Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Kosovo: Waziri mkuu arushiwa maji bungeni kabla ya vita kuzuka kati ya wabunge
Wabunge walirushiana makonde baada ya Waziri mkuu wa Kosovo kurushiwa maji na picha yake kukatwa na mbunge wa upinzani ndani ya bunge la Kosovo.
Ghasia hizo zilizuka kufuatia mjadala mkali wa siku tatu kuhusu machafuko kaskazini mwa Kosovo.
Waziri Mkuu Albin Kurti alikuwa akihutubia bunge wakati ghasia hizo zilipozuka