Urusi yawakamata waandishi wengine wawili - Ripoti
Urusi imeripotiwa kuwakamata wanahabari wawili ambao wamekuwa wakifanya kazi na vyombo vya habari vya kimataifa.
Sergei Karelin, raia wa Urusi na Israel, alizuiliwa siku ya Ijumaa, shirika la habari la Associated Press liliripoti.
Hapo awali amefanya kazi na shirika hilo la habari. Anashutumiwa kwa vitendo vya "itikadi kali" kuhusiana na madai ya kazi katika wakfu wa kiongozi wa upinzani marehemu Alexei Navalny, mashtaka anayokanusha.
Siku moja mapema, Konstantin Gabov aliwekwa kizuizini kwa mashtaka kama hayo.
Bw.Gabov amefanya kazi na vyombo vya habari vya kigeni ikiwa ni pamoja na Reuters.
Wanaume wote wawili wanakabiliwa na kifungo cha chini cha miaka miwili jela iwapo watapatikana na hatia ya "kushiriki katika shirika lenye itikadi kali".
Hao ndio waandishi wa habari wa hivi karibuni kukabiliwa na mashtaka huku kukiwa na ukandamizaji uliokithiri nchini Urusi, ambao umeshuhudia uhuru wa vyombo vya habari kuwa mdogo. "Shirika la habari la Associated Press linasikitishwa sana na kuzuiliwa kwa mwandishi wa habari wa video wa Urusi Sergey Karelin," shirika la habari la Marekani lilisema katika taarifa yake. "Tunatafuta maelezo ya ziada."
Bw Karelin na Bw Gabov wanatuhumiwa kusaidia kuandaa video za chaneli ya YouTube ya Bw Navalny, ambaye kwa miaka mingi alikuwa mkosoaji mkubwa wa Rais wa Urusi Vladimir Putin kwa miaka mingi.
Bw Navalny alikufa mnamo Februari katika gereza la Arctic ambapo alikuwa amefungwa.
Mnamo 2021, mashirika yaliyohusishwa na Bw Navalny yalipigwa marufuku wakielezwa kuwa "wasimamizi wenye msimamo mkali", kumaanisha wale wanaowaunga mkono wanakabiliwa na kifungo jela.
Mwandishi wa habari wa Forbes Russia, Sergei Mingazov, pia alikamatwa wiki hii.Anashutumiwa kwa kukosoa jeshi la Urusi.
Mnamo 2022 Urusi ilipitisha sheria inayoweka kifungo cha hadi miaka 15 jela kwa kueneza habari "ghushi" kuhusu jeshi.
Unaweza kusoma;