za kijinsia , kesi hiyo iliangazia pia suala dogo la kutumia kemikali yaani dawa kudhulumu mtu.

    Caroline Darian, amejitolea kupambana na dhuluma ya aina hiyo ya kutumia kemikali kumuumiza muathiriwa , hali ambayo japo inatumika kuwadhuru waathiriwa wengi hairipotiwi kwa ukubwa kwa sababu wengi hawana ufahamu kuhusu dhuluma waliyopitia na huenda wakakosa kuelewa kwamba hata walipewa dawa ya kuwadhuru.

  4. Walowezi wa Israel katika ukingo wa magharibi wauona ushindi wa Trump kama fursa

    Katika siku ambayo hali ya anga iko sawa, majumba marefu yaliyopo Jijini Tel Aviv yanaonekana vizuri kutoka kwa mlima uliojuu ya Karnei Shomron, ambapo ni makazi ya walowezi wa Israel katika eneo lililokaliwa la Ukingo wa magharibi.

    “Ninahisi tofauti kati ya hapa na Tel Aviv,” amesema Sondra Boras, ambaye ameishi katika mtaa wa Karnei Shomron kwa takriban miaka 40. “Ninaishi katika eneo ambalo mababu zangu wa zamani waliishi kwa zaidi ya miaka elfu moja iliyopita. Siishi katika eneo lililokaliwa; Ninaishi katika eneo lililotambuliwa katika bibilia la Judea na Samaria.”

    Kwa walowezi wengi wanaoishi hapa, hawatofautishi kati ya taifa la Israel nae neo ambalo taifa hilo ilinyakua kutoka Jordan katika vita vya mashariki ya kati vya 1967.

    Suala hili limefutika kutoka kwenye mtazamo na matamshi yao.

    Kulingana na malelezo ya wageni yaliyorekodiwa katika eneo la juu la mlimani, linaelezea ukingo wa magharibi kama eneo ambalo lipo chini ya himaya ya Israel, na kwamba mji wa Kipalestina wa Nablus, ni eneo ambalo Mwenyezi Mungu aliwaahidi wa Israeli kuwa ardhi yao.

    Ila, kukatwa rasmi kwa eneo hili kumesalia kuwa ndoto kwa sasa kwa walowezi kama Sondra, japo makazi ya walowezi, yanatajwa kama makazi haramu na mahakama ya juu kabisa ya umoja wa mataifa na vilevile baadhi ya mataifa duniani, yamezidi kuongezeka mwaka baada ya mwaka.

    Sasa wengi wanaona fursa ya kuendelea mbele, kufuatia uchaguzi wa Donald Trump kama Rais wa Marekani. “ Nilifurahi sana kwamba Trump alishinda uchaguzi wa Urais,” Sondra aliiambia BBC.

    Ningependa sana kupanua Utaifa wa Judea na Samaria. Na ninahisi, kwamba ni jambo ambalo Trump ataliunga mkono.

    Kuna ishara kwamba baadhi katika serikali ya Trump inayoingia madarakani huenda wakakubaliana na Sondra.

    Mike Huckabee, ambaye ameteuliwa kuhudumu kama Balozi wa Marekani nchini Israel, ameashiria kwamba anaunga mkono madai ya Israel kuhusu Ukingo wa Magharibi katika mahojiano yaliyofanyika mwaka jana.

    “Wakati watu wanatumia neno ‘KUKALIWA”, ninasema : “Ndio, Israel inakalia ardhi hiyo, lakini ni hali ya kukalia ardhi ambayo Mwenyezi Mungu mwenyewe aliwapa miaka 3500 iliyopita. Ni ardhi yao, “Alisema.

    Unaweza kusoma;

  5. Vifo vya watu 11 vilivyotokana na moto vyathibitishwa na mamlaka za LA

    Jumla ya vifo 11 vinavyohusiana na moto sasa vimethibitishwa na Mkaguzi wa Matibabu wa Kaunti ya Los Angeles.

    Katika taarifa yake ya Ijumaa alasiri, mchunguzi wa kitabibu alisema vifo vitano vilitokea katika moto wa Palisades, na wengine sita kutokana na moto wa Eaton.

    Vifo hivyo vilitokea Altadena, Malibu, Pacific Palisades na Topanga.

    Hakuna taarifa zaidi kuhusu kutambuliwa kwa waathiriwa, ingawa waathiriwa wengine walitambuliwa kupitia vyanzo vingine.

  6. Habari za asubuhi, karibu katika taarifa zetu